• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
    • eVibali |
Shinyanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Shinyanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Yetu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
      • Afya
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Shinyanga
    • Wilaya ya Kahama
    • Wilaya ya Kishapu
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu
    • Halmashauri ya Mji wa Kahama
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu
    • Halmashauri ya Wilaya ya Msalala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
    • Bandari Kavu
  • Huduma
    • Kutoa Ushauri wa Kitaalam
    • Kutafsiri Sheria na Sera
    • Kuratibu Shughuli za Wadau
    • Ulinzi na Usalama
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Tafiti
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha

TUENDELEE KULIOMBEA TAIFA, TUDUMISHE AMANI -RC MHITA

Posted on: October 1st, 2025

Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, Mhe. Mboni Mhita  , ametoa wito kwa viongozi wa dini mkoani humo na Nchini kwa ujumla kuendelea kusali na kuliombea Taifa, wananchi na viongozi, ili kudumisha amani, mshikamano na upendo  hususan katika kipindi hiki tunapoelekea Uchaguzi Mkuu wa 2025.  

Mhe. Mhita ametoa wito huo leo, Oktoba 1, 2025, wakati wa Ibada ya Ufunguzi wa Mkutano wa 22 wa Ushirikiano wa Kimisioni ya Kilutheri (22nd LMC Roundtable Meeting) uliofanyika katika Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania – Dayosisi ya Kusini Mashariki ya Ziwa Victoria (KKKT-DKMZV), Shinyanga, ambapo mkutano huo umehudhuriwa na viongozi mbalimbali wa dini, Serikali na washirika wa kimataifa.  

“Nitoe wito kwa viongozi wa dini kuendelea kusali kwa ajili ya taifa letu, viongozi na wananchi ili tuendelee kuwa na amani, umoja, mshikamano na uchaguzi wetu mkuu ufanyike kwa utulivu na upendo,” alisema RC Mhita.

 Aidha, Mhita amewahakikishia washiriki wote wa mkutano huo kuwa Serikali ya Mkoa wa Shinyanga itaendelea kutoa ushirikiano wa karibu na kuhakikisha mazingira ya mkutano ni salama na tulivu wakati wote. Alisisitiza umuhimu wa kutumia mkutano huo kama fursa ya kubadilishana uzoefu, maarifa na maombi kwa ajili ya kulijenga Taifa kiroho na kijamii.  

Hata hivyo RC Mhita ametumia fursa hiyo kuwaomba wananchi wote wa Mkoa wa Shinyanga kujitokeza kwa wingi kupiga kura kwenye Uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika Octoba 29,2025 ambapo amewahakikishia kwamba siku hiyo kutakuwa na utulivu wa kutosha ikiwa ni pamoja na Amani kwa wale wote watakaojitokeza kupiga Kura ya kumchagua Rais, Wabunge na Madiwani.

Kwa upande wake, Mkuu wa Kanisa la KKKT nchini, Dkt. Alex Malasusa, amesema mkutano huu ni jukwaa muhimu la kuendeleza huduma za kiinjili, kijamii na kimaendeleo huku akihimiza waumini kushikamana katika imani, haki na upendo kama njia ya kuleta mabadiliko chanya katika jamii.  

Mkutano wa 22 wa LMC umebeba kaulimbiu ya kuimarisha ushirikiano kati ya KKKT na mashirika ya kimisheni Duniani kwa ajili ya huduma endelevu na maendeleo ya jamii na kanisa.

Matangazo

  • No records found
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • RC MHITA AWAHAMASISHA WAFANYABIASHARA NA WAWEKEZAJI KUCHANGAMKIA FURSA ZA KIUCHUMI MKOANI SHINYANGA

    November 13, 2025
  • RC MHITA AKUTANA NA MSANII BANDO MC, APONGEZA JUHUDI ZA KUSAIDIA VIJANA SHINYANGA

    November 11, 2025
  • RC MHITA APONGEZA UONGOZI MPYA WA KANISA LA WASABATO NGBF MKOANI SHINYANGA.

    November 07, 2025
  • WANAFUNZI 29,193 KUFANYA MTIHANI WA UPIMAJI KIDATO CHA PILI SHINYANGA.

    November 07, 2025
  • Angalia zote

Video

RC MHITA AWAHAMASISHA WAFANYABIASHARA NA WAWEKEZAJI KUCHANGAMKIA FURSA ZA KIUCHUMI MKOANI SHINYANGA
Video Nyinginezo

Viunganishi vya Haraka

  • Historia
  • Dira na Dhima
  • Hotuba Mbalimbali
  • Video Mbalimbali
  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Picha za Matukio
  • Miongozo na kanuni

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Mfumo wa kutuma, kupokea na kufuatilia malalamiko, mapendekezo, maulizo na pongezi
  • Ofisi ya Rais Menejimenti ya utumishi wa Umma
  • Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    OFISI YA MKUU WA MKOA, MKOA WA SHINYANGA, 04 MTAA WA BOMA

    Anuani: P.O.Box 320, 37180,SHINYANGA, TANZANIA

    Simu: +255 28 2762222

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras@shinyanga.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2018. Mkoa wa Shinyanga. Haki zote zimehifadhiwa