• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
    • eVibali |
Shinyanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Shinyanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Yetu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
      • Afya
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Shinyanga
    • Wilaya ya Kahama
    • Wilaya ya Kishapu
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu
    • Halmashauri ya Mji wa Kahama
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu
    • Halmashauri ya Wilaya ya Msalala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
    • Bandari Kavu
  • Huduma
    • Kutoa Ushauri wa Kitaalam
    • Kutafsiri Sheria na Sera
    • Kuratibu Shughuli za Wadau
    • Ulinzi na Usalama
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Tafiti
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha

Mradi mpya wa kudhibiti Kifua Kikuu watambulishwa Shinyanga

Posted on: June 29th, 2018

Watumishi wa Afya wametakiwa kutoa huduma kwa wananchi kwa moyo kwa kuzingatia maadili na kanuni za taaluma walizonazo. 

Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Mhe. Zainab Telack ametoa wito huo hivi karibuni katika kikao cha kutambulisha mradi mpya wa kudhibiti maambukizi ya Kifua Kikuu unaofadhiliwa na "Global fund".

Mhe. Telack amesema kuwa, watendaji wa afya hasa Madaktari wasiridhike na maelezo ya wagonjwa tu ni wajibu wao kufanya uchunguzi zaidi ili kuibua magonjwa yaliyojificha na kuyatafutia tiba.

"Watendaji wa afya watoe huduma kulingana na taaluma zao, wazitendee haki na rasilimali zilizopo zitumike kwa ajili ya wagonjwa" amesema Telack.

Akizungumzia mradi huo, Mkuu wa Mkoa amewashukuru waratibu na kusema kuwa, tatizo la Kifua kikuu bado ni kubwa hapa nchini kwani Tanzania ni mojawapo ya nchi 30 Duniani zenye kiwango kikubwa cha ugonjwa huu kwa kuwa na wananchi 287 kati ya 100,000 wanaougua kila mwaka.

Naye Meneja mradi wa "Global fund" Bw. John Lyimo amesema mradi huo unaoendeshwa na mradi wa "Management and Development for Health" (MDH) ni wa mwaka mmoja ambapo Wagonjwa wa Kifua Kikuu watafuatwa majumbani kwa ajili ya kupewa elimu, ushauri na uchunguzi.

Aidha, mashine 189 za uchunguzi wa ugonjwa wa Kifua Kikuu zimeshawasili nchini na tayari Mkoa wa Shinyanga unazo mashine 6.

Bw. Lyimo amesema pia kuwa, mradi utafanya kazi katika maeneo makuu manne ambayo ni Migodini, Shule za bweni, Waganga wa jadi na kwenye mikusanyiko ya watu.

Mganga Mkuu wa Mkoa Dkt. Rashid Mfaume amesema pia kuwa, ugonjwa wa Kifua Kikuu umeshamiri sana katika Migodi na shule za bweni.

Mradi huu utasaidia wagonjwa na wananchi kwa ujumla kuwapunguzia gharama za matibabu kwani mgonjwa mmoja kupona inagharimu jumla ya shilingi za Kitanzania milioni 8 hadi 9 katika utaratibu wa kawaida wa matibabu.

Matangazo

  • No records found
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • KIKAO CHA MAPITIO YA ROBO MWAKA KWA KIPINDI CHA OKT - DES 2024 CHA (PJT MMMAM) CHAFANYIKA MKOANI SHINYANGA.

    February 28, 2025
  • RCC SHINYANGA YARIDHIA MAPENDEKEZO NANE (8) YA MATUMIZI BORA YA ARDHI.

    February 27, 2025
  • KUKAMILISHWA KWA MIRADI YA BARABARA KUTAPUNGUZA KERO KWA WANANCHI – RC MACHA

    February 26, 2025
  • WALIMU, TOENI ELIMU INAYOENDANA NA MABADILIKO YA TEKNOLOJIA -RC MACHA

    February 24, 2025
  • Angalia zote

Video

MIFUKO BANDIA ZAIDI YA ELFU 20 YAKAMATWA SHINYANGA
Video Nyinginezo

Viunganishi vya Haraka

  • Historia
  • Dira na Dhima
  • Hotuba Mbalimbali
  • Video Mbalimbali
  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Picha za Matukio
  • Miongozo na kanuni

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Mfumo wa kutuma, kupokea na kufuatilia malalamiko, mapendekezo, maulizo na pongezi
  • Ofisi ya Rais Menejimenti ya utumishi wa Umma
  • Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Boma Street, Mwanza Road

    Anuani: P.O.Box 320, Shinyanga

    Simu: +255 28 2762222

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras@shinyanga.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2018. Mkoa wa Shinyanga. Haki zote zimehifadhiwa