• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
    • eVibali |
Shinyanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Shinyanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Yetu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
      • Afya
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Shinyanga
    • Wilaya ya Kahama
    • Wilaya ya Kishapu
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu
    • Halmashauri ya Mji wa Kahama
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu
    • Halmashauri ya Wilaya ya Msalala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
    • Bandari Kavu
  • Huduma
    • Kutoa Ushauri wa Kitaalam
    • Kutafsiri Sheria na Sera
    • Kuratibu Shughuli za Wadau
    • Ulinzi na Usalama
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Tafiti
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha

RC MNDEME AKUTANA NA WATAALAM WA AFYA - SHINYANGA

Posted on: November 18th, 2023

Na. Shinyanga RS.

MKUU wa Mkoa wa Shinyanga Mhe. Christina S. Mndeme leo katika ofisi yake amekutana na wataalam wa afya mkoa na kupanga namna ambavyo wataifanya kampeni ya utoaji chanjo ya Minyoo ya Tumbo na Kichocho kwa watoto takribani 752, 877 kwa mkoa ambapo walengwa ni watoto wenye umri wa miaka 5 - 14 huku akitoa wito kwa wazazi na wananchi wote kwa ujumla kupeleka wwtoto katika vituo vitakvyoteuliw ili waweze kupata chanjo hii na kwamba hana madhara yoyote kwa wototo.

Hili ni zoezi ambalo mkoa unatarajia kutoa Kinga Tiba ya dawa za Kichocho na Minyoo ya Tumbo, kwa watoto wenye umri wa miaka 5-14, wapatao 752,877 katika Kampeni ambayo itafanyika Novemba 24 mwaka huu.

"Tumekutana hapa kwa lengo la kupanga namna gani twende kuttekeleza kampeni hii ya utoaji chanjo ya minyoo ya tumbo na kichocho kwa watoto 752, 877 kwa mkoa mzima ambapo watoto 286, 782 ni kichocho na 466, 095 chanjo ya minyoo ya tumbo kubwa zaidi na muhimu ni kwamba chanjo hii haina madhara yoyote na haiuzwi inatolewa bure kabisa hivyo wazazi wapeleke watoto wao siiu ikifika", alisema Mhe. Mndeme.

Katika kikao hiki cha Uraghabishi kwa ajili ya Maandalizi ya Kampeni hii ya kutoa kinga tiba ya dawa hizi za Kichocho na Minyoo ya Tumbo tutatoa Kinga tiba kwa watoto 286,782 ambao watapew dawa za Kichocho, na watoto 466,095 dawa za Minyoo ya Tumbo na kufanya jumla yao kuwa ni  752, 877.

Akizungumza katika utangulizi wa kikao, Mratibu wa Magonjwa yasiyopewa kipaumbele Mkoa wa Shinyanga Timothy Sosoma, amesema kampeni hii ya utoaji kinga tiba ya dawa za kichocho na minyoo ya tumbo kwa watoto, itafanyika kwa siku moja ambayo ni Novemba 24 katika shule zote katika mkoa wa shinyanga.

Sosoma amesema kuwa, katika Mkoa wa Shinyanga tatizo hili lipo kwa watoto wengi ambapo huugua kichocho na minyoo ya tumbo, kutokana na kupenda kuogelea kwenye madimbwi ya maji na  majaruba ya mpunga hasa katika kipindi hiki cha msimu wa mvua.

Aidha, muwakili wa Mganga Mkuu Mkoa wa Shinyanga  Mradiolojisti Faustine Mlyutu amesisitiza utoaji elimu kwa wazazi juu ya kuwapatia watoto wao kinga tiba ya dawa hizo.

Matangazo

  • No records found
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • KIKAO CHA MAPITIO YA ROBO MWAKA KWA KIPINDI CHA OKT - DES 2024 CHA (PJT MMMAM) CHAFANYIKA MKOANI SHINYANGA.

    February 28, 2025
  • RCC SHINYANGA YARIDHIA MAPENDEKEZO NANE (8) YA MATUMIZI BORA YA ARDHI.

    February 27, 2025
  • KUKAMILISHWA KWA MIRADI YA BARABARA KUTAPUNGUZA KERO KWA WANANCHI – RC MACHA

    February 26, 2025
  • WALIMU, TOENI ELIMU INAYOENDANA NA MABADILIKO YA TEKNOLOJIA -RC MACHA

    February 24, 2025
  • Angalia zote

Video

MIFUKO BANDIA ZAIDI YA ELFU 20 YAKAMATWA SHINYANGA
Video Nyinginezo

Viunganishi vya Haraka

  • Historia
  • Dira na Dhima
  • Hotuba Mbalimbali
  • Video Mbalimbali
  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Picha za Matukio
  • Miongozo na kanuni

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Mfumo wa kutuma, kupokea na kufuatilia malalamiko, mapendekezo, maulizo na pongezi
  • Ofisi ya Rais Menejimenti ya utumishi wa Umma
  • Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Boma Street, Mwanza Road

    Anuani: P.O.Box 320, Shinyanga

    Simu: +255 28 2762222

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras@shinyanga.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2018. Mkoa wa Shinyanga. Haki zote zimehifadhiwa