• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
    • eVibali |
Shinyanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Shinyanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Yetu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
      • Afya
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Shinyanga
    • Wilaya ya Kahama
    • Wilaya ya Kishapu
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu
    • Halmashauri ya Mji wa Kahama
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu
    • Halmashauri ya Wilaya ya Msalala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
    • Bandari Kavu
  • Huduma
    • Kutoa Ushauri wa Kitaalam
    • Kutafsiri Sheria na Sera
    • Kuratibu Shughuli za Wadau
    • Ulinzi na Usalama
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Tafiti
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha

TRA MSIFUNGE BIASHARA KWA CHANGAMOTO ZINAZOTATULIKA – RC MBONI MHITA

Posted on: September 10th, 2025

Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, Mhe. Mboni Mhita, ametoa wito kwa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) Mkoa wa Shinyanga kuhakikisha inatatua changamoto za wafanyabiashara kwa njia ya mazungumzo badala ya kufunga biashara, hasa pale ambapo matatizo hayo yanaweza kutatuliwa bila kuvunja sheria.

Mhe. Mhita aliyasema hayo leo, Septemba 10, 2025, wakati wa uzinduzi rasmi wa Dawati Maalum la Uwezeshaji Biashara kwa Mkoa wa Shinyanga, uliofanyika katika viwanja vya Ofisi za TRA.

Katika hotuba yake, alisisitiza kuwa Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan imejikita katika mazingira wezeshi ya biashara na uwekezaji, hivyo ni muhimu kwa taasisi za mapato kutekeleza wajibu wake kwa kutoa elimu na kushirikiana na wafanyabiashara badala ya kutumia nguvu ya kufunga.

“Wafanyabiashara ni washirika wetu katika maendeleo. Kama kuna dosari, tusitafute njia rahisi ya kufunga biashara bali tuwasaidie kurekebisha na kuelewa wajibu wao. Changamoto zinazotatulika zisigeuzwe kuwa adhabu,” alisema Mhe. Mhita.

Awali, Meneja wa TRA Mkoa wa Shinyanga, Bw. Emmanuel Maro, alieleza kuwa kuanzishwa kwa dawati hilo ni hatua muhimu ya kuimarisha mahusiano ya karibu na wafanyabiashara kwa kuwapa elimu ya kodi, kuwalea katika biashara zao na kuwasaidia kufikia ndoto zao bila vikwazo visivyokuwa vya lazima.

“Dawati hili litatumika kama daraja la mawasiliano kati ya TRA na wafanyabiashara, kuwasaidia kwa njia ya kitaalamu ili waongeze tija na kuchangia kikamilifu pato la taifa,” alisema Maro.

Matangazo

  • No records found
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • TRA MSIFUNGE BIASHARA KWA CHANGAMOTO ZINAZOTATULIKA – RC MBONI MHITA

    September 10, 2025
  • KAMISHNA WA URAIA NA PASPOTI AMTEMBELEA MKUU WA MKOA WA SHINYANGA, AZUNGUMZIA MABORESHO YA HUDUMA ZA UHAMIAJI

    September 10, 2025
  • SHINYANGA: VITUO VYA AFYA 331 KUSAJILIWA KWENYE MFUMO WA MAMLAKA YA USIMAMIZI WA BIMA (TIRA)

    September 09, 2025
  • WATAHINIWA 41,463 KUFANYA MTIHANI WA DARASA LA SABA SHINYANGA

    September 09, 2025
  • Angalia zote

Video

RC MHITA AZINDUA DAWATI MAALUM LA UWEZESHAJI BIASHARA TRA SHINYANGA
Video Nyinginezo

Viunganishi vya Haraka

  • Historia
  • Dira na Dhima
  • Hotuba Mbalimbali
  • Video Mbalimbali
  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Picha za Matukio
  • Miongozo na kanuni

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Mfumo wa kutuma, kupokea na kufuatilia malalamiko, mapendekezo, maulizo na pongezi
  • Ofisi ya Rais Menejimenti ya utumishi wa Umma
  • Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    OFISI YA MKUU WA MKOA, MKOA WA SHINYANGA, 04 MTAA WA BOMA

    Anuani: P.O.Box 37180,SHINYANGA, TANZANIA

    Simu: +255 28 2762222

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras@shinyanga.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2018. Mkoa wa Shinyanga. Haki zote zimehifadhiwa