• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
    • eVibali |
Shinyanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Shinyanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Yetu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
      • Afya
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Shinyanga
    • Wilaya ya Kahama
    • Wilaya ya Kishapu
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu
    • Halmashauri ya Mji wa Kahama
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu
    • Halmashauri ya Wilaya ya Msalala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
    • Bandari Kavu
  • Huduma
    • Kutoa Ushauri wa Kitaalam
    • Kutafsiri Sheria na Sera
    • Kuratibu Shughuli za Wadau
    • Ulinzi na Usalama
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Tafiti
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha

TUMIENI HATI SAFI MLIYOIPATA KUTEKELEZA YALIYOKUSUDIWA - RC MACHA

Posted on: June 25th, 2024

Na. Paul Kasembo, SHINYANGA DC.

MKUU wa Mkoa wa Shinyanga Mhe. Anamringi Macha ameitaka Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga kuitumia vizuri Hati Safi waliyoipata kutoka kwa Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) kwa ukaguzi wa mwaka 2022/2023 ili kutekeleza yale yote yaliyokuwa yamekusudiwa yakilenga pia Ilani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) huku akisisitiza juhudi zaidi na weledi katika kuzingatia maelekezo ya CAG ili kuendelea kupata hati safi.

RC Macha ameyasema haya leo tarehe 25 Juni, 2024 wakati wa kujadili taarifa ya hoja za CAG kwa mwaka wa fedha kuishia Juni 30, 2023 ambapo pamoja na pongezi zaidi kwa kuendelea kutekeleza miradi ya maendeleo ikiwemo ujenzi wa jengo la Utawala ambalo kwa muda kiasi lilisimama kutokana na uzembe wa mkandarasi aliyekuwepo awali. Baada ya kumuondoa na kuweka mwingine kwa sasa ujenzi unakwenda kasi sana na umefikia hatua ya umaliziaji huku akishauri kuundwa kwa Timu ndogo ya watu (5) ambao watakuwa ni maalum kwa ajili ya kushughulikia na kujibu hoja za CAG peke yake na iwezeshwe kikamilifu kwa ajili ya kazi hii kwa lengo la kuondoa kabisa hoja zinazojitokeza

"Pamoja na kuwapongeza kwa kufanya vizuri aana na hata mkapata hati safi ya CAG, lakini nendeni mkatumie hati hiyo safi mliyoipata kutekeleza yale yote mliyoyakusudia ikiwemo kutekeleza Ilani ya CCM ambayo ndiyo inaunda Serikali yetu na ndiyo ambayo ninyi imewaajiri, hivyo zingatieni haya na mkafikie lengo mlilokusudia na siyo vinginevyo, " amesema RC Macha.

Awali akiwasilisha taarifa ya utekelezaji wa CAG ndg. Thobias Shija ambaye ni Mkuu wa Kitengo cha Fedha kwa niaba ya Mkurugenzi wa Halmashauri ya Shinyanga Dkt. Kalekwa Kasanga amesema kuwa Halmashauri ilikuwa na hoja 35 za mwaka 2022/2023 na hoja za nyuma ni 69 jumla ya hoja 104 ikijumlisha na hoja za nyuma, ambapo 41 zimejibiwa na kufungwa, 47 zinaendelea na utekelezwaji, zilizofutwa ni 15 na majibu ambayo hayajakubalika ni 1.

Mwisho Makamu Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga Mhe. Nicodemus Simoni alisema kuwa, yale yote yaliyoelekezwa wameyapokea na watayatekeleza.


HABARI PICHA



Matangazo

  • No records found
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • KIKAO CHA MAPITIO YA ROBO MWAKA KWA KIPINDI CHA OKT - DES 2024 CHA (PJT MMMAM) CHAFANYIKA MKOANI SHINYANGA.

    February 28, 2025
  • RCC SHINYANGA YARIDHIA MAPENDEKEZO NANE (8) YA MATUMIZI BORA YA ARDHI.

    February 27, 2025
  • KUKAMILISHWA KWA MIRADI YA BARABARA KUTAPUNGUZA KERO KWA WANANCHI – RC MACHA

    February 26, 2025
  • WALIMU, TOENI ELIMU INAYOENDANA NA MABADILIKO YA TEKNOLOJIA -RC MACHA

    February 24, 2025
  • Angalia zote

Video

MIFUKO BANDIA ZAIDI YA ELFU 20 YAKAMATWA SHINYANGA
Video Nyinginezo

Viunganishi vya Haraka

  • Historia
  • Dira na Dhima
  • Hotuba Mbalimbali
  • Video Mbalimbali
  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Picha za Matukio
  • Miongozo na kanuni

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Mfumo wa kutuma, kupokea na kufuatilia malalamiko, mapendekezo, maulizo na pongezi
  • Ofisi ya Rais Menejimenti ya utumishi wa Umma
  • Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Boma Street, Mwanza Road

    Anuani: P.O.Box 320, Shinyanga

    Simu: +255 28 2762222

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras@shinyanga.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2018. Mkoa wa Shinyanga. Haki zote zimehifadhiwa