• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
    • eVibali |
Shinyanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Shinyanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Yetu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
      • Afya
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Shinyanga
    • Wilaya ya Kahama
    • Wilaya ya Kishapu
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu
    • Halmashauri ya Mji wa Kahama
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu
    • Halmashauri ya Wilaya ya Msalala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
    • Bandari Kavu
  • Huduma
    • Kutoa Ushauri wa Kitaalam
    • Kutafsiri Sheria na Sera
    • Kuratibu Shughuli za Wadau
    • Ulinzi na Usalama
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Tafiti
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha

Uzinduzi wa maadhimisho ya Upandaji Miti wafana Kishapu

Posted on: April 3rd, 2018

Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Mhe. Zainab Telack amezindua wiki ya maadhimisho ya upandaji miti kwa kupanda miti zaidi ya 1000 katika kijiji cha Mwatuju, Wilaya ya Kishapu Mkoani Shinyanga.

Akizungumza na wananchi katika uzinduzi wa maadhimisho hayo uliyofanyika leo, Mhe. Telack amewataka wananchi kuacha kusubiri mkono wa sheria uwaangukie isipokuwa kila mmoja atekeleze majukumu yake katika kupanda miti na kuitunza ili kuepuka na tatizo la jangwa linalonyemelea Mikoa ya kanda ya Magharibi kwa kasi

Telack amewataka wadau wa mazingira wajikite katika Mkoa wa Shinyanga kwani bado kazi ni kubwa kuhakikisha Mkoa unatoka katika hali ya Jangwa.

“Shinyanga siyo Jangwa, Jangwa tumelitafuta wenyewe. Kuirudisha Shinyanga katika hali yake na kuwa na misitu inawezekana” amesema Mhe. Telack.

Naye Mkuu wa Mkoa wa Tabora Mhe. Aggrey Mwanri ambaye ameambatana na Mhe. Telack katika uzinduzi huo, amesema wananchi wakipata elimu na kufuata sheria na taratibu zilizowekwa za kuhifadhi mazingira, miti inayopandwa itaota na kuwasaidia katika ustawi wao ikiwemo kupata mvua za kutosha.

Maadhimisho haya ambayo yanafanyika kila mwaka tarehe 3 – 5 Aprili, mwaka huu yanafanyika kitaifa Mkoani Shinyanga, katika Wilaya ya Kishapu.

Kupitia maadhimisho haya, Mkoa utapanda zaidi ya miti 200,000 katika Mamlaka zote za Serikali za Mitaa.

Kilele cha maadhimisho ya upandaji miti kitaifa ni tarehe 5 Aprili, 2018 ambapo mgeni rasmi atakuwa ni Waziri wa Maliasili na Utalii Mhe. Dkt. Hamis Kigwangala.

Matangazo

  • No records found
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • KIKAO CHA MAPITIO YA ROBO MWAKA KWA KIPINDI CHA OKT - DES 2024 CHA (PJT MMMAM) CHAFANYIKA MKOANI SHINYANGA.

    February 28, 2025
  • RCC SHINYANGA YARIDHIA MAPENDEKEZO NANE (8) YA MATUMIZI BORA YA ARDHI.

    February 27, 2025
  • KUKAMILISHWA KWA MIRADI YA BARABARA KUTAPUNGUZA KERO KWA WANANCHI – RC MACHA

    February 26, 2025
  • WALIMU, TOENI ELIMU INAYOENDANA NA MABADILIKO YA TEKNOLOJIA -RC MACHA

    February 24, 2025
  • Angalia zote

Video

MIFUKO BANDIA ZAIDI YA ELFU 20 YAKAMATWA SHINYANGA
Video Nyinginezo

Viunganishi vya Haraka

  • Historia
  • Dira na Dhima
  • Hotuba Mbalimbali
  • Video Mbalimbali
  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Picha za Matukio
  • Miongozo na kanuni

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Mfumo wa kutuma, kupokea na kufuatilia malalamiko, mapendekezo, maulizo na pongezi
  • Ofisi ya Rais Menejimenti ya utumishi wa Umma
  • Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Boma Street, Mwanza Road

    Anuani: P.O.Box 320, Shinyanga

    Simu: +255 28 2762222

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras@shinyanga.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2018. Mkoa wa Shinyanga. Haki zote zimehifadhiwa