• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
    • eVibali |
Shinyanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Shinyanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Yetu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
      • Afya
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Shinyanga
    • Wilaya ya Kahama
    • Wilaya ya Kishapu
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu
    • Halmashauri ya Mji wa Kahama
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu
    • Halmashauri ya Wilaya ya Msalala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
    • Bandari Kavu
  • Huduma
    • Kutoa Ushauri wa Kitaalam
    • Kutafsiri Sheria na Sera
    • Kuratibu Shughuli za Wadau
    • Ulinzi na Usalama
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Tafiti
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha

REA AWAMU YA TATU YAZINDULIWA SHINYANGA

Posted on: April 6th, 2017

Naibu Waziri wa Nishati na Madini, Dk. Medard Kalemani amezindua mradi wa kusambaza umeme vijijini awamu ya tatu katika mkoa wa Shinyanga wilayani Kishapu wenye thamani ya sh. bilioni 35.5.

Katika uzinduzi huo uliofanyika kijiji cha Negezi kata ya Ukenyenge wilayani Kishapu, ukihusiha vijiji 149, Dk. Kalemani aliagiza Wakala wa Nishati Vijijini (REA) kuhakikishwa wanasambaza umeme sehemu zote bila upendeleo.

Aliwahimiza wananchi kutumia fursa ya kuwepo kwa nishati hiyoi katika kuboresha maisha yao kwa kutumia miradi ya uzalishaji mali pamoja na huduma mbalimbali za kijamii.

Aliwataka wautumie kwa kujenga viwanda vya kusindika mazao pamoja na huduma za afya,elimu, maji na viwanda vingine kama mashine za kusaga ambazo zitawapatia kipato na kuboresha maisha.

Aidha, naibu waziri huyo alizitaka serikali za kata na vijiji kubainisha maeneo maalumu ya viwanda ambayo katika mradi huo yatafikishiwa miundombinu ya umeme mkubwa.

”Tunataka kuwezesha wajasiriamali vijijini kupatiwa umeme utakaowezseha kuanzishwa kwa viwanda vidogo na vikubwa vijijini kwa gharama nafuu,” alisema Dk. Kalemani.

Aliongeza kuwa wananchi watakaounganishiwa umeme wanatakiwa kukamilisha utandazaji wa nyaya katikia nyumba zao mapema ili mkandarasi akifika wawe tayari kulipia na kuunganishiwa umeme.

Alisema kwa sehemu ambazo utandazaji utakuwa haujakamilika au nyumba si kubwa wanahimizwa kuomba kufungiwa kifaa cha Umeme Tayari (UMETA) ambacho hakihitaji kutandaza nyaya.

Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Kishapu, Nyabaganga Taraba aliishukuru Serikali kwa mradi huo wa REA huku akisema utasaidia kutengeneza ajira wilayani humo.

Taraba akizungumza kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, Zainab Telack alisema nishati ya umeme vijijini itasaidia kuanzishwa kwa viwanda vidogo na vya kati hivyo aliwataka wananchi kutumia fursa hiyo na kuacha uharibifu wa mazingira.

Hata hivyo, alitoa kilio chake kwa kumuomba naibu waziri kushughulikia changamoto ya baadhi ya wakandarasi kutomaliza miradi kwa wakati jambo ambalo linarudisha nyuma maendeleo.

Pia mkuu huyo wa wilaya aliwaomba wananchi watoe ushirikiano kwa kutoa maeneo kwa ajili ya kupitisha miundombinu ya umeme kwa kuwa ni kujiletea maendeleo yao wenyewe.

 Aliomba Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco) Mkoa wa Shinyanga kutatua kero ya kukatika kwa umeme mara kwa jambo ambalo limekuwa ni kero kwa wananchi na linarudisha nyuma maendeleo.

Utekelezaji wa mradi huo ulianza Februari 2017 na unatarajiwa kukamilika Machi 2019 ambapo tayari sh. bilioni 7.4 zimetumika katika awamu ya kwanza wakati awamu ya pili jumla ya sh. bilioni 22.95 zilitumika.

Matangazo

  • No records found
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • WANUFAIKA WA MIKOPO YA 10% LIPENI KWA WAKATI ILI PIA VIKOPESHWE NA VIKUNDI VINGINE - RC MACHA

    February 13, 2025
  • CP. HAMDUNI AKUTANA NA KAMATI YA MICHEZO YA JWTZ

    February 13, 2025
  • WANANCHI, LIPENI KODI YA ARDHI KWA WAKATI MUEPUKE RIBA - LEO KOMBA

    February 12, 2025
  • WAJUMBE WA BODI, TUMIENI TAALUMA ZENU KUISAIDIA HOSPITALI KUKAMILISHA MIRADI YA UJENZI- RAS CP. HAMDUNI.

    February 11, 2025
  • Angalia zote

Video

MIFUKO BANDIA ZAIDI YA ELFU 20 YAKAMATWA SHINYANGA
Video Nyinginezo

Viunganishi vya Haraka

  • Historia
  • Dira na Dhima
  • Hotuba Mbalimbali
  • Video Mbalimbali
  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Picha za Matukio
  • Miongozo na kanuni

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Mfumo wa kutuma, kupokea na kufuatilia malalamiko, mapendekezo, maulizo na pongezi
  • Ofisi ya Rais Menejimenti ya utumishi wa Umma
  • Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Boma Street, Mwanza Road

    Anuani: P.O.Box 320, Shinyanga

    Simu: +255 28 2762222

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras@shinyanga.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2018. Mkoa wa Shinyanga. Haki zote zimehifadhiwa