• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
    • eVibali |
Shinyanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Shinyanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Yetu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
      • Afya
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Shinyanga
    • Wilaya ya Kahama
    • Wilaya ya Kishapu
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu
    • Halmashauri ya Mji wa Kahama
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu
    • Halmashauri ya Wilaya ya Msalala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
    • Bandari Kavu
  • Huduma
    • Kutoa Ushauri wa Kitaalam
    • Kutafsiri Sheria na Sera
    • Kuratibu Shughuli za Wadau
    • Ulinzi na Usalama
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Tafiti
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha

RC MNDEME AKUTANA NA WAZEE, VIONGOZI WA DINI NA MACHIFU MKOANI SHINYANGA

Posted on: June 17th, 2023

Na. Shinyanga RS.

Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Mhe. Christina Mndeme aekutana na kufanya mazungumzo na viongozi wa dini, wazee na machifu wa Mkoa wa Shinyanga kuhusu mambo mbalimbali yanayowahusu maendeleo ya Nchi yetu huku akiwakumbusha kuwa mpaka sasa Serikali ya Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambavyo imekwisha leta zaidi ya Bilioni 612 katika Mkoa wa Shinyanga ambazo zinafanya kazi katika kutekeleza miradi mbalimbali kwenye Sekta ya Afya, Elimu, Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi, Miundombinu nk.

Mhe.   Mndeme pamoja na mambo mengine amewaeleza kwa kina kuhusu mkataba baina ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Serikali ya Dubai kwenye ushirikiano wa Kiuchumi na Kijamii kwa ajili ya Uendelezaji na Uboreshaji wa Utendaji kazi wa Bandari Tanzania. Katika eneo hili nikiwaeleza na kuwafafanulia namna ambavyo Serikali yetu ilivyo na nia njema zaidi katika hili ikiwa na pamoja na faida zake kama ambavyo DP World walivyofanya katika Nchi nyingine walizowekeza katika Bandari.

‘’Katika hili Wazee wangu, Viongozi wang una Machifu wangu wa Mkoa huu wa Shinyanga nipende kuwaeleza tu kuwa uwepo wa Mkataba huu unakwenda kuboresha zaidi utendaji kazi wa Bandari yetu na hivyo kwenda kuongeza mapato ya nchi, uimarishaji wa utoaji wa huduma kwa wananchi ambao ni wafanyabiashara wet una hata kuimarisha uhusiano wetu kama nchi na Dubai,’’ alisema Mhe. Mndeme.

Kando na hayo, wao kwa umoja wao kwa sehemu kubwa walikuwa wakilielewa vema jambo hili japokuwa baadhi yao walitoa mapendekezo kama vile kuitaka Serikali iendelee kutoa elimu kwa wananchi zaidi kuhusu hili kwakuwa kumekuwa na upotoshaji mkubwa zaidi kutoka kwa wachache wasiokuwa na nia njema kwa Serikali.

Aidha katika hatua nyingine wazee, viongozi wa dini na machifu kwa umoja wao walisoma TAMKO LA MKOA JUU YA KINACHOENDELEA KWENYE MKATABA HUO, tamko ambalo lilisomwa na Chifu Charles Njange Kidola kwa niaba yao wote huku ndani yake likieleza kuwa WANAUNGA MKONO SERIKALI KATIKA KUINGIA MKATABA HUO huku wakisema kuwa wanalaani vikali wale wote wasiokuwa na dhamira njema kwa Taifa kwa kuendelea kupotosha umma.

Pamoja na mambo mengine, Mndeme aliwaeleza wajumbe hao kuwa ataendelea kukutana na kuzungumza na makundi mbalimbali Mkoani hapa ambapo tarehe 19 Juni, 2023 nitakutana na viongozi wa Machinga na Machinga wenyewe wa Mkoa ili tujadiliane tujue changamoto, fursa na namna ya kwenda nazo na tarehe 20 Juni, 2023 nitakutana na wamiliki wa viwanda pamoja na wafanyabiashara wote ambapo pia tutajadiliana kwa kina mambo mbalimbali yanayowahusu wao na namna ya kuboresha, kutatua changamoto na kuzitumia fursa zilizopo Shinyanga na Tanzania kwa ujumla.

Picha ikionesha baadhi ya wazee na viongozi wakiwa katika kikao

Matangazo

  • No records found
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • WANUFAIKA WA MIKOPO YA 10% LIPENI KWA WAKATI ILI PIA VIKOPESHWE NA VIKUNDI VINGINE - RC MACHA

    February 13, 2025
  • CP. HAMDUNI AKUTANA NA KAMATI YA MICHEZO YA JWTZ

    February 13, 2025
  • WANANCHI, LIPENI KODI YA ARDHI KWA WAKATI MUEPUKE RIBA - LEO KOMBA

    February 12, 2025
  • WAJUMBE WA BODI, TUMIENI TAALUMA ZENU KUISAIDIA HOSPITALI KUKAMILISHA MIRADI YA UJENZI- RAS CP. HAMDUNI.

    February 11, 2025
  • Angalia zote

Video

MIFUKO BANDIA ZAIDI YA ELFU 20 YAKAMATWA SHINYANGA
Video Nyinginezo

Viunganishi vya Haraka

  • Historia
  • Dira na Dhima
  • Hotuba Mbalimbali
  • Video Mbalimbali
  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Picha za Matukio
  • Miongozo na kanuni

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Mfumo wa kutuma, kupokea na kufuatilia malalamiko, mapendekezo, maulizo na pongezi
  • Ofisi ya Rais Menejimenti ya utumishi wa Umma
  • Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Boma Street, Mwanza Road

    Anuani: P.O.Box 320, Shinyanga

    Simu: +255 28 2762222

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras@shinyanga.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2018. Mkoa wa Shinyanga. Haki zote zimehifadhiwa