• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
    • eVibali |
Shinyanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Shinyanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Yetu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
      • Afya
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Shinyanga
    • Wilaya ya Kahama
    • Wilaya ya Kishapu
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu
    • Halmashauri ya Mji wa Kahama
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu
    • Halmashauri ya Wilaya ya Msalala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
    • Bandari Kavu
  • Huduma
    • Kutoa Ushauri wa Kitaalam
    • Kutafsiri Sheria na Sera
    • Kuratibu Shughuli za Wadau
    • Ulinzi na Usalama
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Tafiti
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha

WALENGWA WA SASA KUWENI TAYARI KUHITIMU NA MUWAACHIE NA WENGINE WANUFAIKE PIA - RC MACHA

Posted on: November 7th, 2024

Na. Paul Kasembo, SHY RS.

Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Mhe. Anamringi Macha amewaasa walengwa wanaonufaika na Mpango wa Kunusuru Kaya Maskini (TASAF) Mkoa wa Shinyanga ambao wamefikia hatua ya kuhitimu na mpango huu kuwa tayari kuwaachia wanufaika wengine ili na wao pia wanufaike.

RC Macha ameyasema haya leo tarehe 7 Novemba, 2024 wakati akifungua Kikao Kkazi cha kujenga uelewa kuhusu utekelezaji wa mpango wa kunusuru kaya masikini kwa viongozi na waandishi wa habari Mkoa wa Shinyanga, Simiyu, Mwanza, Kagera na Geita kikao ambacho kimefanyika kwenye Ukumbi wa Mikutano uliopo Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga.

“Ndugu zangu wanahabari, malengo makubwa ya TASAF ni kuhakikisha wanawasaidia walengwa ambao watajinusuru na umaskini na msingi huu sasa, walengwa wote ambao kwa sasa wananufaika na tayari wamehitimu tayari wawe tayari kuwaachia na wengine ili nao wanufaike na mpango huu na hatimae waweze kuondokana na umaskini na mwisho wajikwamue kiuchumi wao na familia zao na ndiyo lengo hasa la Serikali,” amesema RC Macha.

Aidha RC Macha ameongeza kuwa lengo kubwa la Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan na uongozi wake ni kuhakikisha kuwa Watanzania wote wanaishi katika hali nzuri ya kiuchumi na kwa ustawi sawa na hatimaye kuondokana na umaskini.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Mfumo wa Mawasiliano TASAF Makao Makuu Ndg. Japhet Boaz amesema kuwa kufikia Juni 2024 jumla ya vikundi 60,342 Tanzania nzima vyenye wananchama 838,241 vimefanikiwa kukusanya akiba ya shilingi Bilioni 7.9 na kukopeshana shilingi Bilioni 3.2 kwa ajiri ya kuanzisha na kuendeleza miradi mbalimbali inayowaongezea kipato ili kukuza uchumi wa kaya.

Aidha ameongeza kuwa kaya za walengwa 84,674 zimepewa mafunzo ya ujasiriamali na usimamizi wa biashara na kupatiwa ruzuku ya uzalishaji ambapo mpaka sasa wameanzisha shughuli za kiuchumi zenye thamani ya shilingi Bilioni 31.3 na hivyo kufanikiwa kuhitimu kwenye mpango wa kaya maskini ili kuwapisha wengine wanufaike na mpango huu.

Matangazo

  • No records found
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • KIKAO CHA MAPITIO YA ROBO MWAKA KWA KIPINDI CHA OKT - DES 2024 CHA (PJT MMMAM) CHAFANYIKA MKOANI SHINYANGA.

    February 28, 2025
  • RCC SHINYANGA YARIDHIA MAPENDEKEZO NANE (8) YA MATUMIZI BORA YA ARDHI.

    February 27, 2025
  • KUKAMILISHWA KWA MIRADI YA BARABARA KUTAPUNGUZA KERO KWA WANANCHI – RC MACHA

    February 26, 2025
  • WALIMU, TOENI ELIMU INAYOENDANA NA MABADILIKO YA TEKNOLOJIA -RC MACHA

    February 24, 2025
  • Angalia zote

Video

MIFUKO BANDIA ZAIDI YA ELFU 20 YAKAMATWA SHINYANGA
Video Nyinginezo

Viunganishi vya Haraka

  • Historia
  • Dira na Dhima
  • Hotuba Mbalimbali
  • Video Mbalimbali
  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Picha za Matukio
  • Miongozo na kanuni

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Mfumo wa kutuma, kupokea na kufuatilia malalamiko, mapendekezo, maulizo na pongezi
  • Ofisi ya Rais Menejimenti ya utumishi wa Umma
  • Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Boma Street, Mwanza Road

    Anuani: P.O.Box 320, Shinyanga

    Simu: +255 28 2762222

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras@shinyanga.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2018. Mkoa wa Shinyanga. Haki zote zimehifadhiwa