• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
    • eVibali |
Shinyanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Shinyanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Yetu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
      • Afya
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Shinyanga
    • Wilaya ya Kahama
    • Wilaya ya Kishapu
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu
    • Halmashauri ya Mji wa Kahama
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu
    • Halmashauri ya Wilaya ya Msalala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
    • Bandari Kavu
  • Huduma
    • Kutoa Ushauri wa Kitaalam
    • Kutafsiri Sheria na Sera
    • Kuratibu Shughuli za Wadau
    • Ulinzi na Usalama
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Tafiti
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha

SERIKALI KUHUDUMIA WAHANGA WOTE WA MAFURIKO SHINYANGA

Posted on: December 7th, 2023

Na. Shinyanga RS

Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Mhe. Christina Mndeme leo tarehe 6 Novemba, 2023 amewatembelea wahanga wa maafa walioezuliwa  na kubomolewa makazi yao katika kata ya Kizumbi na Mwamala kufuatia mvua kubwa iliyonyesha usiku wa kuamkia terehe 6 Desemba, 2023.

Akizungumza na wahanga hao Mhe. Mndeme amewapa pole sana na kuwaeleza kuwa serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan imepokea kwa masikitiko makubwa taatifa za mafuriko haya na kwamba sasa serikali itatoa huduma ya matibabu bure mpaka kupona kwa majeruhi wote, italeta mbegu kwa waathirika wa mashamba, italeta vifaa vya kulalia na itafanya tathimini ya awali ili kujuwa kiasi cha hasara iliyopatikana na mahitaji halisi. 

"Poleni sana ndugu zetu kwa tukio hili, lakini tu niseme kuwa serkali itagharamia matibabu wa majeruhi, kuleta mbegu, vifaa vya kulalia, pia nimuagize Mkuu wa Wilaya ya Shinyanga kufanya tathimini ya awali kujuwa uhalisia wa mahitaji na hasara iliyopatikana ili serikali ijue, niseme tu kuwa, haya ndiyo maelekezo ya Rais wetu Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa wahanga wote," alisema Mhe. Mndeme.

Awali akitoa taarifa ya hali ilivyokuwa, Diwani wa Kata ya Kizumbi Mhe. Reuben Kitinya alisema kuwa, mvua iliyonyesha usiku wa kuamkia tarehe 6 Desemba, 2023 iliyoambatana na upepo mkali pamoja na barafu ndiyo iliyoleta athari yote hiyo huku akisema jumla ya nyumba 31 zimeathirika kwa kung'olewa bati na kaya 27 kubomoka kabisa na hivyo kupelekea wananchi hao kuombewa hifadhi kwa ndugu na jamaa.

Aidha kwa Kata ya Mwamala jumla ya nyumba 51 zimeathirika na mvua hizo pamoja na hekari takribani 10 kuharibiwa kabisa na mvua ya barafu iliyoambatana na upepo mkali katika kijiji cha Ibanza sanjali na kuumiza watu wanne akiwemo bibi kizee ambaye amelazwa hospitali ya Mwawaza.

Mhe. Mndeme ametoa wito kwa wananchi wote kuendelea kuchukua tahadhari ya mvua hizi zilizotabiriwa na Mamlaka ya Hali ya Hewa kuwa zitakuwa za juu ya kiwango, kuondoka maeneo yote hatarishi.


HABARI PICHA




Matangazo

  • No records found
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • NATOA WITO KWA VIJANA HAPA SHINYANGA KUREJEA NA KUTATHIMINI UPYA NJIA ZA KUJIPATIA KIPATO - RC. MACHA

    May 20, 2025
  • SERIKALI YATHIBITISHA VIFO VYA WATU SITA NA MAJERUHI 11 KATIKA AJALI YA MGODI WA MWAKITOLYO.

    May 18, 2025
  • WAZAZI NA WALEZI, NENDENI MKAWE MABALOZI SAHIHI WA KAZI ZA MHE. RAIS DKT. SAMIA SULUHU HASSAN – RC. MACHA

    May 16, 2025
  • WAZAZI NA WALEZI WEKEZENI ZAIDI KATIKA MALEZI NA MAKUZI YA WATOTO – LYAMONGI

    May 15, 2025
  • Angalia zote

Video

MIFUKO BANDIA ZAIDI YA ELFU 20 YAKAMATWA SHINYANGA
Video Nyinginezo

Viunganishi vya Haraka

  • Historia
  • Dira na Dhima
  • Hotuba Mbalimbali
  • Video Mbalimbali
  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Picha za Matukio
  • Miongozo na kanuni

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Mfumo wa kutuma, kupokea na kufuatilia malalamiko, mapendekezo, maulizo na pongezi
  • Ofisi ya Rais Menejimenti ya utumishi wa Umma
  • Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Boma Street, Mwanza Road

    Anuani: P.O.Box 320, Shinyanga

    Simu: +255 28 2762222

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras@shinyanga.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2018. Mkoa wa Shinyanga. Haki zote zimehifadhiwa