• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
    • eVibali |
Shinyanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Shinyanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Yetu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
      • Afya
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Shinyanga
    • Wilaya ya Kahama
    • Wilaya ya Kishapu
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu
    • Halmashauri ya Mji wa Kahama
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu
    • Halmashauri ya Wilaya ya Msalala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
    • Bandari Kavu
  • Huduma
    • Kutoa Ushauri wa Kitaalam
    • Kutafsiri Sheria na Sera
    • Kuratibu Shughuli za Wadau
    • Ulinzi na Usalama
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Tafiti
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha

SOKO LA KAMBARAGE KUJENGWA UPYA KUPITIA MRADI WA TACTIC, RC MHITA AONGOZA USAFI NA KUTOA WITO WA KULINDA MAZINGIRA

Posted on: September 20th, 2025

Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, Mhe. Mboni Mhita  leo Septemba 20, 2025 ameongoza zoezi la usafi katika Soko la Kambarage, Manispaa ya Shinyanga, ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya Siku ya Usafishaji Duniani huku akibainisha kuwa soko hilo lipo mbioni kubomolewa ili kupisha ujenzi wa soko jipya la kisasa kupitia mradi wa TACTIC.

Akizungumza baada ya usafi huo, Mhe. Mhita amesema Serikali imeshapata fedha kwa ajili ya ujenzi wa soko jipya, na kwamba maandalizi ya utekelezaji wa mradi huo yamekamilika, hivyo wananchi wanapaswa kujiandaa na mabadiliko hayo kwa mtazamo chanya.

“Mradi huu wa TACTIC utaliwezesha Soko la Kambarage kuwa la kisasa zaidi, lenye miundombinu bora ya biashara. Lakini pamoja na mabadiliko haya yanayokuja, tunapaswa kuendeleza tabia ya kufanya usafi wa mazingira wakati wote usafi ni afya, si jambo la kulazimishwa,” amesema Mhita.

Aidha, RC Mhita amewapongeza wananchi, wafanyabiashara, taasisi mbalimbali na wadau wote waliojitokeza kushiriki usafi huo, na kutoa rai kwa jamii kuendelea kushiriki katika utunzaji wa mazingira kwa maslahi ya afya ya jamii.

Kwa upande wake, Katibu Tawala wa Mkoa wa Shinyanga, CP Salum Hamduni, amesisitiza kuwa zoezi la usafi halipaswi kuwa la siku moja au kwa ajili ya kumbukumbu, bali liwe sehemu ya maisha ya kila siku.

“Zoezi hili la leo lionesha mwitikio mzuri, lakini ni jukumu letu kuhakikisha usafi huu unaendelea kila wiki. Kila mmoja wetu ana wajibu wa kuifanya Shinyanga kuwa mkoa wa mfano katika usafi,” amesema CP Hamduni.

Kauli mbiu ya Siku ya Usafishaji Duniani kwa mwaka huu ni: “Tunza Mazingira kwa Kuzipa Taka Thamani” ikiwa na lengo la kuhamasisha uchakataji wa taka na matumizi mbadala kwa maendeleo endelevu.

Matangazo

  • No records found
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • RC MHITA AWAHAMASISHA WAFANYABIASHARA NA WAWEKEZAJI KUCHANGAMKIA FURSA ZA KIUCHUMI MKOANI SHINYANGA

    November 13, 2025
  • RC MHITA AKUTANA NA MSANII BANDO MC, APONGEZA JUHUDI ZA KUSAIDIA VIJANA SHINYANGA

    November 11, 2025
  • RC MHITA APONGEZA UONGOZI MPYA WA KANISA LA WASABATO NGBF MKOANI SHINYANGA.

    November 07, 2025
  • WANAFUNZI 29,193 KUFANYA MTIHANI WA UPIMAJI KIDATO CHA PILI SHINYANGA.

    November 07, 2025
  • Angalia zote

Video

RC MHITA AWAHAMASISHA WAFANYABIASHARA NA WAWEKEZAJI KUCHANGAMKIA FURSA ZA KIUCHUMI MKOANI SHINYANGA
Video Nyinginezo

Viunganishi vya Haraka

  • Historia
  • Dira na Dhima
  • Hotuba Mbalimbali
  • Video Mbalimbali
  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Picha za Matukio
  • Miongozo na kanuni

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Mfumo wa kutuma, kupokea na kufuatilia malalamiko, mapendekezo, maulizo na pongezi
  • Ofisi ya Rais Menejimenti ya utumishi wa Umma
  • Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    OFISI YA MKUU WA MKOA, MKOA WA SHINYANGA, 04 MTAA WA BOMA

    Anuani: P.O.Box 320, 37180,SHINYANGA, TANZANIA

    Simu: +255 28 2762222

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras@shinyanga.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2018. Mkoa wa Shinyanga. Haki zote zimehifadhiwa