• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
    • eVibali |
Shinyanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Shinyanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Yetu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
      • Afya
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Shinyanga
    • Wilaya ya Kahama
    • Wilaya ya Kishapu
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu
    • Halmashauri ya Mji wa Kahama
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu
    • Halmashauri ya Wilaya ya Msalala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
    • Bandari Kavu
  • Huduma
    • Kutoa Ushauri wa Kitaalam
    • Kutafsiri Sheria na Sera
    • Kuratibu Shughuli za Wadau
    • Ulinzi na Usalama
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Tafiti
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha

TEKELEZENI KWA VITENDO FALSAFA YA 4RYA RAIS DDKT. SAMIA - MAJALIWA

Posted on: September 6th, 2024

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa amewataka Maafisa waandamizi wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi na viongozi wa vyombo vya usalama wa Wizara hiyo kutekeleza kwa vitendo na kuiishi falsafa ya R nne (4R) ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ili kufikia malengo yaliyokusudiwa.

 Amesema kuwa ni muhimu kuifahamu vyema falsafa hiyo ya Rais Dkt. Samia na kuitekeleza kwa vitendo. “Nina imani kubwa kwamba uongozi wa juu wa Wizara umeielewa vizuri falsafa hiyo, na semina hii elekezi ni ushahidi tosha wa kuitekeleza kwa vitendo”

 Amesema hayo leo (Ijumaa, Septemba 06, 2024) wakati alipofungua Semina elekezi kwa viongozi waandamizi wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi iliyofanyika kwenye ukumbi wa mikutano wa Hoteli ya Weruweru River Lodge, mkoani Kilimanjaro.

 “Falsafa hii inajikita katika masuala ya Maridhiano (Reconciliation), Ustahamilivu (Resilience), Mageuzi (Reforms), na Kujenga upya Taifa (Rebuilding). Hivyo, nitoe wito kwa washiriki ambao ni Maafisa Waandamizi wa Vyombo vya Ulinzi na Usalama chini ya Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi pamoja na Menejimenti ya Wizara na Taasisi zake kuendelea kushiriki na kuishi kikamilifu falsafa hii”

 Ameongeza kuwa semina elekezi hiyo ni sehemu muhimu kwa maendeleo ya kitaaluma na kitaasisi kwa maafisa waandamizi wa vyombo vya usalama, na husaidia katika kuhakikisha wanatekeleza majukumu yao kwa ufanisi na kwa kufuata viwango vya kitaaluma na kisheria. 

 “Semina elekezi hutoa fursa kwa maafisa waandamizi kujifunza mbinu na taratibu mpya katika utendaji wa majukumu yao. Hii inajumuisha teknolojia mpya, mbinu bora za ulinzi na usalama, na mbinu za kisasa za kupambana na uhalifu.”

 Kwa Upande wake Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni amemshukuru Rais Dkt. Samia juu ya nia yake ya dhati kwa kufanya maboresho ya Wizara hiyo na vyombo vyake ikiwemo Jeshi la Polisi, Magereza, Uhamiaji na Zimamoto pamoja na Taasisi ya NIDA. 

 “Maboresho haya yanahusisha upandishaji vyeo wa kihistoria wa Maafisa, Wakaguzi na Askari wapatao 50,971, kuongeza Bajeti ya Miradi ya Maendeleo kutoka mwaka 2021/22 hadi 2024/25 ni Shilingi 262.2 ambayo ni sawa na asilimia 954.59 ya ongezeko la Bajeti ya Miradi ya Maendeleo”

 Amesema kuwa Ongezeko hilo la bajeti limesaidia kwa kiasi kikubwa kupatikana kwa vitendea kazi ikiwemo magari, mitambo, boti, vifaa vya TEHAMA na kadhalika.

Matangazo

  • No records found
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • KIKAO CHA MAPITIO YA ROBO MWAKA KWA KIPINDI CHA OKT - DES 2024 CHA (PJT MMMAM) CHAFANYIKA MKOANI SHINYANGA.

    February 28, 2025
  • RCC SHINYANGA YARIDHIA MAPENDEKEZO NANE (8) YA MATUMIZI BORA YA ARDHI.

    February 27, 2025
  • KUKAMILISHWA KWA MIRADI YA BARABARA KUTAPUNGUZA KERO KWA WANANCHI – RC MACHA

    February 26, 2025
  • WALIMU, TOENI ELIMU INAYOENDANA NA MABADILIKO YA TEKNOLOJIA -RC MACHA

    February 24, 2025
  • Angalia zote

Video

MIFUKO BANDIA ZAIDI YA ELFU 20 YAKAMATWA SHINYANGA
Video Nyinginezo

Viunganishi vya Haraka

  • Historia
  • Dira na Dhima
  • Hotuba Mbalimbali
  • Video Mbalimbali
  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Picha za Matukio
  • Miongozo na kanuni

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Mfumo wa kutuma, kupokea na kufuatilia malalamiko, mapendekezo, maulizo na pongezi
  • Ofisi ya Rais Menejimenti ya utumishi wa Umma
  • Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Boma Street, Mwanza Road

    Anuani: P.O.Box 320, Shinyanga

    Simu: +255 28 2762222

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras@shinyanga.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2018. Mkoa wa Shinyanga. Haki zote zimehifadhiwa