• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
    • eVibali |
Shinyanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Shinyanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Yetu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
      • Afya
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Shinyanga
    • Wilaya ya Kahama
    • Wilaya ya Kishapu
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu
    • Halmashauri ya Mji wa Kahama
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu
    • Halmashauri ya Wilaya ya Msalala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
    • Bandari Kavu
  • Huduma
    • Kutoa Ushauri wa Kitaalam
    • Kutafsiri Sheria na Sera
    • Kuratibu Shughuli za Wadau
    • Ulinzi na Usalama
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Tafiti
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha

USAID KUWANUFAISHA WATOTO NA VIJANA WA MIKOA 9 WENYE CHINI YA UMRI WA MIAKA 17

Posted on: June 29th, 2024

Na. Paul Kasembo, SHY RS.

Wakala wa Kimarekani kwa Misaada ya Kimaendeleo ya Kimataifa (USAID) inafadhiri msaada ambao utaanza kuwanufaisha watoto na vijana chini ya umri wa Miaka 17 ambao wataendelea kunufaika na mradi wa “USAID Kizazi Hodari” unaotekelezwa na Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) katika Mikoa tisa (9) na Halmashauri 41 nchini.

Hayo yamebainishwa na Mkurugenzi Mshiriki anayesimamia matokeo na asasi zinazotekeleza mradi wa “USAID Kizazi Hodari”  Kanda ya Kaskazini Mashariki ndg. Aminiel Mongi kwenye  kikao cha tathmini ya utekelezaji wa mradi huo Juni 27, 2024 mkoani Shinyanga ambapo pamoja na mambo mengine umelenga kuboresha afya, ustawi na ulinzi wa watoto walio katika mazingira hatarishi pamoja na vijana chini ya Miaka 18 ili kutokomeza maambukizi mapya ya virusi vya UKIMWI.

"Lengo kuu la mradi huu ni kuboresha Afya, ustawi na ulinzi wa watoto waliokatika mazingira hatarishi na vijana kuanzia umri wa Miaka 0 hadi 17 ili kufikia malengo ya kidunia ya kupambana na virusi vya UKIMWI kwa maana wale wenye maambukizi waweze kujua hali zao za maambukizi lakini pia wale ambao wamefahamu hali zao za maambukizi waweze kuunganishwa na vituo vya tiba na mafunzo kwa ajili ya kuanzishiwa dawa, lakini pia wale ambao wameanzishiwa dawa kufika kwenye vituo ili kufubaza maambukizi ya virusi vya UKIMWI”. amesema Mongi

Akizungumza mchumi mkuu idara ya Afya, lishe na ustawi wa jamii kutoka ofisi ya Rais TAMISEMI, ndg. Rashid Kitambulio amesema serikali itaendelea kushirikiana na Kanisa la KKKT katika kufikia malengo yaliyokusudiwa huku akishukuru kwa mradi huo wa USAID kizazi hodari ambao unaendelea kuwanufaisha wahanga hasa wa maambukizi ya virusi vya UKIMWI.

KKKT na mradi wa ‘USAID Kizazi Hodari’ wameitisha mkutano wa wadau wanaoshiriki katika utekelezaji wa mradi huo wakiwemo wawakilishi kutoka Ofisi ya Rais TAMISEMI, Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia Wanawake na Makundi Maalum, TACAIDS, Kamati ya Usimamizi wa Afya ngazi ya Mikoa na Halmashauri, wadau wanaosimamia afua za tiba na mafunzo katika Mikoa husika lengo ni kupitia na kutathimini utekelezaji wa shughuli za mradi na kuweka mipango endelevu ya mradi huo.

USAID Tanzania kwa ujumla wake inaangazia rasilimali watu kwa afya, mifumo ya taarifa za afya na utumiaji wa data, utawala bora, ufadhili wa afya, ugavi unaotegemewa na sikivu, na ushirikishwaji wa sekta binafsi. Mradi huu unaofadhiliwa na USAID ambao ndio wafadhili wakuu wa mradi huu na mradi unatekelezwa na makao makuu ya Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) unatekelezwa katika Mikoa tisa (9) ya Tanga, Kilimanjaro, Arusha, Manyara, Singida, Dodoma, Mwanza, Geita na Mara pamoja na jumla ya Halmashauri 41.


HABARI PICHA

Matangazo

  • No records found
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • WANUFAIKA WA MIKOPO YA 10% LIPENI KWA WAKATI ILI PIA VIKOPESHWE NA VIKUNDI VINGINE - RC MACHA

    February 13, 2025
  • CP. HAMDUNI AKUTANA NA KAMATI YA MICHEZO YA JWTZ

    February 13, 2025
  • WANANCHI, LIPENI KODI YA ARDHI KWA WAKATI MUEPUKE RIBA - LEO KOMBA

    February 12, 2025
  • WAJUMBE WA BODI, TUMIENI TAALUMA ZENU KUISAIDIA HOSPITALI KUKAMILISHA MIRADI YA UJENZI- RAS CP. HAMDUNI.

    February 11, 2025
  • Angalia zote

Video

MIFUKO BANDIA ZAIDI YA ELFU 20 YAKAMATWA SHINYANGA
Video Nyinginezo

Viunganishi vya Haraka

  • Historia
  • Dira na Dhima
  • Hotuba Mbalimbali
  • Video Mbalimbali
  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Picha za Matukio
  • Miongozo na kanuni

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Mfumo wa kutuma, kupokea na kufuatilia malalamiko, mapendekezo, maulizo na pongezi
  • Ofisi ya Rais Menejimenti ya utumishi wa Umma
  • Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Boma Street, Mwanza Road

    Anuani: P.O.Box 320, Shinyanga

    Simu: +255 28 2762222

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras@shinyanga.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2018. Mkoa wa Shinyanga. Haki zote zimehifadhiwa