• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
    • eVibali |
Shinyanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Shinyanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Yetu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
      • Afya
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Shinyanga
    • Wilaya ya Kahama
    • Wilaya ya Kishapu
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu
    • Halmashauri ya Mji wa Kahama
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu
    • Halmashauri ya Wilaya ya Msalala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
    • Bandari Kavu
  • Huduma
    • Kutoa Ushauri wa Kitaalam
    • Kutafsiri Sheria na Sera
    • Kuratibu Shughuli za Wadau
    • Ulinzi na Usalama
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Tafiti
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha

RC MNDEME AWATAKA BODABODA KUENDELEA KUSHIRIKIANA NA JESHI LA POLISI

Posted on: October 14th, 2023

Na. Shinyanga RS

MKUU wa mkoa wa shinyanga Mhe. Christina S. Mndeme amewataka wafanyabiashara ya usafirishaji abiria na mizigo kupitia pikipiki (Bodaboda) kuendelea kushirikiana na Jeshi la Polisi katika kuwafichua wahalifu ili kuweza kutokomeza kabisa uhalifu katika maeneo yao huku akiwasisitiza kuendelea kuzingatia na kutii sheria za barabarani kwakuwa kazi zao zinahusisha wananchi.

Mhe. Mndeme ameyasema hayo leo alipomuwakilisha Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Mhe. Dkt. Yahaya Nawanda kama mgeni rasmi kwenye mashindano ya bodaboda yaliyopewa jina la Polisi Bodaboda Marathon -Simiyu ikiwa ni sehemu ya utekelezaji wa kampeni ya Sema Nao iliyoanzishwa na Jeshi la Polisi Mkoani Simiyu sambamba na kumuenzi Baba wa Taifa Hayati Mwl . Julius Kambarage Nyerere akitimiza miaka 24 tangu kifo chake.

"Pamoja na kuwapongeza sana nyote kwa kuandaa mashindano haya, lakini niwatake bodaboda wote kuendelea kushirikiana na jeshi la polisi katika zoezi la kuwafichua wahalifu wote ili tuweze kutokomeza kabisa uhalifu katika maeneo yetu, pia muendelee kuzingatia sheria wakati wote wa kazi zenu kwakuwa zinahusisha wananchi na mali zao," alisema Mhe. Mndeme.

Kwa upande wake Mkuu wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Simiyu Kamishna Msaidizi wa Polisi Edith Swebe alimueleza kaimu mkuu wa mkoa wa Simiyu Mhe. Mndeme kuwa uwepo wa hadhara hii unajieleza namna ambavyo jeshi la polisi lilivyo na ushirikiano mzuri na wananchi wakiwemo bodaboda wenyewe huku akisema kuwa hafla hii ni sehemu ya utekelezaji wa Kampeni ya Ongea Nao iliyoanzishwa maalum kwa ajili ya kujadili na kutatua kero zao.

Kaimu mkuu wa mkoa wa Simiyu Mhe. Mndeme alimuwakisha mkuu wa mkoa wa Simiyu Mhe. Dkt. Yahaya Nawanda ambaye hakuweza kushiriki kwakuwa hakuwepo katika maadhimisho haya ambayo yamefanyika tarehe 14 Oktoba, 2023 ikiwa ni sehemu pia ya kumuenzi baba wa taifa Hayati Mwl. J.K Nyerere.


HABARI PICHA


Matangazo

  • No records found
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • ENDELEENI KUTOA ELIMU ZAIDI KUHUSU AFYA YA AKILI - DC. MBONI

    May 30, 2025
  • TAKUKURU SHINYANGA YAANZA KUCHUKUA HATUA DHIDI YA UBADHIRIFU WA SHILINGI MILIONI 92 ZA WAKULIMA WA TUMBAKU WA USHETU - DONASIAN.

    May 27, 2025
  • MAISHA BAADA YA KUSTAAFU YANAHITAJI UTULIVU - DC. MTATIRO

    May 26, 2025
  • MAFUNZO YA IPOSA NI MKOMBOZI KWA VIJANA WALIO WENGI WANAOKOSA FURSA YA ELIMU YA KAWAIDA - RC. MACHA

    May 23, 2025
  • Angalia zote

Video

MIFUKO BANDIA ZAIDI YA ELFU 20 YAKAMATWA SHINYANGA
Video Nyinginezo

Viunganishi vya Haraka

  • Historia
  • Dira na Dhima
  • Hotuba Mbalimbali
  • Video Mbalimbali
  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Picha za Matukio
  • Miongozo na kanuni

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Mfumo wa kutuma, kupokea na kufuatilia malalamiko, mapendekezo, maulizo na pongezi
  • Ofisi ya Rais Menejimenti ya utumishi wa Umma
  • Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Boma Street, Mwanza Road

    Anuani: P.O.Box 320, Shinyanga

    Simu: +255 28 2762222

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras@shinyanga.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2018. Mkoa wa Shinyanga. Haki zote zimehifadhiwa