• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
    • eVibali |
Shinyanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Shinyanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Yetu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
      • Afya
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Shinyanga
    • Wilaya ya Kahama
    • Wilaya ya Kishapu
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu
    • Halmashauri ya Mji wa Kahama
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu
    • Halmashauri ya Wilaya ya Msalala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
    • Bandari Kavu
  • Huduma
    • Kutoa Ushauri wa Kitaalam
    • Kutafsiri Sheria na Sera
    • Kuratibu Shughuli za Wadau
    • Ulinzi na Usalama
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Tafiti
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha

WAKUFUNZI WA NeST MKOA WA SHINYANGA WAENDESHA MAFUNZO KWA WATAALAM

Posted on: September 13th, 2023

Na. Shinyanga RS.

WAKUFUNZI wa mfumo mpya wa ununuzi NeST kutoka Ofisi ya Mkuu Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga leo tarehe 13 Septemba, 2023 wameanza mafunzo ya mfumo huo kwa wataalam wa Ofisi ya Shinyanga RS na Hospitali ya Rufaa Mkoa wa Shinyanga kwa lengo la kuwapatia uelewa wa matumizi ya mfumo huo unaotajwa kuwa ni mwarobaini wa urasimu na ucheleweshaji katika mchakato wa kupata na kutoa huduma ya zabuni kwa wadau katika nyanja zote.

Wakizungumza kwa nyakati tofauti wakati wa ufunguzi wa mafunzo hayo Mkuu wa Kitengo cha Ugavi Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Ndg.Gervas Lugodisha na Ammy Mohmed ambaye ni Mkuu wa Kitengo cha TEHAMA wamewaeleza washiriki wa mafunzo haya kuwa Serikali imekuja na mfumo huu na kwamba sasa wataalam wanapaswa kuhama kutoka TANePS ule wa awali.

Wakufunzi wamesema kuwa awali Serikali ilikuwa ikitumia mfumo wa TANePS katika ununuzi wa Umma ambao ulibainika kuwa na changamoto, jambo ambalo lilipelekea Serikali kuja na mfumo huu wa NeST ili kuondoa  changamoto hizo kwa lengo la kuboresha utoaji wa huduma na kujikita katika matumizi ya Tehama zaidi.

Mfumo huu wa TANePS utafika ukomo wake rasmi ifikapo Septemba 30, 2023 na hivyo kutoa fursa kwa mfumo huu mpya wa NeST kuanza kutumika rasmi Octoba 1, 2023.

Aidha Taasisi hazitaruhusiwa kufanya ununuzi wowote wa umma nje ya mfumo huu mpya wa NeST, na kwamba Taasisi nunuzi ambayo itafanya ununuzi wowote bila kutumia mfumo wa NeST itakua imetenda kosa na hivyo Afisa Masuhuli wa Taasisi husika atachukuliwa hatua zinazostahili kwa mujibu wa Sheria.


Picha zikionesha baadhi ya washiriki wa mafunzo pamoja na wakufunzi wakiendelea na mafunzo ukumbi uliopo Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga. 

Ndg. Gervas Lugodisha Mkufunzi na Mkuu wa Kitengo cha Ugavi Shinyanga RS.

Ndg. Ammy Mohmed Mkufunzi na Mkuu wa Kitengo cha TEHAMA Shinyanga RS.

Picha za washiriki wakati wa mafunzo


Matangazo

  • No records found
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • WANUFAIKA WA MIKOPO YA 10% LIPENI KWA WAKATI ILI PIA VIKOPESHWE NA VIKUNDI VINGINE - RC MACHA

    February 13, 2025
  • CP. HAMDUNI AKUTANA NA KAMATI YA MICHEZO YA JWTZ

    February 13, 2025
  • WANANCHI, LIPENI KODI YA ARDHI KWA WAKATI MUEPUKE RIBA - LEO KOMBA

    February 12, 2025
  • WAJUMBE WA BODI, TUMIENI TAALUMA ZENU KUISAIDIA HOSPITALI KUKAMILISHA MIRADI YA UJENZI- RAS CP. HAMDUNI.

    February 11, 2025
  • Angalia zote

Video

MIFUKO BANDIA ZAIDI YA ELFU 20 YAKAMATWA SHINYANGA
Video Nyinginezo

Viunganishi vya Haraka

  • Historia
  • Dira na Dhima
  • Hotuba Mbalimbali
  • Video Mbalimbali
  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Picha za Matukio
  • Miongozo na kanuni

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Mfumo wa kutuma, kupokea na kufuatilia malalamiko, mapendekezo, maulizo na pongezi
  • Ofisi ya Rais Menejimenti ya utumishi wa Umma
  • Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Boma Street, Mwanza Road

    Anuani: P.O.Box 320, Shinyanga

    Simu: +255 28 2762222

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras@shinyanga.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2018. Mkoa wa Shinyanga. Haki zote zimehifadhiwa