• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
    • eVibali |
Shinyanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Shinyanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Yetu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
      • Afya
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Shinyanga
    • Wilaya ya Kahama
    • Wilaya ya Kishapu
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu
    • Halmashauri ya Mji wa Kahama
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu
    • Halmashauri ya Wilaya ya Msalala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
    • Bandari Kavu
  • Huduma
    • Kutoa Ushauri wa Kitaalam
    • Kutafsiri Sheria na Sera
    • Kuratibu Shughuli za Wadau
    • Ulinzi na Usalama
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Tafiti
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha

RC MNDEME ASHIRIKI TAMASHA LA SANJO YA BUSIYA - SHINYANGA

Posted on: July 7th, 2023

Na. Shinyanga RS.

MKUU wa Mkoa wa Shinyanga Mhe. Christina Solomon Mndeme leo tarehe 7 Julai, 2023 ameshiriki katika Tamasha la Sanjo Busiya ambalo limefanyika katika Kijiji cha Negezi Kata ya Ukenyenge Wilaya ya Kishapu hapa Mkoani Shinyanga na kuwapongeza sana waandaaji kwakuwa tamasha hili limeanza rasmi tarehe 1 Julai, 2023 na linatajwa kuhudhuriwa na watu zaidi ya 10,000 kutoka pande mbalimbali na kwamba huu ni mwaka wa 13 tangua kuanzishwa kwa tamasha.

Pamoja na pongezi nyinhi kwa ma Chifu na uongozi wote kwa kufanikisha sherehe hizi lakini pia amewasihi kukemea kwa nguvu zote mmomonyoko wowote wa maadili ambao unaweza kuharibu jamii yetu na vizazi vyetu kwa ujumla huku akiwakumbusha watambue kazi njema anayoifanya Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika sekta mbalimbali ikiwamo afya, elimu, miundombinu, ustawi wa jamii huku akiwataka kumuunga mkono kwa kazi zote za kuwaletea maendeleo wananchi.

"Ndugu zangu wanaTamasha la Busiya nawapongeza sana kwa kufanikisha vema sana tamasha hili muhimu ambalo limehudhuriwa na watu zaidi ya elfu kumi kutoka ndani nan nje ya Mkoa wa Shinyanga, lakini pia niwakumbushe ndugu zangu kuendelea kusimamia maadili yetu ya Kitanzania na tuendelee kumuunga mkono Rais wetu kwa kazi kubwa na njema ambazo anazifanya katika kutuletea maendeleo sisi wananchi," alisema Mhe. Mndeme.

Serikali imepokea changamoto zote zilizowasilishwa na Chifu Edward na kwamba zitashulikiwa kulingana na zilivyo kwakuwa zipo za kisera na kibajeti.

Kwa upande wake Mtemi wa Busiya Ndugu Edward Makwaiya aliipongeza sana Serikalikwa kazi inazozifanya kwa wananchi huku akiomba Serikali kuanzisha Chombo Maalumu kiwe na Mamlaka kama zilivyo Mamlaka nyingine ili waweze kuwa na maamuzi katika kuisaidia Serikali kupambana na mila potofu zenye kuharibu jamii.

Aidha Mtemi Mwakwaiya alisema kuwa lengo la tamasha hili ni pamoja na kumshukuru Mungu kwa mwaka uliopita, na kukaribisha mwaka mwingine ikiwa ni pamoja na kudumisha tamaduni zetu na kuwaelimisha wananchi wote kuacha kuiga utamaduni wa nje na kuhamasisha utalii wa ndani kwa mashindano ya ngoma za jadi.

 

Matangazo

  • No records found
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • WANUFAIKA WA MIKOPO YA 10% LIPENI KWA WAKATI ILI PIA VIKOPESHWE NA VIKUNDI VINGINE - RC MACHA

    February 13, 2025
  • CP. HAMDUNI AKUTANA NA KAMATI YA MICHEZO YA JWTZ

    February 13, 2025
  • WANANCHI, LIPENI KODI YA ARDHI KWA WAKATI MUEPUKE RIBA - LEO KOMBA

    February 12, 2025
  • WAJUMBE WA BODI, TUMIENI TAALUMA ZENU KUISAIDIA HOSPITALI KUKAMILISHA MIRADI YA UJENZI- RAS CP. HAMDUNI.

    February 11, 2025
  • Angalia zote

Video

MIFUKO BANDIA ZAIDI YA ELFU 20 YAKAMATWA SHINYANGA
Video Nyinginezo

Viunganishi vya Haraka

  • Historia
  • Dira na Dhima
  • Hotuba Mbalimbali
  • Video Mbalimbali
  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Picha za Matukio
  • Miongozo na kanuni

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Mfumo wa kutuma, kupokea na kufuatilia malalamiko, mapendekezo, maulizo na pongezi
  • Ofisi ya Rais Menejimenti ya utumishi wa Umma
  • Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Boma Street, Mwanza Road

    Anuani: P.O.Box 320, Shinyanga

    Simu: +255 28 2762222

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras@shinyanga.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2018. Mkoa wa Shinyanga. Haki zote zimehifadhiwa