• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
    • eVibali |
Shinyanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Shinyanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Yetu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
      • Afya
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Shinyanga
    • Wilaya ya Kahama
    • Wilaya ya Kishapu
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu
    • Halmashauri ya Mji wa Kahama
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu
    • Halmashauri ya Wilaya ya Msalala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
    • Bandari Kavu
  • Huduma
    • Kutoa Ushauri wa Kitaalam
    • Kutafsiri Sheria na Sera
    • Kuratibu Shughuli za Wadau
    • Ulinzi na Usalama
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Tafiti
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha

"Sitaruhusu nyumba ya mwananchi kuuzwa kwa sababu ya riba" - RC

Posted on: July 21st, 2017

Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Mhe. Zainab Telack amezitaka taasisi za fedha zinazokopesha kuwaambia ukweli wananchi kuhusu riba na kiasi cha fedha wanachotakiwa kulipa.

Mhe. Telack ametoa agizo hilo katika kikao cha pamoja na wafanyabiashara wa Mkoa wa Shinyanga kilichofanyika katika Ukumbi wa Mikutano wa Ofisi yake.

Telack amesema hatakubaliana na biashara hizo kwani wananchi wengi wamekuwa wakiumizwa na madeni kutoka kwenye taasisi hizo na kufikia kuuzwa kwa mali zao ili kufidia madeni. “Taasisi hizi haziwasaidii wananchi wengi na matokeo yake kuwaumiza”

“Mikopo iwe ni kwa ustawi wa wananchi na kwa maendeleo yao” amesisitiza Mhe. Telack.

Mhe. Telack amesema kuwa taasisi hizo wanatumia uelewa mdogo wa wananchi kuwaumiza kwa mikopo yenye riba kubwa kuliko uwezo wao.

Aidha, taasisi hizo pia zimeshauriwa kutumia lugha ya Kiswahili ambayo wananchi wengi wanaimudu ili waweze kuelewa wakati wa kujaza fomu za mikopo.

Katika kikao hicho, Wafanyabiashara wametakiwa kuwa na ushirikiano baina yao pamoja na Serikali ili kuweza kutambua fursa mbalimbali zilizopo katika Mkoa na kuwekeza kwa manufaa yao na Mkoa wa ujumla. Telack amesema Ofisi yake iko wazi kutoa msaada wa aina yoyote kwa wafanyabiashara.

Aidha, Mhe. Telack ametoa rai kwa wafanyabiashara wa Mkoa wa Shinyanga kujitangaza kwa kushiriki maonesho mbalimbali ikiwemo maadhimisho ya Wakulima yaani Nane nane yanayofanyika Mwezi ujao, pamoja na kuandaa maonesho ya bidhaa zao kimkoa.

Matangazo

  • No records found
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • RC MHITA AWAHAMASISHA WAFANYABIASHARA NA WAWEKEZAJI KUCHANGAMKIA FURSA ZA KIUCHUMI MKOANI SHINYANGA

    November 13, 2025
  • RC MHITA AKUTANA NA MSANII BANDO MC, APONGEZA JUHUDI ZA KUSAIDIA VIJANA SHINYANGA

    November 11, 2025
  • RC MHITA APONGEZA UONGOZI MPYA WA KANISA LA WASABATO NGBF MKOANI SHINYANGA.

    November 07, 2025
  • WANAFUNZI 29,193 KUFANYA MTIHANI WA UPIMAJI KIDATO CHA PILI SHINYANGA.

    November 07, 2025
  • Angalia zote

Video

RC MHITA AWAHAMASISHA WAFANYABIASHARA NA WAWEKEZAJI KUCHANGAMKIA FURSA ZA KIUCHUMI MKOANI SHINYANGA
Video Nyinginezo

Viunganishi vya Haraka

  • Historia
  • Dira na Dhima
  • Hotuba Mbalimbali
  • Video Mbalimbali
  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Picha za Matukio
  • Miongozo na kanuni

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Mfumo wa kutuma, kupokea na kufuatilia malalamiko, mapendekezo, maulizo na pongezi
  • Ofisi ya Rais Menejimenti ya utumishi wa Umma
  • Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    OFISI YA MKUU WA MKOA, MKOA WA SHINYANGA, 04 MTAA WA BOMA

    Anuani: P.O.Box 320, 37180,SHINYANGA, TANZANIA

    Simu: +255 28 2762222

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras@shinyanga.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2018. Mkoa wa Shinyanga. Haki zote zimehifadhiwa