• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
    • eVibali |
Shinyanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Shinyanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Yetu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
      • Afya
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Shinyanga
    • Wilaya ya Kahama
    • Wilaya ya Kishapu
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu
    • Halmashauri ya Mji wa Kahama
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu
    • Halmashauri ya Wilaya ya Msalala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
    • Bandari Kavu
  • Huduma
    • Kutoa Ushauri wa Kitaalam
    • Kutafsiri Sheria na Sera
    • Kuratibu Shughuli za Wadau
    • Ulinzi na Usalama
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Tafiti
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha

TANROADS SHINYANGA YAFANYA MALIPO YA MAPUNJO

Posted on: April 30th, 2024

Na. Paul Kasembo, SHY RS.

MENEJA TANROADS Mkoa wa Shinyanga Mhandisi Joel Mwambungu ameongoza timu ya wataalam kufanya malipo ya mapunjo wa fidia kwa wananchi wa eneo la Ibadakuli waliopisha utekelezaji wa mradi wa ujenzi wa Uwanja wa Ndege Shinyanga huku akiwaomba kuendelea kuwa wazalendo wa kulinda mali na uwanja huu wa ndege ambao kimsingi ni mali yao.

Malipo haya kwa wananchi yaliyofanyika kwa njia ya Hundi yamefanyika katika Ofisi ya Kata ya Ibadakuli hapa Manispaa ya Shinyanga huku yakishuhudiwa na viongozi mbalimbali akiwemo Eng. Eugene Soka aliyemuwakilisha Katibu Tawala Mkoa wa Shinyanga Prof. Siza Tumbo, Kamishna Msaidizi wa Ardhi Mkoa wa Shinyanga Ndg. Leo Komber, uongozi wa Serikali ya Tarafa, Kata na Mtaa huku wananchi wakionesha furaha zaidi kuwa na hatma ya jambo lililochukua muda kiasi katika uhitimishaji ambalo leo limefikia mwisho wake.

"Ndugu zangu wananchi wa Ibadakuli, kwa dhati kabisa na kwa niaba ya Mtendaji Mkuu wa TANROADS Mhandisi Mohamed Besta ninamshukuru sana Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuwezesha malipo haya ya mapunjo ya fidia kwenu ili kupisha ujenzi wa uwanja wa ndege Shinyanga ambao kimsingi ni maendeleo na mali yenu wananchi," amesema Mha. Joel.

"Pamoja na shukrani kwenu kwa uvumilivu wenu mkubwa wakati mkisubiria malipo haya ya mapunjo, niwaombe muendelee kuwa walinzi wa miundombinu yote ya uwanja huu wa ndege na mali zote kwakuwa vyote hivi ni mali yenu hivyo ni wajibu wetu sote kuwa sehemu ya umiliki na ulinzi," amesisitiza Mha. Joel.

Kwa upande wake Diwani wa Kata ya Ibadakuli Mhe.Msabila Malale amemshukuru sana Mwenyezi Mungu kwa kuwezesha uhai mpaka kufikia leo, amemshukuru pia Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuwezesha kufikia mwisho wa kero kubwa ya wananchi wa Ibadakuli huku akiwapongeza TANROADS Mkoa wa Shinyanga kwa utekelezaji wa tukio hili kwa wananchi wake huku akiwasihi kwenda kutumia fedha hizo katika kujiletea maendeleo yao.


HABARI PICHA





Matangazo

  • No records found
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • KIKAO CHA MAPITIO YA ROBO MWAKA KWA KIPINDI CHA OKT - DES 2024 CHA (PJT MMMAM) CHAFANYIKA MKOANI SHINYANGA.

    February 28, 2025
  • RCC SHINYANGA YARIDHIA MAPENDEKEZO NANE (8) YA MATUMIZI BORA YA ARDHI.

    February 27, 2025
  • KUKAMILISHWA KWA MIRADI YA BARABARA KUTAPUNGUZA KERO KWA WANANCHI – RC MACHA

    February 26, 2025
  • WALIMU, TOENI ELIMU INAYOENDANA NA MABADILIKO YA TEKNOLOJIA -RC MACHA

    February 24, 2025
  • Angalia zote

Video

MIFUKO BANDIA ZAIDI YA ELFU 20 YAKAMATWA SHINYANGA
Video Nyinginezo

Viunganishi vya Haraka

  • Historia
  • Dira na Dhima
  • Hotuba Mbalimbali
  • Video Mbalimbali
  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Picha za Matukio
  • Miongozo na kanuni

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Mfumo wa kutuma, kupokea na kufuatilia malalamiko, mapendekezo, maulizo na pongezi
  • Ofisi ya Rais Menejimenti ya utumishi wa Umma
  • Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Boma Street, Mwanza Road

    Anuani: P.O.Box 320, Shinyanga

    Simu: +255 28 2762222

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras@shinyanga.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2018. Mkoa wa Shinyanga. Haki zote zimehifadhiwa