• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
    • eVibali |
Shinyanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Shinyanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Yetu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
      • Afya
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Shinyanga
    • Wilaya ya Kahama
    • Wilaya ya Kishapu
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu
    • Halmashauri ya Mji wa Kahama
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu
    • Halmashauri ya Wilaya ya Msalala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
    • Bandari Kavu
  • Huduma
    • Kutoa Ushauri wa Kitaalam
    • Kutafsiri Sheria na Sera
    • Kuratibu Shughuli za Wadau
    • Ulinzi na Usalama
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Tafiti
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha

RC Telack azindua kampeni ya "Usichukulie poa, nyumba ni choo"

Posted on: September 3rd, 2019

Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Mhe. Zainab Telack amezindua kampeni ya Kitaifa ya kuhamasisha wananchi kujenga vyoo bora na kuvitumia leo tarehe 03/09/2019, katika uwanja wa Zimamoto, eneo la Nguzonane, Manispaa ya Shinyanga inayojulikana kwa jina la usichukulie poa, Nyumba ni choo.

Katika hotuba yake ya uzinduzi, Mhe. Telack amewataka Maafisa Afya wa Halmashauri zote Mkoani hapa kuwasilisha mpango kazi wa kuhakikisha kila nyumba ina choo kufikia Desemba mwaka huu.

Aidha, Wakurugenzi wa Halmashauri kupitia Maafisa Tarafa na Watendaji wa kata na vijiji vyote wahakikishe wanapata taarifa za kaya ambazo hazina vyoo na hatua gani zimechukuliwa.

“Kufikia mwezi Desemba mwaka huu, tuwe hatuzungumzii mtu kutokuwa na choo tena, Mkoa una asilimia 50.6 tu ya vyoo bora. kwa hiyo turudi tujipange vizuri kuwa na vyoo bora” amesema Telack.

Mhe. Telack ameishukuru Wizara ya Afya na wadau Benki ya Dunia kwa kufanikisha Kampeni hii iliyoanza mwaka 2012 na kusema kuwa, ni kazi kubwa imefanyika kufikia asilimia zaidi ya 50 ya wananchi wanaotumia vyoo kutoka asilimia 17.

Awali, akitoa taarifa ya hali ya vyoo katika Mkoa, Afisa Afya wa Mkoa Bi. Neema Simba amesema, mila potofu ikiwemo ya marufuku wakwe kuchangia choo kimoja inachangia wananchi kujisaidia vichakani.

Naye Balozi wa Kampeni hiyo Bw. Mrisho Mpoto amesema, haiwezekani Mkoa kuacha shughuli nyingine za uzalishaji na kuzungumzia kujenga vyoo, hivvo kila mwananchi akawe balozi kwa mwingine kuhusu kuwa na vyoo bora na kuvitumia.

Aidha, Mrisho amewahamasisha wananchi kuachana na kasumba potofu ya kuonesha uwezo wa chakula kwenye kaya kwa vinyesi kusambaa.

Katibu Tawala wa Mkoa wa Shinyanga Bw. Albert Msovela amesema ni jambo linawezekana kabisa kwa Mkoa wote kila kaya kuwa na choo bora, iwapo viongozi katika kila ngazi watajipanga.

Matangazo

  • No records found
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • WANUFAIKA WA MIKOPO YA 10% LIPENI KWA WAKATI ILI PIA VIKOPESHWE NA VIKUNDI VINGINE - RC MACHA

    February 13, 2025
  • CP. HAMDUNI AKUTANA NA KAMATI YA MICHEZO YA JWTZ

    February 13, 2025
  • WANANCHI, LIPENI KODI YA ARDHI KWA WAKATI MUEPUKE RIBA - LEO KOMBA

    February 12, 2025
  • WAJUMBE WA BODI, TUMIENI TAALUMA ZENU KUISAIDIA HOSPITALI KUKAMILISHA MIRADI YA UJENZI- RAS CP. HAMDUNI.

    February 11, 2025
  • Angalia zote

Video

MIFUKO BANDIA ZAIDI YA ELFU 20 YAKAMATWA SHINYANGA
Video Nyinginezo

Viunganishi vya Haraka

  • Historia
  • Dira na Dhima
  • Hotuba Mbalimbali
  • Video Mbalimbali
  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Picha za Matukio
  • Miongozo na kanuni

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Mfumo wa kutuma, kupokea na kufuatilia malalamiko, mapendekezo, maulizo na pongezi
  • Ofisi ya Rais Menejimenti ya utumishi wa Umma
  • Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Boma Street, Mwanza Road

    Anuani: P.O.Box 320, Shinyanga

    Simu: +255 28 2762222

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras@shinyanga.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2018. Mkoa wa Shinyanga. Haki zote zimehifadhiwa