• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
    • eVibali |
Shinyanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Shinyanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Yetu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
      • Afya
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Shinyanga
    • Wilaya ya Kahama
    • Wilaya ya Kishapu
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu
    • Halmashauri ya Mji wa Kahama
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu
    • Halmashauri ya Wilaya ya Msalala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
    • Bandari Kavu
  • Huduma
    • Kutoa Ushauri wa Kitaalam
    • Kutafsiri Sheria na Sera
    • Kuratibu Shughuli za Wadau
    • Ulinzi na Usalama
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Tafiti
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha

TCRA yatoa Elimu ya kuhamia mtandao mwingine bila kubadili namba yako

Posted on: September 27th, 2017

Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA)imetoa elimu kwa waandishi wa Habari wa Mkoa wa Shinyanga kuhusu huduma ya kuhama mtandao pasipo kubadili namba ya simu.

Elimu hiyo imetolewa mapema leo katika Ukumbi wa Mikutano wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga kwa lengo la kuwafikia wananchi na wadau wa mawasiliano kupitia vyombo mbalimbali vya habari. 

Mhandisi Mwesigwa Felician ambaye ni Mhandisi Mwandamizi wa huduma za mawasiliano wa TCRA amesema kuwa, huduma hiyo ni ya hiyari ambayo inamuwezesha mtumiaji wa simu kuhama kutoka mtandao anaoutumia na kuamua kutumia mtandao mwingine kwa namba ileile moja bila usumbufu wowote kwa ndugu, jamaa na marafiki.

Bw. Mwesigwa amesema faida kubwa ya huduma hii ni pamoja na mteja kuchagua mtoa huduma ambaye anaona anatoa huduma bora zaidi kwa wateja na anayekidhi matarajio ya mteja.

Aidha, huduma hii inachangia kuongeza ushindani kati ya watoa huduma za mawasiliano hivyo kuwa kichocheo cha utoaji huduma bora na zenye gharama nafuu kwani wateja watahama kufuata huduma bora.

Naibu Mkurugenzi wa masuala ya watumiaji wa huduma na bidhaa za mawasiliano wa TCRA Bw. Thadayo Ringo amesema kuwa huduma hiyo ni bure na mwananchi anaweza kuhama wakati wowote anaohitaji kwa kutembelea vituo vya mauzo au mawakala akiwa na kitambulisho chenye picha yake pamoja na simu ya kiganjani yenye namba anayotaka kuhamia.

Bw. Ringo amesisitiza wananchi kuwa makini kwenye matumizi ya simu ikiwemo matumizi ya miamala ya fedha kwa kuhakikisha makosa ya uzembe hayajitokezi hivyo kuepuka usumbufu wa kutorudishiwa fedha zao.

Amewataka wananchi kutoa taarifa au malalamiko wakati wowote wanapojikuta wanapata usumbufu katika matumizi ya simu au huduma za mawasiliano.

Matangazo

  • No records found
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • KIKAO CHA MAPITIO YA ROBO MWAKA KWA KIPINDI CHA OKT - DES 2024 CHA (PJT MMMAM) CHAFANYIKA MKOANI SHINYANGA.

    February 28, 2025
  • RCC SHINYANGA YARIDHIA MAPENDEKEZO NANE (8) YA MATUMIZI BORA YA ARDHI.

    February 27, 2025
  • KUKAMILISHWA KWA MIRADI YA BARABARA KUTAPUNGUZA KERO KWA WANANCHI – RC MACHA

    February 26, 2025
  • WALIMU, TOENI ELIMU INAYOENDANA NA MABADILIKO YA TEKNOLOJIA -RC MACHA

    February 24, 2025
  • Angalia zote

Video

MIFUKO BANDIA ZAIDI YA ELFU 20 YAKAMATWA SHINYANGA
Video Nyinginezo

Viunganishi vya Haraka

  • Historia
  • Dira na Dhima
  • Hotuba Mbalimbali
  • Video Mbalimbali
  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Picha za Matukio
  • Miongozo na kanuni

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Mfumo wa kutuma, kupokea na kufuatilia malalamiko, mapendekezo, maulizo na pongezi
  • Ofisi ya Rais Menejimenti ya utumishi wa Umma
  • Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Boma Street, Mwanza Road

    Anuani: P.O.Box 320, Shinyanga

    Simu: +255 28 2762222

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras@shinyanga.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2018. Mkoa wa Shinyanga. Haki zote zimehifadhiwa