• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
    • eVibali |
Shinyanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Shinyanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Yetu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
      • Afya
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Shinyanga
    • Wilaya ya Kahama
    • Wilaya ya Kishapu
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu
    • Halmashauri ya Mji wa Kahama
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu
    • Halmashauri ya Wilaya ya Msalala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
    • Bandari Kavu
  • Huduma
    • Kutoa Ushauri wa Kitaalam
    • Kutafsiri Sheria na Sera
    • Kuratibu Shughuli za Wadau
    • Ulinzi na Usalama
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Tafiti
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha

RC MNDEME AIPONGEZA MSALALA KWA USIMAMIZI MZURI WA FEDHA ZA SERIKALI

Posted on: December 13th, 2023

MKUU wa Mkoa wa Shinyanga Mhe. Christina S. Mndeme ameipongeza Halmashauri ya Wilaya ya Msalala kwa ujenzi bora wa shule ya sekondari Kakola iliyogharimu zaidi ya Tzs. Mil. 603 pamoja na shule ya msingi Bulyanhulu iliyogharimu Mil 561 huku akiridhishwa sana kwa namna walivyosimamia matumizi ya fedha za serikali.

RC Mndeme ameyasema hayo leo tarehe 12 Desemba, 2023 alipokuwa kwenye ziara ya ukaguzi wa miradi ya maendeleo katika Halmashauri ya wilaya ya ushetu huku akimpongeza sana Mwenyekiti wa Halmashauri ya Msalala Mhe. Mibako Mabubu, waheshimiwa madiwani wote, Mbunge wa Jimbo la Msalala Mhe. Iddi Kassim kwa usimamizi na ufuatiliaji mzuri wa fedha za serikali zinazotolewa na serikali ya Rais Mhe. Samia Suluhu Hassan kwa lengo la kuwasogezea huduma wananchi wa msalala na shinyanga kwa ujumla.

"Kwa dhati ya moyo wangu, niwapongeze sana Msalala kwa kazi nzuri ya ujenzi wa shule hizi mbili zenye kuvutia na zenye kuonesha uhalisia wa thamani ya fedha, huu ndiyo usimamizi mzuri wa fedha za serikali unaotakiwa,

", alisema RC Mndeme.

Kando na pongezi hizi, RC Mndeme amesema kuwa, uwepo wa wawekezaji nchini unatokana na mazingira bora na wezeshi kwa wawekezaji yaliyowekwa na Rais Skr. Samia Suluhu Hassan na ndiyo sababu mnaona wapo na wataendelea kuweko Barrick hapa Msalala.

Ziara ya RC Mndeme imejumuisha ukaguzi na uwekaji wa mawe ya msingi katika mbalimbali Msalala ambapo ameweka jiwe la msingi katika jengo la watumishi wa msalala, usambazaji wa umeme wa REA kijiji cha Bunva.

Miradi mingine ni ujenzi wa jengo la wodi maalum la huduma za haraka (Fast Truck), kisha alikagua sekondari ya wasichana Busurulwanhulu inayojengwa na Barrick fedha za mrejesho wa faida kwa umma utokanao na mapato ya mgodi na mwisho akahitimisha na shule.

Kesho tarehe 13 RC Mndeme ataendelea na ziara yake katika Manispaa ya Kahama ambapo pamoja na mambo mengine lakini pia atatembelea na kukagua kituo uwezeshaji Mondo, kutembelea na kukagua kituo cha uwezeshaji Mwendakulima na kuwasha umeme kijiji cha Kahanga kata ya Wendele hapa Kahama.


HABARI PICHA


Matangazo

  • No records found
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • WANUFAIKA WA MIKOPO YA 10% LIPENI KWA WAKATI ILI PIA VIKOPESHWE NA VIKUNDI VINGINE - RC MACHA

    February 13, 2025
  • CP. HAMDUNI AKUTANA NA KAMATI YA MICHEZO YA JWTZ

    February 13, 2025
  • WANANCHI, LIPENI KODI YA ARDHI KWA WAKATI MUEPUKE RIBA - LEO KOMBA

    February 12, 2025
  • WAJUMBE WA BODI, TUMIENI TAALUMA ZENU KUISAIDIA HOSPITALI KUKAMILISHA MIRADI YA UJENZI- RAS CP. HAMDUNI.

    February 11, 2025
  • Angalia zote

Video

MIFUKO BANDIA ZAIDI YA ELFU 20 YAKAMATWA SHINYANGA
Video Nyinginezo

Viunganishi vya Haraka

  • Historia
  • Dira na Dhima
  • Hotuba Mbalimbali
  • Video Mbalimbali
  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Picha za Matukio
  • Miongozo na kanuni

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Mfumo wa kutuma, kupokea na kufuatilia malalamiko, mapendekezo, maulizo na pongezi
  • Ofisi ya Rais Menejimenti ya utumishi wa Umma
  • Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Boma Street, Mwanza Road

    Anuani: P.O.Box 320, Shinyanga

    Simu: +255 28 2762222

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras@shinyanga.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2018. Mkoa wa Shinyanga. Haki zote zimehifadhiwa