• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
    • eVibali |
Shinyanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Shinyanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Yetu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
      • Afya
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Shinyanga
    • Wilaya ya Kahama
    • Wilaya ya Kishapu
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu
    • Halmashauri ya Mji wa Kahama
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu
    • Halmashauri ya Wilaya ya Msalala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
    • Bandari Kavu
  • Huduma
    • Kutoa Ushauri wa Kitaalam
    • Kutafsiri Sheria na Sera
    • Kuratibu Shughuli za Wadau
    • Ulinzi na Usalama
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Tafiti
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha

VIKUNDI 19 VILIVYOKIDHI KUPATA MKOPO WA ASILIMIA KUMI MANISPAA YA SHINYANGA VYAPATIWA MAFUNZO.

Posted on: March 22nd, 2025

Repost @shinyangamanispaa

Katika Kuhakikisha jamii inaondokana na umasikini na kujikwamua kiuchumi Manispaa ya Shinyanga imetoa mafunzo kwa jumla ya vikundi (19) vya wanawake, vijana na watu wenye ulemavu, vikundi vilivyokidhi kupata mkopo wa asilimia kumi inayotolewa na Halmashauri kupitia mapato ya ndani mikopo isiyo na riba.

Akizungumza leo Machi, 22,2025 katika mafunzo haya Afisa maendeleo ya jamii kutoka Manispaa ya Shinyanga Bi. Nyanjula Kiyenze amesema jumla ya Tsh. Milion 225,879,500/= zimetengwa kwa ajili ya vikundi hivyo ambapo Kwa mujibu wa Sheria ya mwaka 2024 inatutaka kabla ya vikundi vilivyokidhi kupata mkopo havijapokea ni lazima vipate mafunzo ili kuongeza uelewa juu ya mkopo huo.

“jumla ya Tsh milioni 225,879,500/= ambapo vikundi vya wanawake ni Tsh 127,927,500/= vikundi vya vijana Milioni 123,952,000/= na Mtu mwenye ulemavu ni Tsh 4,000,000/= zimetolewa na halmashauri mikopo ya asilimia kumi isiyokuwa na riba ili vikundi hivi viweze kujikwamua kiuchumi”. Amesema Bi. Nyanjula.

Awali akifungua mafunzo haya Mstahiki Meya wa Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga Mhe. Elias Masumbuko amevisisitiza vikundi hivyo kuwa na nidhamu ya Fedha, kuwa waaminifu Katika kurejesha mikopo hiyo ili iweze kuwanufaisha wananchi wengine.

“Serikali inayoongozwa na Mhe. Rais wetu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan inafanya kila liwezekanalo Kuhakikisha makundi haya yanajikwamua kiuchumi na kuondokana na umasikini, fedha hizi ni mapato ya ndani ambayo ni Kodi za wananchi, sasa niombe kuwa na nidhamu ya fedha hizi, kuweni waaminifu Katika kurejeshe ili vikundi vingine navyo vipate kama ninyi mlivyopata. Amesema”. Mhe Masumbuko

Katika vikundi hivyo jumla ya mada (5) zimefundishwa Usimamizi wa vikundi, Utatuzi wa migogoro, Usimamizi wa biashara, Utunzaji wa kumbukumbu pamoja na Msaada wa kisheria (MSLAC) zimefundishwa kwa vikundi 19 kutoka kata 9 kati ya Kata 17 za Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga zilizokidhi kupata mkopo huo.


Matangazo

  • No records found
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • ENDELEENI KUTOA ELIMU ZAIDI KUHUSU AFYA YA AKILI - DC. MBONI

    May 30, 2025
  • TAKUKURU SHINYANGA YAANZA KUCHUKUA HATUA DHIDI YA UBADHIRIFU WA SHILINGI MILIONI 92 ZA WAKULIMA WA TUMBAKU WA USHETU - DONASIAN.

    May 27, 2025
  • MAISHA BAADA YA KUSTAAFU YANAHITAJI UTULIVU - DC. MTATIRO

    May 26, 2025
  • MAFUNZO YA IPOSA NI MKOMBOZI KWA VIJANA WALIO WENGI WANAOKOSA FURSA YA ELIMU YA KAWAIDA - RC. MACHA

    May 23, 2025
  • Angalia zote

Video

MIFUKO BANDIA ZAIDI YA ELFU 20 YAKAMATWA SHINYANGA
Video Nyinginezo

Viunganishi vya Haraka

  • Historia
  • Dira na Dhima
  • Hotuba Mbalimbali
  • Video Mbalimbali
  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Picha za Matukio
  • Miongozo na kanuni

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Mfumo wa kutuma, kupokea na kufuatilia malalamiko, mapendekezo, maulizo na pongezi
  • Ofisi ya Rais Menejimenti ya utumishi wa Umma
  • Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Boma Street, Mwanza Road

    Anuani: P.O.Box 320, Shinyanga

    Simu: +255 28 2762222

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras@shinyanga.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2018. Mkoa wa Shinyanga. Haki zote zimehifadhiwa