• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
    • eVibali |
Shinyanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Shinyanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Yetu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
      • Afya
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Shinyanga
    • Wilaya ya Kahama
    • Wilaya ya Kishapu
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu
    • Halmashauri ya Mji wa Kahama
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu
    • Halmashauri ya Wilaya ya Msalala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
    • Bandari Kavu
  • Huduma
    • Kutoa Ushauri wa Kitaalam
    • Kutafsiri Sheria na Sera
    • Kuratibu Shughuli za Wadau
    • Ulinzi na Usalama
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Tafiti
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha

RC MNDEME AWAPONGEZA PASS TRUST KWA KAZI NZURI, AWATAKA KUONGEZA KASI ILI KUWAFIKIA WAKULIMA WOTE HASA VIJANA

Posted on: August 8th, 2023

Na. Shinyanga RS.

MKUU wa Mkoa wa Shinyanga Mhe. Christina Mndeme amewapongeza sana Asasi ya Kusaidia Sekta Binafsi za Kilimo yaani Private Agricultural Sector Support - PASS kwa kazi nzuri wanazozifanya katika Sekta ya Kilimo huku akiwataka kuongeza kasi ili kuweza  kuwafikia wakulima wote hasa vijana kundi ambalo ni kubwa  ambalo likiwezeshwa zaidi litaleta tija kubwa kwa kuinua na kuboresha kipato kwao na Taifa kwa ujumla.

Hayo yamesemwa leo tarehe 08 Agosti, 2023 alipokuwa akihutubia wakulima, wananchi, viongozi wa Serikali, Dini na wadau mbalimbali katika maadhimisho ya Sikukuu ya Wakulima (Nanenane) Kanda ya Ziwa Mashariki katika viwanja vya Nyakabindi Mkoani Simiyu ambapo Mhe. Mndeme ndiye alikuwa Mgeni Rasmi huku akisisitiza kuwa ili Taifa letu liweze kupiga hatua kiuchumi lazima tuanze kwa kuwabadilisha watu wetu ki-fikra hasa vijana na wanawake wafanye kazi kwa bidii na maarifa ili kukuza uchumi wao na kuchangia maendeleo ya taifa letu.

"Nawapongeza sana PASS TRUST kwa kazi nzuri mnayoifanya katika Sekta ya Kilimo kwa Kanda ya Ziwa Mashariki lakini niwatake sasa kwenda kuongeza kasi katika kuwafikia wakulima wote hasa vijana, kundi hili mkilifikia kwa ukubwa wake mtakuwa mmesaidia sana kuwainua kiuchumi na kuongeza ajira kwa vijana nchini," alisema Mhe. Mndeme.

Kando na pongezi hizo, pia Mhe. Mndeme amewataka Taasisi ya Kudhihiti Ubora wa Mbegu Tanzania - TOSCI kufuatilia na kufanya utafiti wa kutosha katika eneo la mbegu bora zinazohimili changamoto ziweze kutumika kwa wakulima wetu.

Pia aliwaelekeza Taasisi ya Utafiti wa Kilimo Tanzania - TARI kufanya tafiti ya kina ili kujuwa na kubaini zaidi magonjwa yanayoathiri mazao na kuyatafutia ufumbuzi wake kwa haraka, na pia aliwataka Bodi ya Pamba kuongeza kasi ya kutoa elimu kwa wakulima katika maeneo yao, kwakuwa kumekuwepo na tatizo la uchafu kwa baadhi ya zao la pamba.

Mhe. Mndeme pia amewahimiza sana wananchi kulima, kupanda na kutumia zaidi mchicha aina ya URUSI, mboga ambayo inatajwa kuwa na virutubisho vingi na bora zaidi kwa afya ya wananchi wetu huku akiwapongeza sana PASS TRUST kwa kuwa mshindi wa jumla katika maadhimisho haya lakini pia pongezi kwao kwa kuwa wadhamini wakuu wa sherehe za nanenane kwa Kanda ya Ziwa Mashariki  2023.

Maadhimisho ya Sikukuu ya Nanenane ya mwaka huu wa 2023 yamebeba Kauli Mbiu isemayo "Vijana na Wanawake ni Msingi Imara wa Mifumo Endelevu ya Chakula".

RC Mndeme akiwa amepanda moja kati ya Trekta zilizopo kwenye Banda PASS TRUST katika maonesho ya nanenane viwanja vya Nyakabindi Bariadi Mkoani Simiyu

RC mndeme akiwa katika banda la Pass Trust 

RC mndeme katika moja kati ya Banda la mifugo linalomilikiwa na Jeshi la Kujenga Taifa (JKT)

Picha na matukio

Matangazo

  • No records found
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • KIKAO CHA MAPITIO YA ROBO MWAKA KWA KIPINDI CHA OKT - DES 2024 CHA (PJT MMMAM) CHAFANYIKA MKOANI SHINYANGA.

    February 28, 2025
  • RCC SHINYANGA YARIDHIA MAPENDEKEZO NANE (8) YA MATUMIZI BORA YA ARDHI.

    February 27, 2025
  • KUKAMILISHWA KWA MIRADI YA BARABARA KUTAPUNGUZA KERO KWA WANANCHI – RC MACHA

    February 26, 2025
  • WALIMU, TOENI ELIMU INAYOENDANA NA MABADILIKO YA TEKNOLOJIA -RC MACHA

    February 24, 2025
  • Angalia zote

Video

MIFUKO BANDIA ZAIDI YA ELFU 20 YAKAMATWA SHINYANGA
Video Nyinginezo

Viunganishi vya Haraka

  • Historia
  • Dira na Dhima
  • Hotuba Mbalimbali
  • Video Mbalimbali
  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Picha za Matukio
  • Miongozo na kanuni

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Mfumo wa kutuma, kupokea na kufuatilia malalamiko, mapendekezo, maulizo na pongezi
  • Ofisi ya Rais Menejimenti ya utumishi wa Umma
  • Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Boma Street, Mwanza Road

    Anuani: P.O.Box 320, Shinyanga

    Simu: +255 28 2762222

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras@shinyanga.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2018. Mkoa wa Shinyanga. Haki zote zimehifadhiwa