• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
    • eVibali |
Shinyanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Shinyanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Yetu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
      • Afya
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Shinyanga
    • Wilaya ya Kahama
    • Wilaya ya Kishapu
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu
    • Halmashauri ya Mji wa Kahama
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu
    • Halmashauri ya Wilaya ya Msalala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
    • Bandari Kavu
  • Huduma
    • Kutoa Ushauri wa Kitaalam
    • Kutafsiri Sheria na Sera
    • Kuratibu Shughuli za Wadau
    • Ulinzi na Usalama
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Tafiti
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha

WAKULIMA, MSICHANGANYE PAMBA NA MAZAO MENGINE KWENYE SHAMBA MOJA - RC MACHA

Posted on: November 9th, 2024

Na. Paul Kasembo, KISHAPU DC.

MKUU wa Mkoa wa Shinyanga Mhe. Anamringi Macha amewakumbusha wakulima wa zao la pamba kuacha tabia ya kuchanganya na mazao mengine kwenye shamba moja huku akisisitiza pia juu ya umuhimu mkubwa wa kung'olea maotea kwani tupo nyuma ya wakati.


RC Macha ameyasema haya leo tarehe 9 Novemba, 2024 katika mkutano wa hadhara uliolenga kuwakumbusha wakulima wa pamba katika Kitongoji cha Mwabusiga wilayani Kishapu wakulima ambao pia wamepata elimu na ushauri wa namna bora ya kulima eneo dogo kwa tija zaidi na Balozi wa Pamba nchini ndugu Aggrey Mwanri.

"Ndugu zangu wakulima wa zao la pamba hapa Mwabusiga, niwaombe sana na kuwakumbusha kwa dhati kabisa kuacha tabia ya kuchanganya zao la pamba na mazao mengine katika shamba moja, kwa kufanya hivyo hatutaona mafanikio tarajiwa kutoka kwenye kilimo hiki na hakutakuwa na maana yoyote tena ya kulima pamba," amesema RC Macha.

Awali akitoa hamasa ya kilimo cha pamba Mwanri amesema kuwa tumekuwa tukifanya makosa makubwa sana kuchelewa kung'olea maotea na kuondoa masalia katika zao la pamba kwakuwa madhara yake ni makubwa sana ambapo amesema kwa mujibu wa utaratibu wa kilimo bora masalia na maotea hupaswa kuondolewa kabla ya tarehe 15 Septemba, 2024 na ukichelewa kufanya hivyo unazalisha pamba mapepe na isiyokuwa na ubora unaotakiwa.


"Niwaombe sana ndugu zangu Wanabusiga tuendelea kufuata ushauri na maelekezo ya wataalam wetu wa kilimo na wengine ili tuweze kuwa na kilimo bora cha kisasa ambapo utapaswa kulima eneo dogo na lenye kukuletea tija zaidi na tusichanganye mazao katika shamba moja na tung'olee maotea na kuondoa masalia kabla ya kuanza kilimo cha msimu unaofuata," amesema Mwanri.

Aidha ndg. Buluma Kalidushi ambaye ni Mkaguzi wa Pamba Kanda ya Magharibi amewataka wakulima kuzingatia Sheria ya Pamba Na. 2 ya mwaka 2001 na marekebisho yake ya mwaka 2009 iliyotengenezewa Kanuni za mwaka 2011 na hasa kanuni ya 14 kanuni ndogo (1) inaweka katazo la kustawisha na kuuza pamba itokanayo na masalia ya miti ya pamba.

Matangazo

  • No records found
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • KIKAO CHA MAPITIO YA ROBO MWAKA KWA KIPINDI CHA OKT - DES 2024 CHA (PJT MMMAM) CHAFANYIKA MKOANI SHINYANGA.

    February 28, 2025
  • RCC SHINYANGA YARIDHIA MAPENDEKEZO NANE (8) YA MATUMIZI BORA YA ARDHI.

    February 27, 2025
  • KUKAMILISHWA KWA MIRADI YA BARABARA KUTAPUNGUZA KERO KWA WANANCHI – RC MACHA

    February 26, 2025
  • WALIMU, TOENI ELIMU INAYOENDANA NA MABADILIKO YA TEKNOLOJIA -RC MACHA

    February 24, 2025
  • Angalia zote

Video

MIFUKO BANDIA ZAIDI YA ELFU 20 YAKAMATWA SHINYANGA
Video Nyinginezo

Viunganishi vya Haraka

  • Historia
  • Dira na Dhima
  • Hotuba Mbalimbali
  • Video Mbalimbali
  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Picha za Matukio
  • Miongozo na kanuni

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Mfumo wa kutuma, kupokea na kufuatilia malalamiko, mapendekezo, maulizo na pongezi
  • Ofisi ya Rais Menejimenti ya utumishi wa Umma
  • Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Boma Street, Mwanza Road

    Anuani: P.O.Box 320, Shinyanga

    Simu: +255 28 2762222

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras@shinyanga.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2018. Mkoa wa Shinyanga. Haki zote zimehifadhiwa