• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
    • eVibali |
Shinyanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Shinyanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Yetu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
      • Afya
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Shinyanga
    • Wilaya ya Kahama
    • Wilaya ya Kishapu
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu
    • Halmashauri ya Mji wa Kahama
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu
    • Halmashauri ya Wilaya ya Msalala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
    • Bandari Kavu
  • Huduma
    • Kutoa Ushauri wa Kitaalam
    • Kutafsiri Sheria na Sera
    • Kuratibu Shughuli za Wadau
    • Ulinzi na Usalama
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Tafiti
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha

WALIMU FANYENI KAZI KWA BIDII NA WELEDI KUINUA UFAULU KWA WANAFUNZI – RC MACHA

Posted on: April 4th, 2025

Na. Paul Kasembo, Shy RC.

Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Mhe. Anamringi Macha amewasisitiza Walimu wa Shule za Msingi na Sekondari mkoani Shinyanga kufanya kazi kwa bidii na weledi wawapo mashuleni ili kuboresha na kuinua ufaulu kwa wanafunzi na hivyo kujiweka katika nafasi nzuri za ufaulu kitaifa kwani kwa muda mrefu mkoa hauna matokeo mazuri.

RC Macha ameyasema haya leo Aprili 4, 2025 wakati akifungua Kikao Kazi na Wadau wa Elimu mkoani Shinyanga kilichofanyika kwenye Ukumbi wa Shule ya Sekondari ya Wasichana Shinyanga, kikao ambacho kimehusisha na kuhudhuriwa na Wadau wakiwemo Walimu, Wakufunzi wa Vyuo na Viongozi wa Serikali kutoka Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga, Kishapu na Shinyanga DC.

“Ninawasisitiza sana Walimu wa Shule za Msingi na Sekondari mkoani hapa, baada ya kikao hiki muende mkafanye kazi kwa bidii na weledi muwapo mashuleni ili kuboresha na kuinua ufaulu kwa wanafunzi shuleni na hivyo kuufanya mkoa uwe kwenye nafasi nzuri za ufaulu kitaifa kwani ni muda mrefu sasa hatuna matokeo mazuri” amesema RC Macha.

Awali akimkaribisha RC Macha, Kaimu Katibu Tawala Mkoa wa Shinyanga Ndg. David Lyamongi alieleza kuwa Kikao Kazi hiki kimelenga kufanya tathmini ya elimu ya mwaka mmoja na miaka kadhaa iliyopita ili kuona ni kwa namna gani mkoa unaweza kupiga hatua na kusonga mbele kwenye sekta ya elimu.

Kwa upande Afisa Elimu Mkoa wa Shinyanga Ndg. Samson Hango akiwasilisha Taarifa ya Elimu ya mkoa ya takribani miaka 9 kuanzia mwaka 2015-2023 amesema mkoa umekuwa hauna matokeo mazuri hususani kwa Shule za Msingi na kwa baadhi ya masomo katika Shule za Sekondari, hivyo amewataka Walimu wakajitathmini na kuona namna bora ya kuboresha na kuinua ufaulu wa wanafunzi kuanzia sasa.

Aidha wadau wa elimu mkoani Shinyanga Wakuu wa Shule za Msingi na Sekondari za Serikali pamoja za kibinafsi, Maafisa Elimu Kata pamoja na viongozi wengine kwa pamoja, wameshukuru kwa uwepo wa kikao kazi hiki kwani kimewasaidia kufahamu walikotoka na wanakoelekea kwenye sekta ya elimu huku wakiahidi kwenda kuyafanyia kazi maagizo yote yaliyotolewa na RC Macha.


Matangazo

  • No records found
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • VYAMA VYA SIASA VYATARAJIWA KUSAINI KANUNI ZA MAADILI YA UCHAGUZI

    April 12, 2025
  • MANISPAA YA SHINYANGA YASHIKA NAFASI YA PILI KITAIFA KATIKA MASHINDANO YA AFYA NA USAFI WA MAZINGIRA MWAKA 2024.

    April 08, 2025
  • KLABU YA WANDISHI WA HABARI MKOA WA SHINYANGA YAFANYA MKUTANO MKUU WA WANACHAMA WAKE

    April 05, 2025
  • WALIMU FANYENI KAZI KWA BIDII NA WELEDI KUINUA UFAULU KWA WANAFUNZI – RC MACHA

    April 04, 2025
  • Angalia zote

Video

MIFUKO BANDIA ZAIDI YA ELFU 20 YAKAMATWA SHINYANGA
Video Nyinginezo

Viunganishi vya Haraka

  • Historia
  • Dira na Dhima
  • Hotuba Mbalimbali
  • Video Mbalimbali
  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Picha za Matukio
  • Miongozo na kanuni

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Mfumo wa kutuma, kupokea na kufuatilia malalamiko, mapendekezo, maulizo na pongezi
  • Ofisi ya Rais Menejimenti ya utumishi wa Umma
  • Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Boma Street, Mwanza Road

    Anuani: P.O.Box 320, Shinyanga

    Simu: +255 28 2762222

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras@shinyanga.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2018. Mkoa wa Shinyanga. Haki zote zimehifadhiwa