• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
    • eVibali |
Shinyanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Shinyanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Yetu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
      • Afya
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Shinyanga
    • Wilaya ya Kahama
    • Wilaya ya Kishapu
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu
    • Halmashauri ya Mji wa Kahama
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu
    • Halmashauri ya Wilaya ya Msalala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
    • Bandari Kavu
  • Huduma
    • Kutoa Ushauri wa Kitaalam
    • Kutafsiri Sheria na Sera
    • Kuratibu Shughuli za Wadau
    • Ulinzi na Usalama
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Tafiti
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha

RC MNDEME AWASIMAMISHA KAZI WATUMISHI WANNE - KAHAMA MC

Posted on: February 29th, 2024

Na. Shinyanga RS.

MKUU wa Mkoa wa Shinyanga Mhe. Christina Mndeme amewasimamisha kazi watumishi wanne wa Dibisheni ya Ardhi na Mipango Miji Manispaa ya Kahama ili kupisha uchunguzi kufuatia msululu wa malalamiko dhidi yao huku akiwataka watumishi wote Mkoa wa Shinyanga kufanya kazi kwa kuzingatia maadili, sheria, utu na bila dhuluma ili wananchi wananchi wafurahie huduma zitolewazo na Serikali.

Tukio hili limetokea leo tarehe 29 Februari, 2024 katika mkutano wa hadhara uliofanyika viwanja vya Parking ya Malori uliopo Kata ya Majengo hapa Manispaa ya Kahama wenye leongo la kupokea, kusikiliza na kuzipatia majawabu kero zote za wananchi.

Akizungumza katika hitimisho la mkutano huu RC MNDEME amesema, kumekuwepo na msululu wa malalamiko dhidi ya watumishi wa Idara ya Ardhi Manispaa ya Kahama, jqmbo linalopelekea kunyooshewa vidole kila kiongozi anapokuja Kahama huku majina yanayotajwa ni yaleyale yanajirudia.

"Kunekuwepo na malalamiko mengi sana Idara ya Ardhi hapa Manispaa ya Kahama, kero hii imekuwa ikiripotiwa kila ugeni wa kiongozi yeyote anayefika hapa na majina yanayotajwa ni hayahaya. Kufuatia msululu wa malalamiko haya, wafuatao watapisha uchunguzi ili watakapobainika hawana hatia watarejeshwa watumishi hawa ni Clemence Mkusa ( Mkuu wa Divisheni ya Ardhi na MipangoMiji ), Yusuph Shaban ( Afisa Ardhi Mteule ), Yahaya Msangi ( Mpima Ardhi ) na Crispine Kisengo ambaye ni Afisa Mipango Miji," amesema RC MNDEME.

Kando na hili RC MNDEME pia ametatua kero ya viwanja 14 mali ya Calorine Magege ya kupatiwa haki yake, mgogoro uliodumu kwa zaidi ya miaka 6 sasa, huku akimuagiza Mkuu wa Polisi Wilaya ya Kahama kuhakikisha anawafuatilia na kuwakamata wamiliki wa nyumba zinazojihusisha na ukahaba sanjali na kuwakamata wale wote wanaojihusisha na ukahaba pamoja na wanunuzi wao.

Picha ikimuonesha RC MNDEME (kulia) akiwa na RAS SHINYANGA Prof. Siza Tumbo wakati wa mkutano wa hadhara kusikiliza na kutatua kero za wananchi Manispaa ya Kahama


Matangazo

  • No records found
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • ENDELEENI KUTOA ELIMU ZAIDI KUHUSU AFYA YA AKILI - DC. MBONI

    May 30, 2025
  • TAKUKURU SHINYANGA YAANZA KUCHUKUA HATUA DHIDI YA UBADHIRIFU WA SHILINGI MILIONI 92 ZA WAKULIMA WA TUMBAKU WA USHETU - DONASIAN.

    May 27, 2025
  • MAISHA BAADA YA KUSTAAFU YANAHITAJI UTULIVU - DC. MTATIRO

    May 26, 2025
  • MAFUNZO YA IPOSA NI MKOMBOZI KWA VIJANA WALIO WENGI WANAOKOSA FURSA YA ELIMU YA KAWAIDA - RC. MACHA

    May 23, 2025
  • Angalia zote

Video

MIFUKO BANDIA ZAIDI YA ELFU 20 YAKAMATWA SHINYANGA
Video Nyinginezo

Viunganishi vya Haraka

  • Historia
  • Dira na Dhima
  • Hotuba Mbalimbali
  • Video Mbalimbali
  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Picha za Matukio
  • Miongozo na kanuni

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Mfumo wa kutuma, kupokea na kufuatilia malalamiko, mapendekezo, maulizo na pongezi
  • Ofisi ya Rais Menejimenti ya utumishi wa Umma
  • Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Boma Street, Mwanza Road

    Anuani: P.O.Box 320, Shinyanga

    Simu: +255 28 2762222

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras@shinyanga.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2018. Mkoa wa Shinyanga. Haki zote zimehifadhiwa