• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
    • eVibali |
Shinyanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Shinyanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Yetu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
      • Afya
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Shinyanga
    • Wilaya ya Kahama
    • Wilaya ya Kishapu
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu
    • Halmashauri ya Mji wa Kahama
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu
    • Halmashauri ya Wilaya ya Msalala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
    • Bandari Kavu
  • Huduma
    • Kutoa Ushauri wa Kitaalam
    • Kutafsiri Sheria na Sera
    • Kuratibu Shughuli za Wadau
    • Ulinzi na Usalama
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Tafiti
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha

WANAHABARI, TUIJENGE JAMII ISIYOKUWA NA MALARIA - MULYUTU

Posted on: January 6th, 2025

Na. Paul Kasembo, SHY RS,

MWAKILISHI wa Katibu Tawala Msaidizi Afya, Lishe na Ustawi Mkoa wa Shinyanga Mjiolojia Faustine Mulyutu amewataka wanahabari kushirikiana na Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inayoongozwa na Mhe. Rais Samia Suluhu Hassan kuhakikisha kuwa wanaijenga, kuisitawisha na kuitunza jamii isiyokuwa na maambukizi ya ugonjwa wa Malaria kwani Tanzania bila Malaria inawezekana.

Mulyutu ameyasema haya leo tarehe 6 Januari, 2025 katika Kikao Kazi cha Uhamasishaji Kampeni ya Ugawaji wa Vyandarua kwenye Kaya bila malipo, ambapo kampeni hii inatarajiwa kutekelezwa katika Halmashauri zote 6 za Mkoa wa Shinyanga huku ikitajwa kuwa zaidi ya vyandarua takribani Milioni 1.5 vyenye dawa vitawafikia wananchi lengwa.

“Ninawasihi mkatumie Kikao Kazi hiki kwenda kuijenga, kuisitawisha na kuitunza jamii isiyokuwa na maambukizi ya ugonjwa wa malaria kwani Serikali inaendelea kupiga vita ugonjwa huu ambao unarudisha nyuma kasi ya maendeleo ya nchi yetu, hivyo kupitia jukwaa hili naamini mtaenda kuwahamasisha wananchi ili kwa pamoja tuijenge Tanzania isiyokuwa na Malaria,” amesema Mulyutu.

Kwa upande wake Mdhibiti wa Wadudu Dhurifu Ofisi ya Rais - TAMISEMI Best Yoram amesema kupitia kampeni hii itaenda kuwasaidia wajumbe kuunga mkono jitihada za Serikali za kupinga malaria kwa kuielimisha jamii ili kuhakikisha kwamba asilimia 80 ya kila kaya inamiliki chandarua ili kujikinga na ugonjwa huu.

Naye Afisa Mradi - Malaria kutoka Wizara ya Afya amewasihi wajumbe kutumia jukwaa hili kuihabarisha jamii juu ya matumizi sahihi ya vyandarua kwani baadhi ya wanajamii wamekuwa na dhana potofu juu ya matumizi ya vyandarua hivyo watumie fursa hii kuisaidia jamii kuhusu umuhimu wa kutumia vuandarua vyenye dawa.

Akiwasilisha taarifa ya zoezi zima la ugawaji wa vyandarua, Afisa Mpango wa Taifa wa Udhibiti Malaria kutoka Wizara ya Afya Peter Gitanya amesema kampeni hii itasaidia kuleta vyandarua sawa sawa na idadi ya watu kwani mpaka sasa zoezi la usajili wa kaya limeshaanza na kufikia tarehe 16 Januari, 2025 vyandarua vinategemewa kuanza kusambazwa kwa wananchi ambao wameshasajiliwa.

Matangazo

  • No records found
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • KIKAO CHA MAPITIO YA ROBO MWAKA KWA KIPINDI CHA OKT - DES 2024 CHA (PJT MMMAM) CHAFANYIKA MKOANI SHINYANGA.

    February 28, 2025
  • RCC SHINYANGA YARIDHIA MAPENDEKEZO NANE (8) YA MATUMIZI BORA YA ARDHI.

    February 27, 2025
  • KUKAMILISHWA KWA MIRADI YA BARABARA KUTAPUNGUZA KERO KWA WANANCHI – RC MACHA

    February 26, 2025
  • WALIMU, TOENI ELIMU INAYOENDANA NA MABADILIKO YA TEKNOLOJIA -RC MACHA

    February 24, 2025
  • Angalia zote

Video

MIFUKO BANDIA ZAIDI YA ELFU 20 YAKAMATWA SHINYANGA
Video Nyinginezo

Viunganishi vya Haraka

  • Historia
  • Dira na Dhima
  • Hotuba Mbalimbali
  • Video Mbalimbali
  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Picha za Matukio
  • Miongozo na kanuni

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Mfumo wa kutuma, kupokea na kufuatilia malalamiko, mapendekezo, maulizo na pongezi
  • Ofisi ya Rais Menejimenti ya utumishi wa Umma
  • Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Boma Street, Mwanza Road

    Anuani: P.O.Box 320, Shinyanga

    Simu: +255 28 2762222

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras@shinyanga.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2018. Mkoa wa Shinyanga. Haki zote zimehifadhiwa