• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
    • eVibali |
Shinyanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Shinyanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Yetu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
      • Afya
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Shinyanga
    • Wilaya ya Kahama
    • Wilaya ya Kishapu
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu
    • Halmashauri ya Mji wa Kahama
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu
    • Halmashauri ya Wilaya ya Msalala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
    • Bandari Kavu
  • Huduma
    • Kutoa Ushauri wa Kitaalam
    • Kutafsiri Sheria na Sera
    • Kuratibu Shughuli za Wadau
    • Ulinzi na Usalama
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Tafiti
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha

TANESCO NA SHUWASA FANYENI KAZI KWA UKARIBU NA OFISI ZA WAKURUGENZI WA HALMASHAURI - RC MACHA.

Posted on: January 9th, 2025

Na. Paul Kasembo, SHY RS.

MKUU wa Mkoa wa Shinyanga Mhe. Anamringi Macha ameiagiza Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Shinyanga (SHUWASA) pamoja na Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) Mkoa wa Shinyanga kufanya kazi kwa kushirikiana na Ofisi za Wakurugenzi wa Halmashauri husika kabla hawajapeleka huduma katika maeneo ya makazi ya wananchi ili kuepukana na migogoro ya ardhi ambayo inaweza kujitokeza.

RC Macha ameyasema haya leo tarehe 9 Januari, 2025 wakati akitoa salamu za mwaka mpya kwenye Kikao Kazi na Watumishi wa Serikali, Mkuu wa Wilaya ya Shinyanga Mhe. Julius Mtatiro (Wakili) na Mhe. Joesph Mkude Mkuu wa Wilaya ya Kishapu na Kaimu Mkuu wa Wilaya ya Kahama, na Wakuu wa Taasisi za Umma zikiwemo TANESCO, TARURA, TANROAD, SHUWASA, RUWASA, KUWASA, KASHWASA, BODI YA PAMBA na NFRA Mkoani wa Shinyanga pamoja na wakuu wa Sehemu na Vitengo.

“Ninawaagiza SHUWASA na TANESCO mkafanye kazi kwa ushirikiano mkubwa pamoja na Ofisi za Wakurugenzi wa Halmashauri husika kabla hamjaanza kupeleka huduma katika maeneo ya makazi ya wananchi ili maeneo hayo myafahamu vizuri na hivyo mtaepuka na kuzuia migogoro ya ardhi isiyokuwa ya lazima ambayo imekuwa ikijitokeza kwa kutofanya kazi kwa pamoja,” amesema RC Macha.

Awali akimkaribisha RC Macha kuzungumza na wajumbe wa kikao ambacho , Katibu Tawala Mkoa wa Shinyanga CP. Salum Hamduni amesema kuwa wametekeleza kikamilifu maelekezo yaliyotolewa kwa kuandaa kikao kazi hiki ambacho kimelenga kuangazia shughuli mbalimbali za maendeleo ikiwemo Elimu, Kilimo, Afya, Utatuzi wa migogoro, Tathmini ya Mbio za Mwenge 2024 na maandalizi ya Mbio za Mwenge zijazo kwa mwaka 2025 nk.

Kwa nyakati tofauti, Mkurugenzi wa SHUWASA Mha. Yusuph Katopola na Kaimu Meneja wa TANESCO Mkoa wa Shinyanga Mha. Antony Tarimo wamekiri kupokea maelekezo, ushauri na mapendekezo ya RC Macha na kwamba kuanzia sasa watafanya kwa karibu na Ofisi za Wakurugenzi kabla ya kuanza mchakato wa kuwafikishia huduma wananchi.


Matangazo

  • No records found
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • KIKAO CHA MAPITIO YA ROBO MWAKA KWA KIPINDI CHA OKT - DES 2024 CHA (PJT MMMAM) CHAFANYIKA MKOANI SHINYANGA.

    February 28, 2025
  • RCC SHINYANGA YARIDHIA MAPENDEKEZO NANE (8) YA MATUMIZI BORA YA ARDHI.

    February 27, 2025
  • KUKAMILISHWA KWA MIRADI YA BARABARA KUTAPUNGUZA KERO KWA WANANCHI – RC MACHA

    February 26, 2025
  • WALIMU, TOENI ELIMU INAYOENDANA NA MABADILIKO YA TEKNOLOJIA -RC MACHA

    February 24, 2025
  • Angalia zote

Video

MIFUKO BANDIA ZAIDI YA ELFU 20 YAKAMATWA SHINYANGA
Video Nyinginezo

Viunganishi vya Haraka

  • Historia
  • Dira na Dhima
  • Hotuba Mbalimbali
  • Video Mbalimbali
  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Picha za Matukio
  • Miongozo na kanuni

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Mfumo wa kutuma, kupokea na kufuatilia malalamiko, mapendekezo, maulizo na pongezi
  • Ofisi ya Rais Menejimenti ya utumishi wa Umma
  • Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Boma Street, Mwanza Road

    Anuani: P.O.Box 320, Shinyanga

    Simu: +255 28 2762222

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras@shinyanga.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2018. Mkoa wa Shinyanga. Haki zote zimehifadhiwa