• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
    • eVibali |
Shinyanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Shinyanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Yetu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
      • Afya
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Shinyanga
    • Wilaya ya Kahama
    • Wilaya ya Kishapu
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu
    • Halmashauri ya Mji wa Kahama
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu
    • Halmashauri ya Wilaya ya Msalala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
    • Bandari Kavu
  • Huduma
    • Kutoa Ushauri wa Kitaalam
    • Kutafsiri Sheria na Sera
    • Kuratibu Shughuli za Wadau
    • Ulinzi na Usalama
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Tafiti
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha

TJMEANZA KUFANYIA KAZI MAELEKEZO YA MHE. WAZIRI MKUU - PROF. MBARAWA.

Posted on: February 20th, 2025

Na. Paul Kasembo, SHY MC,

WAZIRI wa Uchukuzi nchini Prof. Makame Mbarawa amesema kuwa Wizara ya Uchukuzi kwa kushirikiana na wataalamu tayari wameanza kufanyia kazi maelekezo ya Waziri Mkuu wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa ambaye aliagiza kufungwa taa kwenye uwanja wa ndege wa Ibadakuli mkoani Shinyanga na mpaka sasa tayari wameagiza vifaa ili kuhakikisha maagizo hayo yanatekelezwa ipasavyo ili uwanja huu ufanye kazi masaa 24 huku wakisubiria jengo la abiria kukamilika ambalo kwa sasa limefikia asilimia 50.

Prof. Mbarawa ameyasema haya Februari 20, 2025 wakati akikagua ujenzi wa jengo la abiria lililopo uwanja wa ndege wa Shinyanga ambapo ameongeza kuwa huu ni utekelezaji wa maagizo ya  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ambaye alitoa maelekezo mahususi kwamba uwanja huu wa ndege wa Ibadakuli pamoja na viwanja vingine vikarabatiwe na kuanza kutumika tena kama ilvyokuwa awali, hivyo anaamini kuwa uwanja huu utakamilika na kuanza kutumika kwa muda uliopangwa.

“Wizara ya Uchukuzi kwa kushirikiana na wataalam mbalimbali tayari tumeanza kufanyia kazi maelekezo ya Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa ambaye aliagiza uwanja huu uwekewe taa na uanze kufanya kazi kwa masaa 24, hivyo mpaka sasa tayari tumeagiza vifaa ambayo vitatumika ili kuhakikisha uwanja huu unakamilika na kuanza kufanya kazi tena kama ilivyokuwa awali,” amesema Prof. Mbarawa.

Kwa upande wake, Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Mhe. Anamringi Macha amemshukuru sana Waziri wa Uchukuzi kwa kutembelea ili kufahamu maendeleo ya ukarabati mkubwa wa uwanja huu lakini pia ameshukuru kwa jitihada zilizofanyika ili kuboresha uwanja licha ya kwamba changamoto mbalimbali zilizojitokeza na kupelekea kucheleweshwa kwa ukarabati.

Kukamilika kwa uwanja wa ndege wa Ibadakuli mkoani Shinyanga kutafungua fursa za kiuchumi kwa wakazi wa Shinyanga na maeneo ya jirani ikiwemo Simiyu, Geita na viunga vyake na hivyo kurahisisha usafiri wa watu na mizigo ambapo awali walikuwa wanasafiri Kilometa zaidi ya 164 kwenda Mwanza kupanda ndege.


Matangazo

  • No records found
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • RC MHITA AWAHAMASISHA WAFANYABIASHARA NA WAWEKEZAJI KUCHANGAMKIA FURSA ZA KIUCHUMI MKOANI SHINYANGA

    November 13, 2025
  • RC MHITA AKUTANA NA MSANII BANDO MC, APONGEZA JUHUDI ZA KUSAIDIA VIJANA SHINYANGA

    November 11, 2025
  • RC MHITA APONGEZA UONGOZI MPYA WA KANISA LA WASABATO NGBF MKOANI SHINYANGA.

    November 07, 2025
  • WANAFUNZI 29,193 KUFANYA MTIHANI WA UPIMAJI KIDATO CHA PILI SHINYANGA.

    November 07, 2025
  • Angalia zote

Video

RC MHITA AWAHAMASISHA WAFANYABIASHARA NA WAWEKEZAJI KUCHANGAMKIA FURSA ZA KIUCHUMI MKOANI SHINYANGA
Video Nyinginezo

Viunganishi vya Haraka

  • Historia
  • Dira na Dhima
  • Hotuba Mbalimbali
  • Video Mbalimbali
  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Picha za Matukio
  • Miongozo na kanuni

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Mfumo wa kutuma, kupokea na kufuatilia malalamiko, mapendekezo, maulizo na pongezi
  • Ofisi ya Rais Menejimenti ya utumishi wa Umma
  • Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    OFISI YA MKUU WA MKOA, MKOA WA SHINYANGA, 04 MTAA WA BOMA

    Anuani: P.O.Box 320, 37180,SHINYANGA, TANZANIA

    Simu: +255 28 2762222

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras@shinyanga.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2018. Mkoa wa Shinyanga. Haki zote zimehifadhiwa