• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
    • eVibali |
Shinyanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Shinyanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Yetu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
      • Afya
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Shinyanga
    • Wilaya ya Kahama
    • Wilaya ya Kishapu
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu
    • Halmashauri ya Mji wa Kahama
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu
    • Halmashauri ya Wilaya ya Msalala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
    • Bandari Kavu
  • Huduma
    • Kutoa Ushauri wa Kitaalam
    • Kutafsiri Sheria na Sera
    • Kuratibu Shughuli za Wadau
    • Ulinzi na Usalama
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Tafiti
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha

WAJASIRIAMALI, TUMIENI FURSA VIZURI - RC MACHA

Posted on: September 9th, 2024

Na. Paul Kasembo, SHY RS.

Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Mhe. Anamiringi Macha amewataka wajasiriamali wanaotengeneza bidhaa za ngozi katika Halmashauri ya Manispaa yq Shinyanga kutumia vizuri fursa za upatikanaji wa ngozi kutokana na machinjio ya wanyama yaliyopo Mkoa wa Shinyanga kutengeneza bidhaa nyingi zaidi na hivyo kukuza uchumi wa Taifa.

Ameyasema hayo leo tarehe 9 Septemba, 2024 wakati akifungua mafunzo ya wajasiriamali wanaotengeneza bidhaa za ngozi Manispaa ya Shinyanga ambayo yanaratibiwa na Shirika la Viwango Tanzania (TBS) yanafanyika kwa siku (2) kwenye ukumbi wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga na kuhudhuriwa na wataalam mbalimbali kutoka TAMISEMI, SIDO, TBS, wadau nk huku akisisitiza ubunifu zaidi.

“Ningependa kuwaasa mjitahidi kutumia vizuri fursa za upatikanji wa ngozi kwa sababu ndani ya Mkoa wa Shinyanga kuna machinjio ya wanyama mbalimbali kama ng’ombe, mbuzi na kondoo ambayo kupitia machinjio haya mnaweza mkapata kiasi kikubwa cha ngozi na mkafanikiwa kutengeneza bidhaa nyingi zaidi na kupata faida kubwa hatimaye kukuza uchumi wetu na Serikali pia kongeza pato lake hapo,” amesema RC Macha.

Kwa upande wake meneja wa Shirika la Viwango Tanzania (TBS) kitengo cha Tafiti na Mafunzo Mwl. Hamisi Mwanasala amesema mafunzo haya yamelenga kuwafikia wajasiriamali takribani 40 wanaojishughulisha na bidhaa za ngozi na amewataka washiriki wote kutumia vema mafunzo haya ili kuboresha bidhaa wanazozalisha ziendane na viwango vya TBS.

“Mafunzo haya yamekusudia kuwasaidia wajasiriamali wanaojishughulisha na bidhaa za ngozi takribani 40 ili waweze kuboresha  bidhaa zao za ngozi ziendane na viwango ambavyo Shirika la Viwango Tanzania limethibitisha ili kukuza soko la ngozi nchini” amesema Hamisi.

Mafunzo haya ya wajasiriamali yatafanyika kwa siku mbili kuanzia leo Jumatatu tarehe 9 Septemba, 2024 hadi Alhamis tarehe 10 Septemba, 2024 mafunzo ambayo yanatajwa kuwa yenye tija zaidi kwani yatawaongezea ujuzi na maarifa na kwenda kuchechemua uchumi wao na wa Taifa kwa ujumla.


Matangazo

  • No records found
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • KIKAO CHA MAPITIO YA ROBO MWAKA KWA KIPINDI CHA OKT - DES 2024 CHA (PJT MMMAM) CHAFANYIKA MKOANI SHINYANGA.

    February 28, 2025
  • RCC SHINYANGA YARIDHIA MAPENDEKEZO NANE (8) YA MATUMIZI BORA YA ARDHI.

    February 27, 2025
  • KUKAMILISHWA KWA MIRADI YA BARABARA KUTAPUNGUZA KERO KWA WANANCHI – RC MACHA

    February 26, 2025
  • WALIMU, TOENI ELIMU INAYOENDANA NA MABADILIKO YA TEKNOLOJIA -RC MACHA

    February 24, 2025
  • Angalia zote

Video

MIFUKO BANDIA ZAIDI YA ELFU 20 YAKAMATWA SHINYANGA
Video Nyinginezo

Viunganishi vya Haraka

  • Historia
  • Dira na Dhima
  • Hotuba Mbalimbali
  • Video Mbalimbali
  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Picha za Matukio
  • Miongozo na kanuni

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Mfumo wa kutuma, kupokea na kufuatilia malalamiko, mapendekezo, maulizo na pongezi
  • Ofisi ya Rais Menejimenti ya utumishi wa Umma
  • Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Boma Street, Mwanza Road

    Anuani: P.O.Box 320, Shinyanga

    Simu: +255 28 2762222

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras@shinyanga.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2018. Mkoa wa Shinyanga. Haki zote zimehifadhiwa