• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
    • eVibali |
Shinyanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Shinyanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Yetu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
      • Afya
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Shinyanga
    • Wilaya ya Kahama
    • Wilaya ya Kishapu
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu
    • Halmashauri ya Mji wa Kahama
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu
    • Halmashauri ya Wilaya ya Msalala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
    • Bandari Kavu
  • Huduma
    • Kutoa Ushauri wa Kitaalam
    • Kutafsiri Sheria na Sera
    • Kuratibu Shughuli za Wadau
    • Ulinzi na Usalama
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Tafiti
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha

RC MNDEME APONGEZA UWEKEZAJI WA VIWANDA MKOANI SHINYANGA

Posted on: November 22nd, 2023

Na. Shinyanga RC.

MKUU wa Mkoa wa Shinyanga Mhe. Christina S. Mndeme amepongeza sana uwekezaji sekta ya viwanda uliofanyika na unaoendelea katika mkoa wa shinyanga huku akipiga nduru kwa wawekezaji wengine kuja kuwekeza mkoa wa shinyanga kwakuwa kuna mahitaji yote muhimu kwa uwekezaji wa aina yoyote.

Mhe. Mndeme amesema hayo leo tarehe 21 Novemba, 2023 alipotembelea kiwanda cha Jambo Food Production C. Ltd kinachozalisha bidhaa za maji, juisi, biskuti, mikate na nyingine nyingi za chakula na Gilitu Enterprises Co. Ltd kinachozalisha mafuta ya kupikia ( SANICO), mchele na unga wa ugali viwanda vyote hivi vipo Manispaa ya Shinyanga.

"Kwa dhati ya moyo wangu nipongeze sana uwekezaji huu mkubwa unaofanywa na wazawa hawa, jambo ambalo linatia moyo na faraja kubwa kwa serikali kwakuwa wanazalisha ajira, wanalipa kodi stahiki, na wanauheshimisha mkoa na nchi kwa ujumla wake, hongereni sana Jambo na Gilitu," alisema Mhe. Mndeme.

Huu ni Utaliiwa Viwanda Mkoa wa Shinyanga, ambapo Mhe. Mndeme ametoa wito kwa wadau na woye wenye nia ya kujifunza watembelee shinyanga waje kuona uwekezaji bora, wenye tija, wenye kuvutia uliopo hapa shinyanga, hakika shinyanga ya sasa siyo ya zamani.

Aidha serikali imeahidi kuwapatia ushirikiano wa kutosha wawekezaji hawa, waliopo, watakaokuja wawe wazawa au wageni serikali itawawekea mazingira rafiki wakati wote na hayo ndiyo maelekezo ya Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, hivyo waje kuwekeza shinyanga.


Huu ni muendelezo wa ziara za Mhe. Mndeme ndani ya mkoa ambapo anaangalizia na kuhamasisha uwekezaji zaidi ikiwa ni sehemu ya utekelezaji wa Ilani ya CCM wa kuhakikisha maendeleo yanawafiiia wananchi vyote kupitia uwekezaji uliopo shinyanga hasa katika sekta ya viwanda, elimu nk huku akiitaja ziara hii kuwa ni UTALII WA VIWANDA MKOANI SHINYANGA.

HABARI PICHA



Matangazo

  • No records found
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • WANUFAIKA WA MIKOPO YA 10% LIPENI KWA WAKATI ILI PIA VIKOPESHWE NA VIKUNDI VINGINE - RC MACHA

    February 13, 2025
  • CP. HAMDUNI AKUTANA NA KAMATI YA MICHEZO YA JWTZ

    February 13, 2025
  • WANANCHI, LIPENI KODI YA ARDHI KWA WAKATI MUEPUKE RIBA - LEO KOMBA

    February 12, 2025
  • WAJUMBE WA BODI, TUMIENI TAALUMA ZENU KUISAIDIA HOSPITALI KUKAMILISHA MIRADI YA UJENZI- RAS CP. HAMDUNI.

    February 11, 2025
  • Angalia zote

Video

MIFUKO BANDIA ZAIDI YA ELFU 20 YAKAMATWA SHINYANGA
Video Nyinginezo

Viunganishi vya Haraka

  • Historia
  • Dira na Dhima
  • Hotuba Mbalimbali
  • Video Mbalimbali
  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Picha za Matukio
  • Miongozo na kanuni

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Mfumo wa kutuma, kupokea na kufuatilia malalamiko, mapendekezo, maulizo na pongezi
  • Ofisi ya Rais Menejimenti ya utumishi wa Umma
  • Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Boma Street, Mwanza Road

    Anuani: P.O.Box 320, Shinyanga

    Simu: +255 28 2762222

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras@shinyanga.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2018. Mkoa wa Shinyanga. Haki zote zimehifadhiwa