• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
    • eVibali |
Shinyanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Shinyanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Yetu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
      • Afya
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Shinyanga
    • Wilaya ya Kahama
    • Wilaya ya Kishapu
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu
    • Halmashauri ya Mji wa Kahama
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu
    • Halmashauri ya Wilaya ya Msalala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
    • Bandari Kavu
  • Huduma
    • Kutoa Ushauri wa Kitaalam
    • Kutafsiri Sheria na Sera
    • Kuratibu Shughuli za Wadau
    • Ulinzi na Usalama
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Tafiti
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha

SHIRIKIANENI NA MFANYE KAZI KWA KARIBU NA OFISI YA CAG - RC MACHA

Posted on: June 28th, 2024

Na. Paul Kasembo, KAHAMA MC.

MKUU wa Mkoa wa Shinyanga Mhe. Anamringi Macha amewataka watalaam wakiongozwa na Wakurugenzi wao kubadilika na kuanza kushirikiana na kufanya kazi kwa karibu zaidi wakati wote na ofisi ya Mdhibiti na Mkaguzi wa Hesabu za Serikali (CAG) ili waweze kuzipunguza kama siyo kuziondoa hoja zote badala ya kusubiria wakati wa ukaguzi ili waanze kupambana kujibu wakati nafasi ilikuwepo ya kufanya hivyo awali.

RC Macha ameyasema haya leo tarehe 28 Juni, 2024 alipokuwa akifunga mkutano maalum wa baraza la madiwani katika Manispaa ya Kahama ikiwa ni hitimisho la mikutano maalum ya CAG kwa Halmashauri zote sita (6) zinazounda Mkoa wa Shinyanga huku akisisitiza umuhimu wa waheshimiwa madiwani kusimamia miradi ya maendeleo kwa wananchi wao ili waweze kuaminika na kupata hati safi za vipimo vya wananchi na wapate ridhaa tena ya kuongoza ukizingatia kuwa wananchi nao wanayo nafasi ya kupimwa kwa wananchi wao.

"Niwashauri sana wataalam wetu mkiongozwa na wakurugenzi wenu mbadilike na muanze kushirikiana kwa kufanya kazi kwa karibu zaidi wakati wote na ofisi ya CAG ili itakapofika wakati wa ukaguzi muweze kuziondoa kama siyo kuzifuta hoja zote badala ya kusubiria ufike muda wa ukaguzi ndiyo muanze kupambana kuziondoa wakati mlikuwa na hiyo nafasi kufanya kazi pamoja na kushirikiana," amesema RC Macha.

Aidha RC Macha ameitaka Manispaa ya Kahama kuhakikisha wanavipata vikundi vyote vioivyotajwa kuwa havionekani baada ya kukopa fedha kutoka kwenye mfuko wa asilimia 10 ambapo wanawake 4%, vijana 4% na watu wenye ulemavu 2% ili waweze kuzirejesha pamoja na kujibu hoja ya CAG inayotokana na madeni hayo.

Akiwasilisha taarifa ya utekelezaji wa mapendekezo ya CAG kwa 2022/2023 Mkuu wa Kitengo cha Fedha na Uhasibu ndg. Godwin Dinda kwa niaba ya Mkurugenzi ndg. Masudi Kibeto amesema kuwa Manispaa ya Kahama ilikuwa na hoja 25 ambapo hoja 9 zimejibiwa na kufungwa, huku 12 zikiwa kwenye utekelezaji, hoja 3 hazijatekelezwa na hoja 1 imejirudia.

Akiahirisha baraza Mstahiki Meya wa Manispaa ya Kahama Mhe. Yahaya Bundala amesema kuwa wamepokea pongezi zote kwa kupata hati safi mfululizo, wamepokea maelekezo, ushauri na mapendekezo yote yaliyotolewa na viongozi na kwamba wanakwenda kuyatekeleza kikamilifu ili mwaka wa fedha ujao wasiwe na hoja kabisa.

mh

Mstahiki Meya Manispaa ya Kahama Mhe. Yahaya Bundala

Mkurugenzi wa Manispaa ya Kahama ndg. Masudi Kibeto

Wataalam kutoka Ofisi ya RAS - Shinyanga pamoja na Ofisi ya CAG

Sehemu ya wataalam kutoka ofisi ya Manispaa ya Kahama

Waheahimiwa madiwani Manispaa ya Kahama

Matangazo

  • No records found
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • NATOA WITO KWA VIJANA HAPA SHINYANGA KUREJEA NA KUTATHIMINI UPYA NJIA ZA KUJIPATIA KIPATO - RC. MACHA

    May 20, 2025
  • SERIKALI YATHIBITISHA VIFO VYA WATU SITA NA MAJERUHI 11 KATIKA AJALI YA MGODI WA MWAKITOLYO.

    May 18, 2025
  • WAZAZI NA WALEZI, NENDENI MKAWE MABALOZI SAHIHI WA KAZI ZA MHE. RAIS DKT. SAMIA SULUHU HASSAN – RC. MACHA

    May 16, 2025
  • WAZAZI NA WALEZI WEKEZENI ZAIDI KATIKA MALEZI NA MAKUZI YA WATOTO – LYAMONGI

    May 15, 2025
  • Angalia zote

Video

MIFUKO BANDIA ZAIDI YA ELFU 20 YAKAMATWA SHINYANGA
Video Nyinginezo

Viunganishi vya Haraka

  • Historia
  • Dira na Dhima
  • Hotuba Mbalimbali
  • Video Mbalimbali
  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Picha za Matukio
  • Miongozo na kanuni

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Mfumo wa kutuma, kupokea na kufuatilia malalamiko, mapendekezo, maulizo na pongezi
  • Ofisi ya Rais Menejimenti ya utumishi wa Umma
  • Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Boma Street, Mwanza Road

    Anuani: P.O.Box 320, Shinyanga

    Simu: +255 28 2762222

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras@shinyanga.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2018. Mkoa wa Shinyanga. Haki zote zimehifadhiwa