• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
    • eVibali |
Shinyanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Shinyanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Yetu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
      • Afya
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Shinyanga
    • Wilaya ya Kahama
    • Wilaya ya Kishapu
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu
    • Halmashauri ya Mji wa Kahama
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu
    • Halmashauri ya Wilaya ya Msalala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
    • Bandari Kavu
  • Huduma
    • Kutoa Ushauri wa Kitaalam
    • Kutafsiri Sheria na Sera
    • Kuratibu Shughuli za Wadau
    • Ulinzi na Usalama
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Tafiti
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha

WAFANYABIASHARA NDOGONDOGO, JITOKEZENI MSAJILIWE NA KUTAMBULIKA ILI MPATE FURSA - ROSE

Posted on: January 8th, 2025

Na. Paul Kasembo, SHY RS.

AFISA Biashara kutoka Ofisi ya Mkuu Mkoa wa Shinyanga Bi. Rose Tungu amewataka wafanyabiashara dogondogo Manispaa ya Shinyanga kujitokeza kusajiliwa na kutambuliwa ili waweze kupata kadi za utambuzi kwani Serikali kupitia Halmashauri ina malengo ya kuwasaidia kwa kuwapatia mikopo maaulumu ya asilimia 7 na waweze kukuza na kuboresha biashara zao.

Ameyasema haya leo tarehe 8 Januari, 2025 wakati akitoa elimu kwa wafanyabiashara Kata ya Ngokolo Manispaa ya Shinyanga kuhusu umuhimu wa kusajiliwa kwenye mfumo ambapo pamoja na yote amesema zoezi hili litakuwa ni endelevu na tayari limeshaanza katika maeneo yote.

“Ninawahimiza wafanyabiashara wote kujitokeza kwa wingi kusajiliwa ili muweze kutambulika na kupata kadi za biashara ambapo kupitia kadi hizi mtapata fursa mbalimbali ikiwemo kupewa mikopo maalumu ya asilimia 7 ambayo itawasaidia kuboresha na kukuza biashara zenu,” amesema Bi. Rose.

Akizungumzia kuhusu sifa za kupata mikopo ya asilimia 7 Afisa Maendeleo kutoka Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Bi. Bestina Gunje amewasihi wafanyabiashara kutumia fursa hii kujitokeza kwa wingi kujisajili kwani zoezi hili ni endelevu na linalenga kuwasaidia wafanyabiashara kunufaika na mikopo hii ambayo Serikali itatoa ili kuwasaidia kuinua biashara zao hivyo kuwaepusha na mikopo yenye riba kubwa (kausha damu).

Kwa upande wake Afisa Uhusiano Benki ya NMB - Manonga ndugu Filbert Busiri amesema Serikali imetoa Shilingi Bilioni 18 kwa Benki ya NMB kwa Mkoa wa Shinyanga unatarajiwa kupokea takribani Shilingi Milioni 140 ambazo zitatolea kama mikopo Wafanyabiashara ambao tayari wamesajiliwa katika mfumo wa kidigitali na wanaofanya katika maeneo yanayotambulika.

Zoezi la Usajili wa wafanyabiashara ndogondogo lilianza tarehe 19 Februari, 2024 ambapo Serikali kupitia Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalumu ndio inaratibu zoezi hili.

Matangazo

  • No records found
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • KIKAO CHA MAPITIO YA ROBO MWAKA KWA KIPINDI CHA OKT - DES 2024 CHA (PJT MMMAM) CHAFANYIKA MKOANI SHINYANGA.

    February 28, 2025
  • RCC SHINYANGA YARIDHIA MAPENDEKEZO NANE (8) YA MATUMIZI BORA YA ARDHI.

    February 27, 2025
  • KUKAMILISHWA KWA MIRADI YA BARABARA KUTAPUNGUZA KERO KWA WANANCHI – RC MACHA

    February 26, 2025
  • WALIMU, TOENI ELIMU INAYOENDANA NA MABADILIKO YA TEKNOLOJIA -RC MACHA

    February 24, 2025
  • Angalia zote

Video

MIFUKO BANDIA ZAIDI YA ELFU 20 YAKAMATWA SHINYANGA
Video Nyinginezo

Viunganishi vya Haraka

  • Historia
  • Dira na Dhima
  • Hotuba Mbalimbali
  • Video Mbalimbali
  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Picha za Matukio
  • Miongozo na kanuni

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Mfumo wa kutuma, kupokea na kufuatilia malalamiko, mapendekezo, maulizo na pongezi
  • Ofisi ya Rais Menejimenti ya utumishi wa Umma
  • Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Boma Street, Mwanza Road

    Anuani: P.O.Box 320, Shinyanga

    Simu: +255 28 2762222

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras@shinyanga.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2018. Mkoa wa Shinyanga. Haki zote zimehifadhiwa