Na. Paul Kasembo Shy RS.
Makamu Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (BARA) ndugu Stephen Wasira amemtaka Mkandarasi anayefanya Ukarabati Mkubwa wa Uwanja wa Ndege wa Shinyanga kukamilisha kazi hiyo kwa wakati ili uweze kuongeza fursa zaidi ukizingatia kuwa Shinyanga ni Mkoa wa Madini.
Ndugu Wasira ameyasema hayo leo Machi 28, 2025 alipotembelea uwanjani hapo ili kuona mwenendo wa ukarabati huo ambao kwa mujibu wa taarifa ya Mkandarasi China Henan International Cooperation Group Co. Ltd (CHICO) unaotarajiwa kukamilika ifikapo Juni, 2025.
"Mkoa wa Shinyanga ni Madini, naufahamu Mkoa huu ambapo ndiyo wenye madini ya Almasi kutoka hapo Mwadui, lakini tumetoka Wilaya ya Kahama ambapo kuna madini mengi ya Dhahabu na maeneo mengi hapa Shinyanga yanatoa madini, kwa hiyo kamilisheni kwa wakati ili muongeze fursa na mzunguko wa fedha kupitia uwanja huu," alisema Ndg. Wasira.
Aidha, amesema kuwa uwanja utakapokamilika yeye mwenyewe ndugu Wasira atawashawishi Shirika la Ndege la Tanzania (ATCL) @airtanzania_atcl ili waanze safari zao kuja Shinyanga na yeye atakuwa mmoja wa watakaokuja na ATCL katika safari yao ya kwanza hapa ili aje ashuhudie kuanza rasmi kwa matumizi ya uwanja huo unaotajwa kuwa mkombozi kwa Shinyanga na maeneo jirani.
Hii siku ya tatu ya ziara ya ndugu Wasira hapa mkoani Shinyanga ambapo alitembelea na kufanya mikutano katika Wilaya ya Shinyanga, Kahama na leo Machi 28, 2025 atamalizia na Wilaya ya Kishapu.
Boma Street, Mwanza Road
Anuani: P.O.Box 320, Shinyanga
Simu: +255 28 2762222
Simu ya Mkononi:
Barua Pepe: ras@shinyanga.go.tz
Hakimiliki@2018. Mkoa wa Shinyanga. Haki zote zimehifadhiwa