• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
    • eVibali |
Shinyanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Shinyanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Yetu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
      • Afya
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Shinyanga
    • Wilaya ya Kahama
    • Wilaya ya Kishapu
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu
    • Halmashauri ya Mji wa Kahama
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu
    • Halmashauri ya Wilaya ya Msalala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
    • Bandari Kavu
  • Huduma
    • Kutoa Ushauri wa Kitaalam
    • Kutafsiri Sheria na Sera
    • Kuratibu Shughuli za Wadau
    • Ulinzi na Usalama
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Tafiti
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha

WANAKISHAPU WALIPONGEZA JESHI LA POLISI

Posted on: May 23rd, 2024

Na. Paul Kasembo, Kishapu.

WANANCHI Wilayani Kishapu wamelipongeza Jeshi la Polisi kwa kuimarisha kazi ya kulinda raia na mali zao jambo ambalo limepelekea kuongeza mzunguuko wa fedha kwakuwa hivi sasa wanafanya kazi bila hofu na kiongeza masaa zaidi ya kutekeleza majukumu yao ambayo yanaboresha maisha yao kiuchumi.

Pongezi hizi zimetolewa tarehe 23 Mei, 2024 na wananchi mbele ya Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Mhe. Anamringi Macha wakati akifungua soko rasmi soko la Pamba katika Wilaya ya Kishapu baada ya kuanza kusikiliza na kutatua kero za wananchi, ambapo wananchi wamekiri na kupongeza kwa dhati kuwa Jeshi la Polisi limekuwa na msaada mkubwa kwao.

RC Macha Mhe. Macha kwa nyakati tofauti amekuwa akilipongeza sana Jeshi la Polisi na hususani RPC Shinyanga SACP Janeth Magomi, na wasaidizi wake wote kwa namna ambavyo anaridhishwa na utekelezaji wa majukumu yao. RC Macha amesisitiza kuwa kasoro zilizopo katika Jeshi la Polisi ni za mtu mmoja mmoja na siyo Jeshi lote na kwamba Jeshi la Polisi ni safi na utendaji kazi wake unaridhisha na hauna shaka kabisa kama ambavyo wananchi wa Kishapu walivyokiri, kuthibitisha na kupongeza wao wenyewe baada ya kuridhishwa ambapo pongezi hizi zimepokelewa na ASP Samwel Joseph, ambaye ni Operasheni Ofisa Wilaya ya Kishapu kwa niaba ya OCD.

"Kwa dhati kahisa na kwa niaba ya wananchi wenzangu tunalipongeza sana Jeshi la Polisi hapa Wilayani Kishapu, kwa kweli wanafanya kazi nzuri sana matukio hamna tena na amani sasa ipo ya kutosha muda wote kwa hili tunawapongeza sana," amesema Charles Mashenene mkazi wa Kishapu.

RC Macha anaendelea na ziara ya kukagua utekelezaji wa miradi ya maendeleo katika Halmashauri zote sita (6) na Wilaya zote tatu (3) ambapo leo anafungua msimu wa soko la pamba katika Vyama vya Ushirika vilivyopo Wilaya ya Kishapu na baadae atakagua upanuzi wa mnada wa Mhunze kisha atafanya mkutano wa hadhara kupokea, kusikiliza na kutatua kero za wananchi katika mnada wa Mhunze.

Matangazo

  • No records found
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • WANUFAIKA WA MIKOPO YA 10% LIPENI KWA WAKATI ILI PIA VIKOPESHWE NA VIKUNDI VINGINE - RC MACHA

    February 13, 2025
  • CP. HAMDUNI AKUTANA NA KAMATI YA MICHEZO YA JWTZ

    February 13, 2025
  • WANANCHI, LIPENI KODI YA ARDHI KWA WAKATI MUEPUKE RIBA - LEO KOMBA

    February 12, 2025
  • WAJUMBE WA BODI, TUMIENI TAALUMA ZENU KUISAIDIA HOSPITALI KUKAMILISHA MIRADI YA UJENZI- RAS CP. HAMDUNI.

    February 11, 2025
  • Angalia zote

Video

MIFUKO BANDIA ZAIDI YA ELFU 20 YAKAMATWA SHINYANGA
Video Nyinginezo

Viunganishi vya Haraka

  • Historia
  • Dira na Dhima
  • Hotuba Mbalimbali
  • Video Mbalimbali
  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Picha za Matukio
  • Miongozo na kanuni

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Mfumo wa kutuma, kupokea na kufuatilia malalamiko, mapendekezo, maulizo na pongezi
  • Ofisi ya Rais Menejimenti ya utumishi wa Umma
  • Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Boma Street, Mwanza Road

    Anuani: P.O.Box 320, Shinyanga

    Simu: +255 28 2762222

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras@shinyanga.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2018. Mkoa wa Shinyanga. Haki zote zimehifadhiwa