• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
    • eVibali |
Shinyanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Shinyanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Yetu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
      • Afya
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Shinyanga
    • Wilaya ya Kahama
    • Wilaya ya Kishapu
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu
    • Halmashauri ya Mji wa Kahama
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu
    • Halmashauri ya Wilaya ya Msalala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
    • Bandari Kavu
  • Huduma
    • Kutoa Ushauri wa Kitaalam
    • Kutafsiri Sheria na Sera
    • Kuratibu Shughuli za Wadau
    • Ulinzi na Usalama
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Tafiti
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha

RC MNDEME ATOA MWAROBAINI YA KERO ZA WANANCHI - KAHAMA

Posted on: September 21st, 2023

Na. Shinyanga RS.

Mkuu wa mkoa wa Shinyanga Mhe. Christina  Mndeme  Septemba 20,  2023 amesikiliza na kutatua papo hapo kero za wananchi wakati wa mkutano wa hadhara uliofanyika katika Mtaa wa Shunu Kata ya Nyahanga Manispaa ya Kahama.

Akizungumza katika mkutano huo Mhe. Mdeme mesema baadhi ya kero  zilizowasilishwa na  wananchi zimeanza kushughulikiwa  ikiwamo ya ubovu wa miundombinu ya barabara ambaopo fedha zinaendelea kutolewa na ujenzi unaendelea.

Kero ya maji ilipatiwa ufumbuzi papo hapo ambapo alimuagiza Mkuugenzi wa Mamlaka ya MajiSafi na Usafi wa Mazingira Kahama Ndg. Allen Marwa kulishughulikia kwa haraka suala la kubadilisha mtandao wa bomba za zamani na kuweka mpya, huku suala la migogoro ya ardhi akimuagiza Mkuu wa Wilaya ya Kahama Mhe. Mboni Mhita kushirikiana na Mkurugenzi wa Manispaa ya Kahama Ndg. Anderson Msumba ili kuliondoa haraka na wananchi waendelee na shughuli zao za maendeleo.

Sanjari na hilo, kuhusu Kero ya Shule ya Sekondari kwa eneo hilo la Nyahanga  kwa sasa Serikali inamalizia ujenzi wa Shule mpya ya Nyahanga inayogharimu zaidi ya milioni 603 huku akiwaeleza kuwa amemuagiza Mkurugenzi wa Manispaa ya Kahama kuongeza shule nyingine kupitia bajeti ijayo.

Mhe. Mndeme amesema katika Mkoa wa Shinyanga pekee, Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ametoa zaidi shilingi Trilioni moja ndani ya utawala wake fedha ambazo zitatumika kutekeleza miradi mbalimbali ya maendeleo.

Aidha, amewasihi pia wananchi waendelee  kumuunga Mkono Rais Samia ili aendelee kutekeleza miradi mbalimbali ya maendeleo. Awali baadhi ya wananchi waliowasilisha kero zao kwenye mkutano huo ambazo zilipatiwa majibu na RC Mndeme.

PICHA NA MATUKIO KATIKA MKUTANO WA HADHARA NYAHANGA - KAHAMA

Matangazo

  • No records found
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • WANUFAIKA WA MIKOPO YA 10% LIPENI KWA WAKATI ILI PIA VIKOPESHWE NA VIKUNDI VINGINE - RC MACHA

    February 13, 2025
  • CP. HAMDUNI AKUTANA NA KAMATI YA MICHEZO YA JWTZ

    February 13, 2025
  • WANANCHI, LIPENI KODI YA ARDHI KWA WAKATI MUEPUKE RIBA - LEO KOMBA

    February 12, 2025
  • WAJUMBE WA BODI, TUMIENI TAALUMA ZENU KUISAIDIA HOSPITALI KUKAMILISHA MIRADI YA UJENZI- RAS CP. HAMDUNI.

    February 11, 2025
  • Angalia zote

Video

MIFUKO BANDIA ZAIDI YA ELFU 20 YAKAMATWA SHINYANGA
Video Nyinginezo

Viunganishi vya Haraka

  • Historia
  • Dira na Dhima
  • Hotuba Mbalimbali
  • Video Mbalimbali
  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Picha za Matukio
  • Miongozo na kanuni

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Mfumo wa kutuma, kupokea na kufuatilia malalamiko, mapendekezo, maulizo na pongezi
  • Ofisi ya Rais Menejimenti ya utumishi wa Umma
  • Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Boma Street, Mwanza Road

    Anuani: P.O.Box 320, Shinyanga

    Simu: +255 28 2762222

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras@shinyanga.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2018. Mkoa wa Shinyanga. Haki zote zimehifadhiwa