• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
    • eVibali |
Shinyanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Shinyanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Yetu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
      • Afya
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Shinyanga
    • Wilaya ya Kahama
    • Wilaya ya Kishapu
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu
    • Halmashauri ya Mji wa Kahama
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu
    • Halmashauri ya Wilaya ya Msalala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
    • Bandari Kavu
  • Huduma
    • Kutoa Ushauri wa Kitaalam
    • Kutafsiri Sheria na Sera
    • Kuratibu Shughuli za Wadau
    • Ulinzi na Usalama
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Tafiti
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha

Shinyanga yaazimia kupambana na mimba kwa wanafunzi

Posted on: July 21st, 2017

Wadau wa Elimu Mkoani Shinyanga wameazimia kwa pamoja kuhakikisha tatizo la mimba kwa wanafunzi linakwisha kwa kuzitaka kila Halmashauri kuweka mkakati wa kutoa elimu ya kujitambua kwa watoto wa kike na kujenga shule angalau mbili.

Maazimio hayo yamefikiwa katika kikao cha kila mwaka cha wadau kilichojadili changamoto zinazoikabili sekta ya elimu Mkoani hapa, kilichofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa.

Katika kikao hicho kilichoongozwa na Katibu Tawala wa Mkoa wa Shinyanga Bw. Albert Msovela, suala la mimba za utotoni limechukua nafasi ya wadau kujadili kwa mapana na kufikia maazimio hayo ambapo wadau wamesisitiza kuwa, iwapo watoto wa kike watapata elimu ya kujitambua, itawasaidia kujiepusha na vishawishi vya kujiingiza kwenye matendo mabaya. 

Maazimio mengine ni pamoja na kuendelea kuwapima wanafunzi wa kike ujauzito kila baada ya miezi mitatu, kuwataka watoto wa kike kutembea kwa makundi na pia kila shule kuwa na mwalimu wa kike angalau mmoja.

Pamoja na malengo hayo, wadau wameazimia kuhakikisha kila Halmashauri inaongeza vyumba vya madarasa na madawati ili kukabiliana ongezeko la wanafunzi kila mwaka wanaoandikishwa darasa la kwanza na wanaojiunga na kidato cha kwanza.

Aidha, Wakurugenzi wa Mamlaka za Serikali za Mitaa wamesisitizwa kuweka bajeti za kuboresha miundombinu ya shule zenye kidato cha tano na sita ili wanafunzi wanaofaulu kidato cha nne wapate nafasi katika shule hizo. Imesisitizwa pia kwa mwaka wa fedha 2017/2018 Halmashauri za Mji Kahama na Manispaa ya Shinyanga zijenge shule za kidato cha tano na sita ili kuongeza idadi ya wanafunzi waliofanya vizuri kidato cha nne.

Akifunga kikao hicho, Bw. Msovela amewataka kila mmoja afanye kazi kwa nafasi yake ili kuyatekeleza yote yaliyokubaliwa na kuondoa changamoto zinazoikabili Sekta ya elimu, aidha amepongeza Sekta binafsi kwa mchango wao wa kufanya Mkoa uwe katika nafasi nzuri ya ufaulu.


Matangazo

  • No records found
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • WANUFAIKA WA MIKOPO YA 10% LIPENI KWA WAKATI ILI PIA VIKOPESHWE NA VIKUNDI VINGINE - RC MACHA

    February 13, 2025
  • CP. HAMDUNI AKUTANA NA KAMATI YA MICHEZO YA JWTZ

    February 13, 2025
  • WANANCHI, LIPENI KODI YA ARDHI KWA WAKATI MUEPUKE RIBA - LEO KOMBA

    February 12, 2025
  • WAJUMBE WA BODI, TUMIENI TAALUMA ZENU KUISAIDIA HOSPITALI KUKAMILISHA MIRADI YA UJENZI- RAS CP. HAMDUNI.

    February 11, 2025
  • Angalia zote

Video

MIFUKO BANDIA ZAIDI YA ELFU 20 YAKAMATWA SHINYANGA
Video Nyinginezo

Viunganishi vya Haraka

  • Historia
  • Dira na Dhima
  • Hotuba Mbalimbali
  • Video Mbalimbali
  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Picha za Matukio
  • Miongozo na kanuni

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Mfumo wa kutuma, kupokea na kufuatilia malalamiko, mapendekezo, maulizo na pongezi
  • Ofisi ya Rais Menejimenti ya utumishi wa Umma
  • Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Boma Street, Mwanza Road

    Anuani: P.O.Box 320, Shinyanga

    Simu: +255 28 2762222

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras@shinyanga.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2018. Mkoa wa Shinyanga. Haki zote zimehifadhiwa