• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
    • eVibali |
Shinyanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Shinyanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Yetu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
      • Afya
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Shinyanga
    • Wilaya ya Kahama
    • Wilaya ya Kishapu
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu
    • Halmashauri ya Mji wa Kahama
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu
    • Halmashauri ya Wilaya ya Msalala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
    • Bandari Kavu
  • Huduma
    • Kutoa Ushauri wa Kitaalam
    • Kutafsiri Sheria na Sera
    • Kuratibu Shughuli za Wadau
    • Ulinzi na Usalama
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Tafiti
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha

TAKUKURU MKOA WA SHINYANGA YARIDHISHWA NA MIRADI YA SEQUIP

Posted on: February 7th, 2024

TAKUKURU Mkoa wa Shinyanga imesema kuwa imeridhishwa na utekelezaji wa Miradi ya SEQUIP Mkoani hapa ambapo kwa kipindi cha robo ya pili ya mwaka wa fedha 2023/2024 ambapo TAKUKURU ilifanya ufuatiliaji katika miradi ya Mpango wa Uboreshaji wa Elimu ya Sekondari SEQUIP ili kuona kama miradi hii inatekelezwa kwa wakati na katika ubora wa viwango vinavyohitajika.

Hayo yamesemwa leo tarehe 7 Februari, 2024 na Mkuu wa TAKUKURU Mkoa wa Shinyanga Ndg. Donasian Kessy alipokuwa akitoa taarifa yake kwa waandishi wa habari ofisini kwake ambapo pamoja na mambo mengine pia amesisitiza umuhimu wa wananchi wa Mkoa wa Shinyanga kutoa ushirikiano kwa serilkali ili kuhakikisha miradi yote inayoendelea katika Mkoa wetu inakamilika kwa wakati na kwa ubora.

"TAKUKURU Mkoa wa Shinyanga umeridhishwa na utekelezaji wa miradi ya Mpango wa Uboreshaji wa Elimu ya Sekondari SEQUIP, na hivyo basi natoa wito kwa wananchi Mkoa wetu kuendelea kutoa ushirikiano kwa Serikali katika kuhakikisha kuwa miradi hii inakamilika kwa wakati na kwa ubora stahiki," amesema Kessy.

Aidha, TAKUKURU imejiwekea mikakati ya utendaji kazi kwa kipindi cha Januari hadi Machi, 2024 ambapo itajikita zaidi kwenye ufuatiliaji wa fedha za miradi ya maendeleo ili kuhakikisha miradi inatekelezwa kwa thamani halisi ya fedha kama serikali ilivyokusudia. Pia itaendelea kufanya warsha za kusimamia utekelezaji wa maazimio yote ya changamoto mbalimbali zilizobainika kwenye chambuzi za mifumo na miradi ya maendeleo.


KUZUIA RUSHWA NI JUKUMU LAKO NA LANGU; TUTIMIZE WAJIBU WETU

Mkuu wa TAKUKURU Mkoa wa Shinyanga Ndg. Donasian Kessy akielezea jambo wakati akizungumza na wanahabari (hawapo hewani)

Matangazo

  • No records found
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • WANUFAIKA WA MIKOPO YA 10% LIPENI KWA WAKATI ILI PIA VIKOPESHWE NA VIKUNDI VINGINE - RC MACHA

    February 13, 2025
  • CP. HAMDUNI AKUTANA NA KAMATI YA MICHEZO YA JWTZ

    February 13, 2025
  • WANANCHI, LIPENI KODI YA ARDHI KWA WAKATI MUEPUKE RIBA - LEO KOMBA

    February 12, 2025
  • WAJUMBE WA BODI, TUMIENI TAALUMA ZENU KUISAIDIA HOSPITALI KUKAMILISHA MIRADI YA UJENZI- RAS CP. HAMDUNI.

    February 11, 2025
  • Angalia zote

Video

MIFUKO BANDIA ZAIDI YA ELFU 20 YAKAMATWA SHINYANGA
Video Nyinginezo

Viunganishi vya Haraka

  • Historia
  • Dira na Dhima
  • Hotuba Mbalimbali
  • Video Mbalimbali
  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Picha za Matukio
  • Miongozo na kanuni

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Mfumo wa kutuma, kupokea na kufuatilia malalamiko, mapendekezo, maulizo na pongezi
  • Ofisi ya Rais Menejimenti ya utumishi wa Umma
  • Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Boma Street, Mwanza Road

    Anuani: P.O.Box 320, Shinyanga

    Simu: +255 28 2762222

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras@shinyanga.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2018. Mkoa wa Shinyanga. Haki zote zimehifadhiwa