• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
    • eVibali |
Shinyanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Shinyanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Yetu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
      • Afya
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Shinyanga
    • Wilaya ya Kahama
    • Wilaya ya Kishapu
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu
    • Halmashauri ya Mji wa Kahama
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu
    • Halmashauri ya Wilaya ya Msalala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
    • Bandari Kavu
  • Huduma
    • Kutoa Ushauri wa Kitaalam
    • Kutafsiri Sheria na Sera
    • Kuratibu Shughuli za Wadau
    • Ulinzi na Usalama
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Tafiti
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha

WAKULIMA WA PAMBA WATAKIWA KUTUMIA NJIA ZA KITAALAM NA KULIMA KISASA ZAO LA PAMBA - MSIGWA

Posted on: May 3rd, 2025

Na. Paul Kasembo, SHY DC.

Msemaji Mkuu wa Serikali ambaye pia ni Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Ndg. Gerson Msigwa ametoa wito kwa wakulima wa zao la pamba mkoani Shinyanga kuachana na kilimo cha mazoea na kuanza kutumia mbinu za kitaalamu ili kuongeza uzalishaji na wenye tija.

Akizungumza Mei 3, 2025 katika Mkutano na Waandishi wa Habari uliofanyika katika Kijiji cha Sayu, Kata ya Pandagichiza, Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga, Msigwa alisema Serikali imedhamiria kumsaidia mkulima kwa vitendo kupitia uwekezaji mkubwa kwenye Sekta ya kilimo, ikiwa ni pamoja na kutoa zaidi ya Tzs. Mil 17 kwa ajili ya kukuza kilimo cha pamba katika Mkoa huu.

“Natoa wito kwa wakulima wote wa zao la pamba hapa mkoani Shinyanga kuanza kutumia njia za kisasa na kitaalamu ukizingatia Serikali imalenga kumtoa mkulima kutoka kwenye kilimo cha mazoea kwenda kwenye kilimo chenye tija, na ndiyo maana tumewekeza Tzs. Bilioni 17 kwa ajili ya kukuza na kuboresha kilimo, hususan zao la pamba,” alisema Msigwa.

Aliongeza kuwa Serikali imepeleka vifaa vya kupima udongo vitakavyomuwezesha mkulima kutambua aina ya udongo na mazao yanayofaa kulimwa, pamoja na vifaa vya kisasa vya umwagiliaji. Vilevile, Maafisa Ugani wameajiriwa, kupatiwa mafunzo na vifaa vya kazi ili waweze kuwahudumia wakulima kwa ufanisi zaidi.

Kwa mujibu wa Msigwa, katika msimu uliopita, uzalishaji wa pamba ulikuwa takribani tani Mil 22, ambapo kwa wastani, kila hekari ilizalisha kilo 300 pekee – kiwango ambacho ni kidogo. Kupitia msukumo, usimamizi na ufuatiliaji mzuri wa Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Mhe. Anamringa Macha na mbinu bora za kilimo, na sasa Serikali imalenga kuona uzalishaji huo ukiongezeka hatua itakayoongeza thamani ya zao hilo na kuwapa wakulima motisha zaidi.

Huu ni muendelezo wa ziara za Msigwa kama Msemaji Mkuu wa Serikali katika Mikoa akielezea umma juu ya kazi zinazofanywa na Serikali katika Mkoa husika na Taifa kwa ujumla kupitia Sekta mbalimbali



Matangazo

  • No records found
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • TUNAMPONGEZA NA KUMSHUKURU MHE. RAIS DKT. SAMIA SULUHU HASSAN KWA KUENDELEA KUJALI AFYA ZA WANANCHI

    June 23, 2025
  • TUTAENDELEA KUKABILIANA NA MABADILIKO YA TABIANCHI – RC. MACHA

    June 17, 2025
  • SERIKALI ITAENDELEA KUWALINDA WAZEE- NAIBU WAZIRI MWANAIDI

    June 15, 2025
  • SERIKALI YA MHE. DKT. SAMIA SULUHU HASSAN ITAENDELEA KUWATAMBUA, KUWATHAMINI NA KUWAHESHIMU WAZEE – RC MACHA

    June 14, 2025
  • Angalia zote

Video

MIFUKO BANDIA ZAIDI YA ELFU 20 YAKAMATWA SHINYANGA
Video Nyinginezo

Viunganishi vya Haraka

  • Historia
  • Dira na Dhima
  • Hotuba Mbalimbali
  • Video Mbalimbali
  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Picha za Matukio
  • Miongozo na kanuni

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Mfumo wa kutuma, kupokea na kufuatilia malalamiko, mapendekezo, maulizo na pongezi
  • Ofisi ya Rais Menejimenti ya utumishi wa Umma
  • Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Boma Street, Mwanza Road

    Anuani: P.O.Box 320, Shinyanga

    Simu: +255 28 2762222

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras@shinyanga.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2018. Mkoa wa Shinyanga. Haki zote zimehifadhiwa