• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
    • eVibali |
Shinyanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Shinyanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Yetu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
      • Afya
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Shinyanga
    • Wilaya ya Kahama
    • Wilaya ya Kishapu
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu
    • Halmashauri ya Mji wa Kahama
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu
    • Halmashauri ya Wilaya ya Msalala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
    • Bandari Kavu
  • Huduma
    • Kutoa Ushauri wa Kitaalam
    • Kutafsiri Sheria na Sera
    • Kuratibu Shughuli za Wadau
    • Ulinzi na Usalama
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Tafiti
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha

SERIKALI IMEONGEZA WIGO WA HUDUMA ZA WATOTO - MHE. MAJALIWA

Posted on: September 7th, 2024

Dar es salaam.

WAZIRI Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa amesema kuwa Serikali imefanya mageuzi makubwa kwa kuongeza wigo wa upatikanaji wa huduma kwa watoto wachanga.

Mhe. Majaliwa ameyasema hayo leo Jumamosi, Septemba 7, 2024 wakati akizungumza na viongozi na wadau walioshiriki mbio za hisani za 2024 zilizoandaliwa na Benki ya Maendeleo (Maendeleo Bank Marathon 2024) katika viwanja vya Green Park, Oysterbay, jijini Dar es Salaam.

"Serikali imekuwa ikitekeleza mikakati na afua mahsusi za kuhakikisha upatikanaji wa huduma bora kwa watoto wachanga. Ni jambo la fahari sana kuwa hivi sasa huduma maalum za watoto wachanga na ile ya Mama Kangaroo hadi kufikia Julai 2024, zimeanzishwa katika hospitali 245,” amesema Mhe. Majaliwa.

Waziri Mkuu amesema mafanikio haya yametokana na dhamira ya dhati ya Serikali ya Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ya kuhakikisha Tanzania inapunguza vifo vya watoto wachanga kufikia lengo namba tatu la Maendeleo Endelevu la vifo chini ya 12 katika kila vizazi hai 1,000 kwa mwaka 2030 kutoka vifo 24 kwa kila vizazi hai 1,000 kwa mwaka 2022.

Akizungumzia kuhusu kaulimbiu ya tukio hilo ambayo ni Hatua ya Faraja - Msimu wa Pili, Waziri Mkuu amesema kaulimbiu yao inasawiri mpango wa Benki hiyo wa kuendeleza kazi yao ya mwaka jana ya ununuzi wa vitanda maalumu vya kutunzia watoto njiti (Infant Baby Warmer) katika Hospitali ya KCMC.

Sambamba na ujenzi wa kituo kipya cha watoto wenye changamoto ya ulemavu wa akili na usonji kinachotarajiwa kujengwa wilayani Bagamoyo

“Kama mlivyosikia, pale KCMC, idadi ya vifo vya watoto wanaozaliwa njiti ni kubwa na ipo kati ya asilimia 20 mpaka 25. Hawa ni binadamu wenzetu wanaostahili kuishi na tuna kila sababu ya kuonesha upendo kwa kuchangia hatua za faraja.

"Hivyo basi, nitoe wito kwa wananchi wote wenye mapenzi mema kuendelea kuiunga mkono Benki ya Maendeleo katika utekelezaji wa afua hizi muhimu,” amesisitiza.

Amewapongeza viongozi wa benki hiyo kwa kuongeza lengo la uchangiaji kwenye mbio za mwaka huu kutoka sh. milioni 120 hadi sh. milioni 200 ili kukamilisha kazi waliyoianza mwaka 2023.


Matangazo

  • No records found
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • WANUFAIKA WA MIKOPO YA 10% LIPENI KWA WAKATI ILI PIA VIKOPESHWE NA VIKUNDI VINGINE - RC MACHA

    February 13, 2025
  • CP. HAMDUNI AKUTANA NA KAMATI YA MICHEZO YA JWTZ

    February 13, 2025
  • WANANCHI, LIPENI KODI YA ARDHI KWA WAKATI MUEPUKE RIBA - LEO KOMBA

    February 12, 2025
  • WAJUMBE WA BODI, TUMIENI TAALUMA ZENU KUISAIDIA HOSPITALI KUKAMILISHA MIRADI YA UJENZI- RAS CP. HAMDUNI.

    February 11, 2025
  • Angalia zote

Video

MIFUKO BANDIA ZAIDI YA ELFU 20 YAKAMATWA SHINYANGA
Video Nyinginezo

Viunganishi vya Haraka

  • Historia
  • Dira na Dhima
  • Hotuba Mbalimbali
  • Video Mbalimbali
  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Picha za Matukio
  • Miongozo na kanuni

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Mfumo wa kutuma, kupokea na kufuatilia malalamiko, mapendekezo, maulizo na pongezi
  • Ofisi ya Rais Menejimenti ya utumishi wa Umma
  • Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Boma Street, Mwanza Road

    Anuani: P.O.Box 320, Shinyanga

    Simu: +255 28 2762222

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras@shinyanga.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2018. Mkoa wa Shinyanga. Haki zote zimehifadhiwa