• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
    • eVibali |
Shinyanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Shinyanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Yetu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
      • Afya
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Shinyanga
    • Wilaya ya Kahama
    • Wilaya ya Kishapu
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu
    • Halmashauri ya Mji wa Kahama
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu
    • Halmashauri ya Wilaya ya Msalala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
    • Bandari Kavu
  • Huduma
    • Kutoa Ushauri wa Kitaalam
    • Kutafsiri Sheria na Sera
    • Kuratibu Shughuli za Wadau
    • Ulinzi na Usalama
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Tafiti
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha

WAFANYABIASHARA NDOGONDOGO, HAMISHIENI NGUVU KWENYE UONGEZAJI THAMANI WA MAZAO - RC MACHA.

Posted on: February 14th, 2025

Na. Paul Kasembo, SHY RS.

MKUU wa Mkoa wa Shinyanga Mhe. Anamringi Macha amewataka wafanyabiashara ndogondogo kubadilika na kuelekeza nguvu, maarifa na mitaji katika biashara mpya ya uongezaji thamani kupitia mazao (kilimo) kwani sehemu kubwa ya biashara ndogondogo zinaonekana kutokwenda kwa kasi ambayo wengi wao wanaitarajia huku akisisitiza kuwa njia rahisi, salama, ya uhakika na kweli ni kilimo.

RC Macha ameyasema hayo leo tarehe 14 Februari, 2025 wakati akizindua na kukabidhi Vitambulisho vya Kidigitali kwa Wafanyabiashara ndogondogo 172, hafla iliyofanyika katika ukumbi wa mikutano uliopo Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga na kuhudhuriwa na viongozi mbalimbali wa Serikali, Machinga  na wanachama wao ambao ndiyo walengwa wa hafla hiyo.

"Niwatake sasa wafanyabiashara ndogondogo hapa Shinyanga muanze sasa kubadilisha mwelekeo kutoka katika biashara za mazoea za hapa mjini kati, na badala yake mhamishie nguvu, maarifa na mitaji yenu katika biashara ya uongezaji thamani mazao ambapo huko mkajikite kwenye kilimo hata cha bustani kwa kuanzia," amesema RC Macha.

Akitoa mfano wa mafanikio kupitia Kikundi cha Jipage kilichopo Kata ya Kishapu, wilayani Kishapu ambao wao waliamua kuelekeza nguvu katika kuongeza thamani ya mazao kwa kulima bustani ambapo kwa mwaka 2023 walilima na kupata tikiti elfu 11 ambazo waliuza Tzs. Milioni 22 na baada ya kutoa gharama za uendeshaji walipata faida ya Milioni 11 na mwaka 2024 walilima na kupata tikiti elfu 25 zilizotoa Tzs. Mil. 75 na walipotoa gharama za uendeshaji wakabakiwa na Mil 48 kama faida.

Akitoa salamu za wanachama wake, Mwenyekiti wa Machinga Mkoa wa Shinyanga ndg. Mupinda Bwesa amemshukuru sana Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuendelea kuwajali na kuwathamini machinga ambapo pamoja na bitambulisho vya kidigitali ambavyo vinakwenda kuwasaifia sana kupata fursa, lakini pia aliwezesha kujengwa kwa Ofisi zao Mikoa yote ukiwemo na Shonyanga na sasa wanamuombea zaidi ili awndelee kuwahudumia watanzania wote wakiwemo wao machinga.


Matangazo

  • No records found
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • KIKAO CHA MAPITIO YA ROBO MWAKA KWA KIPINDI CHA OKT - DES 2024 CHA (PJT MMMAM) CHAFANYIKA MKOANI SHINYANGA.

    February 28, 2025
  • RCC SHINYANGA YARIDHIA MAPENDEKEZO NANE (8) YA MATUMIZI BORA YA ARDHI.

    February 27, 2025
  • KUKAMILISHWA KWA MIRADI YA BARABARA KUTAPUNGUZA KERO KWA WANANCHI – RC MACHA

    February 26, 2025
  • WALIMU, TOENI ELIMU INAYOENDANA NA MABADILIKO YA TEKNOLOJIA -RC MACHA

    February 24, 2025
  • Angalia zote

Video

MIFUKO BANDIA ZAIDI YA ELFU 20 YAKAMATWA SHINYANGA
Video Nyinginezo

Viunganishi vya Haraka

  • Historia
  • Dira na Dhima
  • Hotuba Mbalimbali
  • Video Mbalimbali
  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Picha za Matukio
  • Miongozo na kanuni

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Mfumo wa kutuma, kupokea na kufuatilia malalamiko, mapendekezo, maulizo na pongezi
  • Ofisi ya Rais Menejimenti ya utumishi wa Umma
  • Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Boma Street, Mwanza Road

    Anuani: P.O.Box 320, Shinyanga

    Simu: +255 28 2762222

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras@shinyanga.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2018. Mkoa wa Shinyanga. Haki zote zimehifadhiwa