• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
    • eVibali |
Shinyanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Shinyanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Yetu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
      • Afya
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Shinyanga
    • Wilaya ya Kahama
    • Wilaya ya Kishapu
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu
    • Halmashauri ya Mji wa Kahama
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu
    • Halmashauri ya Wilaya ya Msalala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
    • Bandari Kavu
  • Huduma
    • Kutoa Ushauri wa Kitaalam
    • Kutafsiri Sheria na Sera
    • Kuratibu Shughuli za Wadau
    • Ulinzi na Usalama
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Tafiti
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha

RC MNDEMEAWEKA JIWE LA MSINGI MRADI WA MAJI - MWALUKWA, AKAGUA UKARABATI WA BWAWA NA KUFANYA MKUTANO WA HADHARA KIJIJI CHA MWALUKWA

Posted on: September 26th, 2023

Na. Shinyanga RS.

MKUU wa Mkoa wa Shinyanga Mhe. Christina S. Mndeme ameweka Jiwe la Msingi katika ujenzi wa Tangi la Maji lenye ujazo wa Lita 100,000 pamoja na bomba kuu la maji lililojengwa kwa ushirikiano wa Life Water International pamoja na RUWASA utaohudumia Vijiji 4 vya Mwalukwa, Bulambila, Kadoto na Ng'hama na kuhudumia wananchi zaidi ya 8400 na jumla ya mtandao wa KM 34 mradi ambao umetekelezwa katika Kijiji cha Bulambila Kata ya Mwalukwa.

Akizungumza mara baada ya kuweka jiwe la msingi Mhe. Mndeme amesema, Serikali ya awamu sita inayoongozwa na Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inauhusiano mzuri sana na Mashirka yasiyo ya Kiserikali na ndiyo sababu leo tunashuhudia kukamilishwa utekelezaji wa mradi huu muhimu ambao umekuja kuondoa kero hapa Kata ya Mwalukwa huku akiwataka Life Water International na RUWASA kuona namna ya kuongeza Tangi na mtandao wa maji zaidi ili uweze kuwahudumia watu wegi zaidi.

"Nawapongeza sana Life Water International na RUWASA kwa kutekeleza mradi huu mkubwa kabisa uliogharimu zaidi ya Bilioni 1 na ambao unaondoa na kutatua kero za uhaba wa maji kwa wananchi zaidi elfu 8484 ukiwa ni mtandao wenye urefu wa KM 34, hakika ni furaha sana hata wananchi mmewasikia hapa wakimshukuru Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuwezesha ukamilikaji wa mredi huu", alisema Mhe. Mndeme.

Kando na mradi huu, Mhe. Mndeme pia alitembelea na Ukarabati wa Bwawa la Mwalukwa ambalo awali lilikuwa na kina cha Mita 2.25 na sasa litakuwa na kina cha Mita 4.1 ambapo kwa upande wa ujazo wa lita za maji awali lilikuwa ni zaidi ya lita elfu 71 na litakapokamilika litakapokamilika litakuwa na uwezo wa lita zaidi ya laki 2.93.

Ukarabati huu wa Bwawa unakwenda kuwanufaisha wananchi zaidi ya elfu 22 ambao watawekea Birika kwa ajili ya kutumia maji haya na mifugo zaidi ya 13 ambapo kutaondoa kabisa kero ya uhaba wa maji eneo hili.

Ziara ya Mhe. Mndeme imehitimishwa kwa kufanya mkutano wa hadhara katika Kijiji cha Mwalukwa ambapo alisikiliza na kutatua kero za wananchi huku kubwa zaidi ikiwa ni kucheleweshwa kwa ukamilikaji wa bwawa hilo, ukosefu wa nyumba za walimu na ucheleweshaji wa usambazaji wa umeme wa REA.

Kero zote zilitatuliwa papo hapo ambapo suala la uchelewesha wa mradi aliagizwa msimamizi kukamilisha haraka ifikapo tarehe 15 Oktoba, 2023, kero ya nyumba ya walimu alimuagiza Mkuu wa Wilaya kulishughulikia huku kero ya REA akimueleza mwananchi kuwa umeme utawafikia hivi karibuni kwani ni jana tu ambapo mkandarasi alikutana na Mhe. Mndeme akamuahidi kufikisha huduma hiyo mapema Oktoba, 2023.

Huu ni muendelezo wa ziara za Mhe. Mndeme za kukagua utekelezaji wa miradi, kusikiliza na kutatua kero za wananchi katika Halmashauri zote 6 za Mkoa wa Shinyanga ambapo leo iilkuwa ni zamu ya Shinyanga DC.

MATUKIO KATIKA PICHA




Matangazo

  • No records found
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • KIKAO CHA MAPITIO YA ROBO MWAKA KWA KIPINDI CHA OKT - DES 2024 CHA (PJT MMMAM) CHAFANYIKA MKOANI SHINYANGA.

    February 28, 2025
  • RCC SHINYANGA YARIDHIA MAPENDEKEZO NANE (8) YA MATUMIZI BORA YA ARDHI.

    February 27, 2025
  • KUKAMILISHWA KWA MIRADI YA BARABARA KUTAPUNGUZA KERO KWA WANANCHI – RC MACHA

    February 26, 2025
  • WALIMU, TOENI ELIMU INAYOENDANA NA MABADILIKO YA TEKNOLOJIA -RC MACHA

    February 24, 2025
  • Angalia zote

Video

MIFUKO BANDIA ZAIDI YA ELFU 20 YAKAMATWA SHINYANGA
Video Nyinginezo

Viunganishi vya Haraka

  • Historia
  • Dira na Dhima
  • Hotuba Mbalimbali
  • Video Mbalimbali
  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Picha za Matukio
  • Miongozo na kanuni

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Mfumo wa kutuma, kupokea na kufuatilia malalamiko, mapendekezo, maulizo na pongezi
  • Ofisi ya Rais Menejimenti ya utumishi wa Umma
  • Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Boma Street, Mwanza Road

    Anuani: P.O.Box 320, Shinyanga

    Simu: +255 28 2762222

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras@shinyanga.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2018. Mkoa wa Shinyanga. Haki zote zimehifadhiwa