• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
    • eVibali |
Shinyanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Shinyanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Yetu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
      • Afya
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Shinyanga
    • Wilaya ya Kahama
    • Wilaya ya Kishapu
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu
    • Halmashauri ya Mji wa Kahama
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu
    • Halmashauri ya Wilaya ya Msalala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
    • Bandari Kavu
  • Huduma
    • Kutoa Ushauri wa Kitaalam
    • Kutafsiri Sheria na Sera
    • Kuratibu Shughuli za Wadau
    • Ulinzi na Usalama
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Tafiti
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha

RC SHINYANGA AAGIZA HALMASHAURI KUIMARISHA HUDUMA KWA WAZEE – AZUNGUMZA KUHUSU MATIBABU, DAWA

Posted on: September 23rd, 2025

Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Mhe. Mboni Mhita kupitia kwa mwakilishi wake Wakili Julius Mtatiro ambaye ni Mkuu wa Wilaya ya Shinyanga,  amezitaka halmashauri zote sita za Mkoa wa Shinyanga kuhakikisha kuwa zinayasimamia ipasavyo Mabaraza ya Wazee na kuyawezesha kwa kutenga bajeti mahsusi, kuwashirikisha katika vikao vya maamuzi, pamoja na kuhakikisha wazee wanapata huduma bora za afya.

Mtatiro ametoa maelekezo hayo Septemba 23, 2025, wakati akimwakilisha Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, Mhe. Mboni Mhita, kwenye Maadhimisho ya Siku ya Kimataifa ya Wazee Duniani yaliyofanyika katika Kijiji cha Jomu, Kata ya Tinde, Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga.

“Nawaagiza Wakurugenzi wote wa halmashauri kuhakikisha wanatenga fedha kwenye bajeti kwa ajili ya utekelezaji wa shughuli za wazee na kuwashirikisha wawakilishi wa mabaraza yao kwenye vikao vya maamuzi. Ni muhimu wazee wetu wakahusishwa katika ujenzi wa jamii,” amesema Mtatiro.

Kwa mujibu wa takwimu za Sensa ya Watu na Makazi ya mwaka 2022, Mkoa wa Shinyanga una jumla ya wazee 100,626. Kati ya hao, 43,256 wamepatiwa kadi za matibabu bila malipo, sawa na asilimia 43, na wengine 11,063 wamepatiwa kadi za CHF, sawa na asilimia 11.

“Nazipongeza halmashauri zilizofanikiwa kutoa kadi za matibabu kwa wazee bila malipo. Hii ni hatua muhimu katika kuhakikisha wazee wanapata huduma bora za afya,” ameongeza Mtatiro.

Aidha, ameagiza halmashauri zote kuhakikisha kila robo mwaka zinafanya ukaguzi wa dawa na fedha kwenye vituo vya kutolea huduma, kuagiza dawa kwa wakati, na kuhakikisha dawa kwa makundi ya msamaha zinakuwepo ili kuondoa usumbufu kwa wazee.

Akihitimisha hotuba yake, Mtatiro ametoa wito kwa wananchi wote wa Mkoa wa Shinyanga kujitokeza kwa wingi kushiriki uchaguzi utakaofanyika Oktoba 29, 2025, huku akisisitiza umuhimu wa kudumisha amani kabla, wakati na baada ya uchaguzi.

“Ni haki ya msingi ya kikatiba kushiriki uchaguzi. Tuende tukapige kura kwa amani na tuilinde nchi yetu dhidi ya vurugu,” amesisitiza.

Maadhimisho ya mwaka huu yamebeba kaulimbiu: “Wazee Tushiriki Uchaguzi Mkuu kwa Ustawi wa Jamii Yetu.

Matangazo

  • No records found
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • RC MHITA ARIDHISHWA NA UTOAJI HUDUMA HOSPITALI YA RUFAA YA MKOA WA SHINYANGA.

    September 28, 2025
  • WATENDAJI AMCOS WATAKIWA KUWA WABUNIFU ILI KUONGEZA UZALISHAJI NA THAMANI YA MAZAO YA KIBIASHARA.

    September 27, 2025
  • RC MHITA AITEMBELEA SHULE YA WASICHANA SHINYANGA, ATOA WITO WA KUWEKEZA KATIKA MAADILI NA ELIMU BORA KWA MTOTO WA KIKE.

    September 27, 2025
  • HALMASHAURI SHINYANGA ZATAKIWA KUTENGA BAJETI KUENDELEZA UTOAJI WA HUDUMA ZA MADAWATI YA USTAWI WA JAMII KATIKA STENDI ZA MABASI

    September 27, 2025
  • Angalia zote

Video

RC MHITA AAGIZA MKANDARASI KUKATWA MILIONI 2 KILA SIKU KWA KUCHELEWESHA BARABARA KAHAMA
Video Nyinginezo

Viunganishi vya Haraka

  • Historia
  • Dira na Dhima
  • Hotuba Mbalimbali
  • Video Mbalimbali
  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Picha za Matukio
  • Miongozo na kanuni

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Mfumo wa kutuma, kupokea na kufuatilia malalamiko, mapendekezo, maulizo na pongezi
  • Ofisi ya Rais Menejimenti ya utumishi wa Umma
  • Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    OFISI YA MKUU WA MKOA, MKOA WA SHINYANGA, 04 MTAA WA BOMA

    Anuani: P.O.Box 37180,SHINYANGA, TANZANIA

    Simu: +255 28 2762222

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras@shinyanga.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2018. Mkoa wa Shinyanga. Haki zote zimehifadhiwa