• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
    • eVibali |
Shinyanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Shinyanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Yetu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
      • Afya
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Shinyanga
    • Wilaya ya Kahama
    • Wilaya ya Kishapu
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu
    • Halmashauri ya Mji wa Kahama
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu
    • Halmashauri ya Wilaya ya Msalala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
    • Bandari Kavu
  • Huduma
    • Kutoa Ushauri wa Kitaalam
    • Kutafsiri Sheria na Sera
    • Kuratibu Shughuli za Wadau
    • Ulinzi na Usalama
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Tafiti
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha

Wahusika wa Mimba za utotoni na Ukatili wa watoto wapewa angalizo

Posted on: February 4th, 2020

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Shinyanga Kamishna Msaidizi wa Polisi Debora Magiligimba ametoa angalizo kwa watendaji wanaoshiriki kuwaficha watuhumiwa wanaowapatia mimba watoto wa shule na wanaofanya ukatili kwa watoto kuwa wataingia kwenye matatizo.

Akizungumza katika kikao cha Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Mhe. Zainab Telack na Watendaji wa kata, Maafisa Elimu kata pamoja na Wakuu wa shule za msingi na sekondari leo tarehe 04/02/2020 kwenye ukumbi wa shule ya sekondari Mwalimu Nyerere, Magiligimba amesema kuwa, kuna baadhi ya watumishi wanashiriki kuwafumbia macho watuhumiwa hao.

"Natoa angalizo kwa Watumishi wanaojiingiza kwenye hili, mtaingia kwenye matatizo. Kwa kipindi hiki cha mapambano ya mimba za utotoni, tupeni taarifa, tutawakamata wote" amesema.

Wakati huo huo, Mkuu wa Mkoa amemuagiza Kamanda wa Polisi Mkoa kuhakikisha wazazi wote wanaowazuia watoto kwenda sekondari wanakamatwa mara moja.

"Kamata wazazi wote ambao watoto wao hawajaripoti shule hadi sasa na dhamana ya kutoka ni watoto wao kwenda shule" amesisitiza Mhe. Telack.

Aidha, katika kikao hicho Telack ametoa rai kwa walimu wa kike kufanya kazi kwa kujiamini bila kuyumbishwa na mtu yeyote kwa sababu za kimapenzi.

"Hakuna mtu atakufukuza kazi kwa sababu ya kumkatalia kimapenzi. Ukiona kiongozi anakujia vibaya njoo kwangu, nitawalinda kwa nguvu zote, simameni imara" amesema Telack.

Amesisitiza pia kuwa na mahusiano mazuri ya kikazi ili kuepukana na migogoro isiyo ya lazima.

Mhe. Telack amemaliza ziara yake katika Halmashauri ya Msalala leo, ambapo kesho ataendelea kwenye Halmashauri ya Mji Kahama.

Matangazo

  • No records found
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • WANUFAIKA WA MIKOPO YA 10% LIPENI KWA WAKATI ILI PIA VIKOPESHWE NA VIKUNDI VINGINE - RC MACHA

    February 13, 2025
  • CP. HAMDUNI AKUTANA NA KAMATI YA MICHEZO YA JWTZ

    February 13, 2025
  • WANANCHI, LIPENI KODI YA ARDHI KWA WAKATI MUEPUKE RIBA - LEO KOMBA

    February 12, 2025
  • WAJUMBE WA BODI, TUMIENI TAALUMA ZENU KUISAIDIA HOSPITALI KUKAMILISHA MIRADI YA UJENZI- RAS CP. HAMDUNI.

    February 11, 2025
  • Angalia zote

Video

MIFUKO BANDIA ZAIDI YA ELFU 20 YAKAMATWA SHINYANGA
Video Nyinginezo

Viunganishi vya Haraka

  • Historia
  • Dira na Dhima
  • Hotuba Mbalimbali
  • Video Mbalimbali
  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Picha za Matukio
  • Miongozo na kanuni

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Mfumo wa kutuma, kupokea na kufuatilia malalamiko, mapendekezo, maulizo na pongezi
  • Ofisi ya Rais Menejimenti ya utumishi wa Umma
  • Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Boma Street, Mwanza Road

    Anuani: P.O.Box 320, Shinyanga

    Simu: +255 28 2762222

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras@shinyanga.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2018. Mkoa wa Shinyanga. Haki zote zimehifadhiwa