• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
    • eVibali |
Shinyanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Shinyanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Yetu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
      • Afya
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Shinyanga
    • Wilaya ya Kahama
    • Wilaya ya Kishapu
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu
    • Halmashauri ya Mji wa Kahama
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu
    • Halmashauri ya Wilaya ya Msalala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
    • Bandari Kavu
  • Huduma
    • Kutoa Ushauri wa Kitaalam
    • Kutafsiri Sheria na Sera
    • Kuratibu Shughuli za Wadau
    • Ulinzi na Usalama
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Tafiti
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha

SERIKALI HAITAKUWA NA MUHALI KWA YEYOTE ATAKAYEKAMATWA KWA WIZI WA MAJI- RC MACHA

Posted on: April 14th, 2025

Na. Paul Kasembo, SHY RS.

MKUU wa Mkoa wa Shinyanga Mhe. Anamringi Macha amewatahadharisha wale wote wenye nia ovu ya kujipatia huduma ya maji kwa njia isiyokuwa halali (kuiba) kuacha haraka iwezekanavyo kwani Serikali haipo tayari kufanya utetezi kwa aina ya mtu huyo, na badala yake itamchukulia hatua za kisheria ikiwemo kumfikisha kwenye vyombo vya sheria.

RC Macha ameyasema hayo leo Aprili 14, 2025 alipokuwa akiongea na watumishi wa Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Shinyanga (SHUWASA) ambao walifika katika Viwanja vya Ofisi ya Mkuu wa Mkoa kwenye hafla ya kukabidhi Magari mawili (2) mapya yenye thamani ya takribani Milioni 276 yenye lengo la kuboresha utendaji kazi wa Mamlaka hiyi SHUWASA.

"Serikali haipo tayari kabisa kumtetea mtu yeyote na wala haitakuwa na  muhali kwa  mwananchi yeyote mwenye nia ovu ya kujipatia huduma ya maji kwa njia isiyokuwa halali, na badala yake itamchukulia hatua za kisheria ikiwemo kumfikisha Mahakamani ili iwe mfano kwa yeyote asiyeitakia mama Mamlaka," amesema RC Macha.

RC Macha akiwa ameambatana na ndugu David Lyamongi ambaye aliyemuwakilisha Katibu Tawala Mkoa wa Shinyanga CP. Salum Hamduni ametumia nafasi hiyo kuipongeza Menejimenti ya SHUWASA inayoongozwa na Mhandisi Yusuph Katopola na watumishi wote kwa kazi nzuri wanayoifanya katika kuhakikisha huduma ya maji inawafikia wananchi kwa asilimia 95 Mjini na 85 kwa maeneo ya Vijijini huku pongezi zaidi ni kwa utekelezaji wa mradi wa Majisafi na Usafi wa Mazingira katika Manispaa ya Shinyanga na Miji inayokuwa kwa kasi ikiwemo Tinde, Didia na Iselamagazi huku ikitajwa takribani Bilioni 231 zinatarajiwa kutumika katika mradi huo.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa SHUWASA Mha.Yusuph Katopola amekili kupokea malekezo na ushauri wa RC Macha huku akiongeza kwa kusema kuwa Magari hayo yanakwenda kuchechemua usimamizi, ufuatiliaji na ufanisi wa mradi na lengo likiwa ni kuhakikisha huduma ya maji inafikia 95% kwa Mjini na 85% kwa Vijijini na zaidi kufikia 98% baada ya kukamilika kwa mradi huo mwaka 2028.



Matangazo

  • No records found
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • ENDELEENI KUTOA ELIMU ZAIDI KUHUSU AFYA YA AKILI - DC. MBONI

    May 30, 2025
  • TAKUKURU SHINYANGA YAANZA KUCHUKUA HATUA DHIDI YA UBADHIRIFU WA SHILINGI MILIONI 92 ZA WAKULIMA WA TUMBAKU WA USHETU - DONASIAN.

    May 27, 2025
  • MAISHA BAADA YA KUSTAAFU YANAHITAJI UTULIVU - DC. MTATIRO

    May 26, 2025
  • MAFUNZO YA IPOSA NI MKOMBOZI KWA VIJANA WALIO WENGI WANAOKOSA FURSA YA ELIMU YA KAWAIDA - RC. MACHA

    May 23, 2025
  • Angalia zote

Video

MIFUKO BANDIA ZAIDI YA ELFU 20 YAKAMATWA SHINYANGA
Video Nyinginezo

Viunganishi vya Haraka

  • Historia
  • Dira na Dhima
  • Hotuba Mbalimbali
  • Video Mbalimbali
  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Picha za Matukio
  • Miongozo na kanuni

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Mfumo wa kutuma, kupokea na kufuatilia malalamiko, mapendekezo, maulizo na pongezi
  • Ofisi ya Rais Menejimenti ya utumishi wa Umma
  • Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Boma Street, Mwanza Road

    Anuani: P.O.Box 320, Shinyanga

    Simu: +255 28 2762222

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras@shinyanga.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2018. Mkoa wa Shinyanga. Haki zote zimehifadhiwa