• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
    • eVibali |
Shinyanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Shinyanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Yetu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
      • Afya
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Shinyanga
    • Wilaya ya Kahama
    • Wilaya ya Kishapu
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu
    • Halmashauri ya Mji wa Kahama
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu
    • Halmashauri ya Wilaya ya Msalala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
    • Bandari Kavu
  • Huduma
    • Kutoa Ushauri wa Kitaalam
    • Kutafsiri Sheria na Sera
    • Kuratibu Shughuli za Wadau
    • Ulinzi na Usalama
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Tafiti
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha

RC MNDEME AITAKA SINOHYDRO CO. LTD KUKAMILISHA MRADI KWA WAKATI

Posted on: October 29th, 2023

Na. Shinyanga RS.

MKUU wa Mkoa wa Shinyanga Mhe. Christina Solomon Mndeme ameitaka kampuni Sinohydro Company Limited iliyopewa kandarasi ya kujenga Mradi wa Umeme wa Jua wenye thamani ya zaidi ya Bilioni 323 unaotekelezwa katika kijiji cha Ngunga Wilaya ya Kishapu hapa mkoani Shinyanga kukamilisha ujenzi huu kwa wakati, kwa kuzingatia ubora, viwango, muda waliokubaliana na bila kuongeza bajeti ili wananchi waanze kunufaika na huduma ya uhakika ya umeme.

Mhe. Mndeme amemuagiza Mkandarasi huyu leo tarehe 29 Oktoba, 2023 alipokuwa akizungumza na wadau wa mradi huu, baadhi ya wananchi waliopisha mradi huu kijijini Ngunga, viongozi mbalimbali, pamoja na watumishi kutoka taasisi mbalimbali ikiwemo Tanesco huku akimsisitiza kutoa kipaumbele cha ajira kwa vijana wa ngunga, kishapu na shinyanga kwa ujumla katika mradi huu muhimu.

"Nikuombe (Sinohydro Co. Ltd) mkandarasi uliyepewa dhamana ya kujenga mradi huu mkubwa wa umeme hapa kijiji cha ngunga Kishapu, ukamilishe mradi huu kwa wakati na kwa kuzingatia muda, viwango, thamani na bajeti tuliyokubaliana ili wananchi waanze kunufaika na uwepo wa mradi huu," alisema Mhe. Mndeme.

Awali akiwakaribisha wadau wa mradi huu ambao ni Shirika la Maendeleo la Ufaransa AFD group - Dar es salaam Agency  Mndeme aliwaeleza kuwa serikali itafanya kazi nao bega kwa bega, itawapatia ushirikiano wakati wote na pia aliwashukura sana kwa ujio wao kuja kuona eneo litakalotekelezwa mradi huu mkubwa wa umeme.

Mhe. Mndeme kipekee kabisa alimshukuru sana Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kufanikisha mradi huu mkubwa wa umeme ha hasa kuja kutekelezwa katika kijiji cha ngunga kilichopo Wilaya ya Kishapu hapa mkoani Shinyanga, mradi wenye thamani ya zaidi ya Bilioni 323 fedha za kitanzania.

Kwa upande wake Eng. Emmanuel Anderson kutoka Tanesco na ambaye ndiye mhandisi na msimamizi wa mradi huo kwa (MW 50) Ngunga - Kishapu alisema kuwa mradi huu utatekelezwa ndani ya miezi 14 na kwamba mkandarasi yupo tayari na sasa iliyobakia ni kuanza kazi tu.


HABARI PICHA




Matangazo

  • No records found
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • WANUFAIKA WA MIKOPO YA 10% LIPENI KWA WAKATI ILI PIA VIKOPESHWE NA VIKUNDI VINGINE - RC MACHA

    February 13, 2025
  • CP. HAMDUNI AKUTANA NA KAMATI YA MICHEZO YA JWTZ

    February 13, 2025
  • WANANCHI, LIPENI KODI YA ARDHI KWA WAKATI MUEPUKE RIBA - LEO KOMBA

    February 12, 2025
  • WAJUMBE WA BODI, TUMIENI TAALUMA ZENU KUISAIDIA HOSPITALI KUKAMILISHA MIRADI YA UJENZI- RAS CP. HAMDUNI.

    February 11, 2025
  • Angalia zote

Video

MIFUKO BANDIA ZAIDI YA ELFU 20 YAKAMATWA SHINYANGA
Video Nyinginezo

Viunganishi vya Haraka

  • Historia
  • Dira na Dhima
  • Hotuba Mbalimbali
  • Video Mbalimbali
  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Picha za Matukio
  • Miongozo na kanuni

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Mfumo wa kutuma, kupokea na kufuatilia malalamiko, mapendekezo, maulizo na pongezi
  • Ofisi ya Rais Menejimenti ya utumishi wa Umma
  • Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Boma Street, Mwanza Road

    Anuani: P.O.Box 320, Shinyanga

    Simu: +255 28 2762222

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras@shinyanga.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2018. Mkoa wa Shinyanga. Haki zote zimehifadhiwa