• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
    • eVibali |
Shinyanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Shinyanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Yetu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
      • Afya
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Shinyanga
    • Wilaya ya Kahama
    • Wilaya ya Kishapu
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu
    • Halmashauri ya Mji wa Kahama
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu
    • Halmashauri ya Wilaya ya Msalala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
    • Bandari Kavu
  • Huduma
    • Kutoa Ushauri wa Kitaalam
    • Kutafsiri Sheria na Sera
    • Kuratibu Shughuli za Wadau
    • Ulinzi na Usalama
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Tafiti
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha

TANGULIZENI UZALENDO MNAPOCHIMBA MADINI - RC MACHA

Posted on: August 19th, 2024

Na. Paul Kasembo, KISHAPU.

Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Mhe. Anamiringi Macha amewataka wafanyakazi na watumishi katika mgodi wa Williamson Diamonds Ltd (WDL) maarufu kama MWADUI kuwa wazalendo na waaminifu katika shughuli zao za uchimbaji na utunzaji wa madini mgodini hapo huku akisisitiza umuhimu wa kuendelea kutoa elimu kwa wachimbaji wadogo na kuwashirikisha ilI nao wanufaike.

RC Macha ameyasema haya tarehe 19 Agosti, 2024 alipofika mgodini hapo akiwa ameongozana na Waziri wa Madini Mhe. Anthony Mavunde (MB) kwa lengo la kuangalia namna ambavyo mgodi unatekeleza majukumu yake, kusikiliza changamoto zao na kuona namna ya kuzishughulikia ili lengo la mgodi na Serikali liweze kufikiwa.

"Pamoja na kuwapongeza kwa kazi hii nzuri na yenye tija mnayoifanya, niwaombe watumishi wote katika mgodi huu kutanguliza uzalendo katika utekelezaji wa majukumu yenu ili kazi hii iwe na tija zaidi na kufikiwa kwa lengo la kuongeza pato la Serikali na pia muendelee kutoa elimu kwa wachimbaji wadogo na muwashirikishe zaidi ili na wao wanufaike,“ amesema RC Macha.

Akitoa taarifa ya uzalishaji, Meneja Mgodi wa Almasi wa Mwadui ndg. Ayoub Mwenda amesema kuwa uzalishaji kwa sasa umeongezeka lakini wanakabiliwa na changamoto kadhaa ikiwemo moja kubwa ya kushuka kwa soko la Almasi duniani.

Ayoub amesema, kushuka kwa soko kumesababisha kupata mauzo hafifu ya Almasi licha ya kuwa na uzalishaji  mkubwa jambo linalopelekea kupunguza matumizi ambayo siyo ya lazima ikiwa ni pamoja na kupunguza watoa huduma ndani ya mgodi.

Kwa upande wake Mhe. Mavunde amesema kuwa, changamoto ya kushuka kwa soko la madini ya Almasi ni ya dunia nzima na siyo Mwadui pekee, hivyo Serikali itaendelea kushirikiana na Mgodi wa Almasi Mwadui kutatua changamoto hiyo ili kurudisha heshima na hadhi ya madini ya Almasi.

"Changamoto hii ya kushuka kwa soko la madini ya Almasi zipo sababu kuu 4,moja ikiwa ni kuwapo kwa uzalishaji wa madini ya Almasi za Maabara ambazo bei zake ni za chini," amesema Mavunde.

Aidha Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini Mheshimiwa Masache Kasaka amewakumbusha viongozi wa Mgodi wa WDL kutekeleza maelekezo yaliyotolewa na Kamati kwa wakati kama yalivyoelekezwa.




Matangazo

  • No records found
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • KIKAO CHA MAPITIO YA ROBO MWAKA KWA KIPINDI CHA OKT - DES 2024 CHA (PJT MMMAM) CHAFANYIKA MKOANI SHINYANGA.

    February 28, 2025
  • RCC SHINYANGA YARIDHIA MAPENDEKEZO NANE (8) YA MATUMIZI BORA YA ARDHI.

    February 27, 2025
  • KUKAMILISHWA KWA MIRADI YA BARABARA KUTAPUNGUZA KERO KWA WANANCHI – RC MACHA

    February 26, 2025
  • WALIMU, TOENI ELIMU INAYOENDANA NA MABADILIKO YA TEKNOLOJIA -RC MACHA

    February 24, 2025
  • Angalia zote

Video

MIFUKO BANDIA ZAIDI YA ELFU 20 YAKAMATWA SHINYANGA
Video Nyinginezo

Viunganishi vya Haraka

  • Historia
  • Dira na Dhima
  • Hotuba Mbalimbali
  • Video Mbalimbali
  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Picha za Matukio
  • Miongozo na kanuni

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Mfumo wa kutuma, kupokea na kufuatilia malalamiko, mapendekezo, maulizo na pongezi
  • Ofisi ya Rais Menejimenti ya utumishi wa Umma
  • Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Boma Street, Mwanza Road

    Anuani: P.O.Box 320, Shinyanga

    Simu: +255 28 2762222

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras@shinyanga.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2018. Mkoa wa Shinyanga. Haki zote zimehifadhiwa