• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
    • eVibali |
Shinyanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Shinyanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Yetu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
      • Afya
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Shinyanga
    • Wilaya ya Kahama
    • Wilaya ya Kishapu
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu
    • Halmashauri ya Mji wa Kahama
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu
    • Halmashauri ya Wilaya ya Msalala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
    • Bandari Kavu
  • Huduma
    • Kutoa Ushauri wa Kitaalam
    • Kutafsiri Sheria na Sera
    • Kuratibu Shughuli za Wadau
    • Ulinzi na Usalama
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Tafiti
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha

Wanafunzi wa kike kuwekewa mazingira mazuri wakati wa Hedhi

Posted on: May 17th, 2018

Serikali Mkoani Shinyanga imeweka mikakati wa kuwasaidia wanafunzi wa kike waliofikia umri wa kupata hedhi kwa kuwawekea sehemu maalumu na salama za kujihifadhi wakiwa shuleni. 

Mikakati hiyo imewekwa hapo jana katika Mkutano wa uhamasishaji wa masuala ya Afya ya uzazi kwa vijana ulioandaliwa na shirika la "amref health africa" chini ya wa mradi wa "DREAMS" wenye lengo la kuboresha afya ya uzazi kwa vijana.

Washiriki wa Mkutano huo uliowahusisha Viongozi, watendaji wa Serikali na baadhi ya wadau wa masuala ya Afya ya uzazi wamesema wanafunzi wengi wa kike wanashindwa kuhudhuria masomo wanapokuwa kwenye hedhi hivyo kupelekea utoro au kuacha shule kutokana na kutokuwa na mazingira rafiki ya kujihifadhi.

Washiriki hao wameiomba Serikali kuliangalia suala hilo kwani ni moja ya changamoto inayowakwamisha baadhi ya wasichana kutimiza ndoto zao kwa kushindwa kumaliza masomo na kuishukuru "amref" kwa kwenda hadi vijijini kutoa Elimu ya Afya ya uzazi kwa vijana.

Katibu Tawala Mkoa wa Shinyanga Bw. Albert Msovela amesema suala la muhimu hivi sasa ni kuziagiza Mamlaka za Serikali za Mitaa zote Mkoani hapa, kutumia miundombinu iliyopo kutenga mazingira hayo muhimu kwa wasichana wakati maandalizi ya kuweka maeneo hayo vizuri zaidi yakiendelea.

Mikakati mingine iliyowekwa katika Mkutano huo ni pamoja na kuweka suala la kutokomeza mimba za utotoni  kuwa ajenda ya kudumu katika vikao vya ngazi zote kuanzia Mkoani.

Hali kadhalika, kuwakutanisha wadau wote wanaotekeleza Afua mbalimbali zinazofanana kuhusu Afya ya uzazi kwa vijana, ili waweze kuona namna ya kuunganisha nguvu katika kumlinda mtoto wa kike na vijana kwa ujumla.

Awali akisoma hotuba ya Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Mhe. Zainab Telack, Katibu Tawala Mkoa Bw. Msovela amesema kuwa, mradi wa DREAMS unaotekelezwa katika Halmashauri ya Wilaya ya Msalala uwe ni chachu kwa wadau wengine kuusaidia Mkoa kwa kuweka mazingira wezeshi ya kuwasaidia wasichana ili wabaki shuleni  na hatimaye watimize ndoto zao.


Matangazo

  • No records found
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • WANUFAIKA WA MIKOPO YA 10% LIPENI KWA WAKATI ILI PIA VIKOPESHWE NA VIKUNDI VINGINE - RC MACHA

    February 13, 2025
  • CP. HAMDUNI AKUTANA NA KAMATI YA MICHEZO YA JWTZ

    February 13, 2025
  • WANANCHI, LIPENI KODI YA ARDHI KWA WAKATI MUEPUKE RIBA - LEO KOMBA

    February 12, 2025
  • WAJUMBE WA BODI, TUMIENI TAALUMA ZENU KUISAIDIA HOSPITALI KUKAMILISHA MIRADI YA UJENZI- RAS CP. HAMDUNI.

    February 11, 2025
  • Angalia zote

Video

MIFUKO BANDIA ZAIDI YA ELFU 20 YAKAMATWA SHINYANGA
Video Nyinginezo

Viunganishi vya Haraka

  • Historia
  • Dira na Dhima
  • Hotuba Mbalimbali
  • Video Mbalimbali
  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Picha za Matukio
  • Miongozo na kanuni

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Mfumo wa kutuma, kupokea na kufuatilia malalamiko, mapendekezo, maulizo na pongezi
  • Ofisi ya Rais Menejimenti ya utumishi wa Umma
  • Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Boma Street, Mwanza Road

    Anuani: P.O.Box 320, Shinyanga

    Simu: +255 28 2762222

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras@shinyanga.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2018. Mkoa wa Shinyanga. Haki zote zimehifadhiwa