• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
    • eVibali |
Shinyanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Shinyanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Yetu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
      • Afya
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Shinyanga
    • Wilaya ya Kahama
    • Wilaya ya Kishapu
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu
    • Halmashauri ya Mji wa Kahama
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu
    • Halmashauri ya Wilaya ya Msalala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
    • Bandari Kavu
  • Huduma
    • Kutoa Ushauri wa Kitaalam
    • Kutafsiri Sheria na Sera
    • Kuratibu Shughuli za Wadau
    • Ulinzi na Usalama
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Tafiti
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha

"Kujitambua kwa mtoto wa kike ni chachu ya kufikia uchumi wa kati"- DC Taraba

Posted on: July 3rd, 2019

Mkuu wa Wilaya ya Kishapu Mhe. Nyabaganga Taraba amesema watoto wa kike wakilindwa na kuendelezwa ni chachu ya kufikia maendeleo ya uchumi wa kati ikiwa ni lengo la Serikali ya Awamu ya tano.

Akizungumza na watendaji na wadau wa masuala ya kuwalinda watoto, kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga leo tarehe 03/06/2019 wakati wa kikao cha kufunga miradi miwili ya kupinga vitendo vya ukatili dhidi ya watoto na vijana, iliyotekelezwa na shirika la "Save the Children kwa miaka miwili Mkoani hapa.

"Hakuna Taifa lililoendelea kama wanawake wapo nyuma" amesema Mhe. Taraba na kuwataka wadau wote kuhakikisha watoto wa kiume na wa kike wana haki ya kuendelezwa na kulelewa sawa. 

Taraba amesema kuwa, watoto sasa hivi wameachwa wanajilea wenyewe tofauti na zamani, wazazi wamekuwa mbali na wanashindwa kuongea na watoto wao hivyo kuchangia watoto na vijana wengi kushawishika kufanya matendo maovu ikiwemo ngono na hatimaye kutotimiza ndoto zao.

Amewaomba wadau kuendelea kushirikiana na Serikali kuwalinda watoto hawa, kwani bado kuna changamoto kubwa katika Mkoa wa Shinyanga hasa suala la mimba za utotoni.

Shirika la Save the Children limehitimisha utekelezaji wa miradi yake miwili, Mradi wa Ulinzi wa Mtoto na usimamizi wa utekelezaji wa Haki za Mtoto, pamoja na mradi wa kutokomeza Mila na Desturi kandamizi kijinsia ambayo imeweza kuwafikia watoto na vijana katika Halmashauri tano na vijiji 150 Mkoani Shinyanga.

                                                         Mkuu wa Wilaya ya Kishapu akizungumza na wadau wa watoto wakati wa kufunga mradi wa kulinda haki ya mtoto na vijana 

Bw. Jesse Munegezi, Mkurugenzi Msaidizi uendeshaji wa Shirika la Save the Children, akitoa taarifa ya miradi ya kupinga vitendo vya ukatili dhidi ya watoto na vijana

Washiriki wa kikao cha kufunga miradi miwili ya kuwalinda watoto na vijana wakimsikiliza Mgeni rasmi Mhe. Nyabaganga Taraba 

Washiriki wa kikao hicho wakifuatilia kwa makini mada ya video ya jinsi miradi hiyo ilivyotekelezwa

Matangazo

  • No records found
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • WANUFAIKA WA MIKOPO YA 10% LIPENI KWA WAKATI ILI PIA VIKOPESHWE NA VIKUNDI VINGINE - RC MACHA

    February 13, 2025
  • CP. HAMDUNI AKUTANA NA KAMATI YA MICHEZO YA JWTZ

    February 13, 2025
  • WANANCHI, LIPENI KODI YA ARDHI KWA WAKATI MUEPUKE RIBA - LEO KOMBA

    February 12, 2025
  • WAJUMBE WA BODI, TUMIENI TAALUMA ZENU KUISAIDIA HOSPITALI KUKAMILISHA MIRADI YA UJENZI- RAS CP. HAMDUNI.

    February 11, 2025
  • Angalia zote

Video

MIFUKO BANDIA ZAIDI YA ELFU 20 YAKAMATWA SHINYANGA
Video Nyinginezo

Viunganishi vya Haraka

  • Historia
  • Dira na Dhima
  • Hotuba Mbalimbali
  • Video Mbalimbali
  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Picha za Matukio
  • Miongozo na kanuni

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Mfumo wa kutuma, kupokea na kufuatilia malalamiko, mapendekezo, maulizo na pongezi
  • Ofisi ya Rais Menejimenti ya utumishi wa Umma
  • Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Boma Street, Mwanza Road

    Anuani: P.O.Box 320, Shinyanga

    Simu: +255 28 2762222

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras@shinyanga.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2018. Mkoa wa Shinyanga. Haki zote zimehifadhiwa