• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
    • eVibali |
Shinyanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Shinyanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Yetu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
      • Afya
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Shinyanga
    • Wilaya ya Kahama
    • Wilaya ya Kishapu
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu
    • Halmashauri ya Mji wa Kahama
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu
    • Halmashauri ya Wilaya ya Msalala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
    • Bandari Kavu
  • Huduma
    • Kutoa Ushauri wa Kitaalam
    • Kutafsiri Sheria na Sera
    • Kuratibu Shughuli za Wadau
    • Ulinzi na Usalama
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Tafiti
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha

RC MNDEME AZINDUA RASMI MGODI WA MWADUI, ASISITIZA KASI NA UFANISI WA UZALISHAJI

Posted on: July 17th, 2023

Na. Shinyanga RS.

MKUU wa Mkoa wa Shinyanga Mhe. Christina Solomon Mndeme amezindua rasmi uzalishaji wa Almasi katika Mgodi wa Mwadui (Williamson Diamond LTD) na kuagiza kuongezwa kasi ya ufanisi zaidi katika uzalishaji.

Mhe. Mndeme ameyasema leo tarehe 17 katika uzinduzi huo rasmi na kuashiria kuanza rasmi kwa uzalishaji ukiohuduriwa na viogozi mbalimbali wa Serikali, Chama Cha Mapinduzi, Mbunge wa Jimbo la Kishapu pamoja na wataalamu mbalimbali huku akiutaka uongozi wa Mwadui kuanza mara moja kwa usanifu wa bwawa jingine mbadala wa hili la sasa iwapo litajaa liwepo jingine tayari kwa kuendeleza shughuli badala ya kuwa na bwawa moja na punde inapotokea hitirafu inakuwa ni vigumu kendeleza kazi jambo ambalo linapelekea wao kukosa mapayo, Serikali kukosa mapato, kusimama kwa miradi ya maendeleo na kupunguza uchumi wa kipato kwa wafanyakazi wa mgodi pia.

"Kwanza niwapongeze sana uongozi wa Mgodi wa Mwadui pamoja na watumishi wote kwa kuanza tena kwa kazi za uzalishaji kwa wakati, kwani nilipokuja mimi niliagiza muanze kazi kabla ya tarehe 1 Agosti, 2023 na alipokuja Mhe. Dkt. Dotto Biteko aliagiza kuanza muanze tarehe 15 Julai, 2023 na ninyi mmeanza ndani ya muda mliopewa hongereni sana kwa hili, lakini pia niwatake muanze usanifu wa bwawa mbadala wa hili ili kuwa na tahadhari inapotokea shida liwese kusaidia," alisema Mhe. Mndeme.

Akizungumza wakati wa hitimisho la uzinduzi wa uzalishaji Meneja wa Mgodi Mhandisi Ayoub Mwenda alisema kuwa, wamepokea maelekezo yote yaliyotolewa na Mkuu wa Mkoa na kwamba bwawa la majitope maji lililopo hivi sasa litadumu kwa muda wa miaka miwili lakini wakati huu likiendelea kuhudumia wataanza usanifu wa bwawa mbadala kama ilivyoshauriwa na Mhe. Mndeme ambalo litakuwa ni muda mrefu zaidi ili kuweza kwenda na kasi pamoja na maelekezo ya Serikali katika kukidhi matarajio ya Mgodi na Serikali pia.

Awali akiongea katika tukio hilo, Mbunge wa Jimbo la Kishapu Mhe. Boniphace Butondo aliwapongeza sana Mwadui huku akisema kuwa sasa utekelezaji wa miradi ya maedeleo kwa wana Kishapu itarejea kama zamani kwani walikuwa wakinufaika kupitia sehemu ya mrejesho wa faida yao ambayo ilikuwa ikienda kutekeleza miradi yao ya maendeleo.

Mgodi wa Mwadui umeanza tena rasmi uzalishaji baada ya kuwa umesimama kwa takribani miezi nane sasa tangu kutokea kwa hitirafu iliyopelekea kubomoka kwa tuta la majitope jambo ambalo lilipelekea kusitishwa kwa uzalishaji wa Almasi katika eneo hilo.


Picha na matukio wakati wa uzinduzi

Matangazo

  • No records found
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • WANUFAIKA WA MIKOPO YA 10% LIPENI KWA WAKATI ILI PIA VIKOPESHWE NA VIKUNDI VINGINE - RC MACHA

    February 13, 2025
  • CP. HAMDUNI AKUTANA NA KAMATI YA MICHEZO YA JWTZ

    February 13, 2025
  • WANANCHI, LIPENI KODI YA ARDHI KWA WAKATI MUEPUKE RIBA - LEO KOMBA

    February 12, 2025
  • WAJUMBE WA BODI, TUMIENI TAALUMA ZENU KUISAIDIA HOSPITALI KUKAMILISHA MIRADI YA UJENZI- RAS CP. HAMDUNI.

    February 11, 2025
  • Angalia zote

Video

MIFUKO BANDIA ZAIDI YA ELFU 20 YAKAMATWA SHINYANGA
Video Nyinginezo

Viunganishi vya Haraka

  • Historia
  • Dira na Dhima
  • Hotuba Mbalimbali
  • Video Mbalimbali
  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Picha za Matukio
  • Miongozo na kanuni

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Mfumo wa kutuma, kupokea na kufuatilia malalamiko, mapendekezo, maulizo na pongezi
  • Ofisi ya Rais Menejimenti ya utumishi wa Umma
  • Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Boma Street, Mwanza Road

    Anuani: P.O.Box 320, Shinyanga

    Simu: +255 28 2762222

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras@shinyanga.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2018. Mkoa wa Shinyanga. Haki zote zimehifadhiwa